Tuesday, October 31, 2017

MBUNGE KABATI ACHANGIA MIFUKO 100 YA SARUJI SHULE YA MSINGI IGELEKE

IMG-20171028-WA0045
MBUNGE wa viti maalum, Ritta Kabati akizungumza na kamati ya shule na wazazi ambao hawapo pichani juu ya ukarabati wa shule ya Msingi Igeleke ambayo inakabiliwa na uchakavu wa majengo na miundo mbinu mibovu hali inayohatarisha afya na usalama wa wanafunzi na walimu.
Picha na Denis Mlowe
………………….
NA DENIS MLOWE, IRINGA
 
MBUNGE wa viti maalum mkoa wa,Iringa kwa tiketi ya CCM Ritta Kabati amechangia kiasi cha mifuko ya saruji 100 na siling’ibodi 100 kwa shule ya msingi Igeleke iliyoko katika manispaa ya Iringa kutokana na  uchakavu wa majengo ya shule hiyo.
 
Akizungumza na kamati ya shule na wazazi wa shule hiyo mara baada ya kufanya ukaguzi wa miundo mbinu ya shule hiyo mbunge Kabati alisema ni aibu kwa shule kongwe kama hiyo kuwa miundo mbinu mibovu ambayo inawafanya wanafunzi kukaa kwa wasi wasi.
 
 
Alisema kuwa shule hiyo licha ya kufanya vizuri katika matokeo ya mitihani majengo yake hayaendani kabisa na hali halisi ya ufaulu wa wanafunzi hivyo kwa kushirikiana na wazazi ambao wamechangia vitu mbalimbali ukarabati wa shule hiyo utaanza jumamosi wiki hii.
 
Alisema kuwa majengo ya shule hiyo yamechakaa hali ambayo inahatarisha afya na uhai wa wananfunzi kwa kuwa vumbi kwa chini hivyo kutokana na hilo atakahakikisha shule zote chakavu zinafanyiwa ukarabati uendane na ubora unaotakiwa.
 
“ Nimetembelea shule nyingi mkoani kwetu hasa za msingi kuweza kuangalia miundo mbinu na majengo yake kwa kweli hali inatisha na majengo mengi yamekuwa chakavu hivyo nitajitahidi kwa kushirikiana na wadau wa elimu kuweza kukarabati yaendane na hali ya sasa ya kuwa bora zaidi” alisema
 
Kabati aliongeza kuwa shule ya Igeleke ni moja ya shule zinazofanya vizuri katika mitihani yake lakini imeharika hovyo na inahitaji msaada wa haraka kuikarabati kwa kuwa wanafunzi wanasoma katika mazingira magumu na kudumisha elimu ya wanafunzi hao waendelee kuongoza mkoani hapa.
 
Hadi sasa Kabati amekwisha fanya ukarabati kwa shule za msingi za Azimio, Kihesa,Mtwivira na shule ya Kibwabwa ambazo alizitembelea na kubaini uchakavu mkubwa wa majengo na miundo mbinu mibaya na shule nyingine alizoahidi kuzifanyia ukarabati ni shule ya msingi Gangilonga.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More