Monday, October 30, 2017

KAIRUKI AHAIDI KUFANYIA KAZI MAOMBI YA KUONGEZEWA ENEO MGODI WA BUSOLWA

Moja kati ya shimo ambapo shughuli za uchimbaji wa madini ukiendelea kwenye mgodi wa Busolwa uliopo kata ya Nyarugusu Wilayani na Mkoani Geita.

Mkurugenzi wa Busolwa Baraka Ezekiel  Nyandu akiwa na Waziri wa Madini  Angellah Kairuki wakati alipotembelea Mgodi huo na kujionea shughuli za uzalishaji madini ya dhahabu zikiendelea.

Mitambo ya kuchenjulia dhahabu kwenye mgodi wa Busolwa.
Waziri wa Madini  Angellah Kairuki akipatiwa maelekezo na moja kati ya wataalam wa mgodi wa Busolwa namna ambavyo mtambo wa kuchenjua dhahabu umekuwa ukifanya kazi.
Msafara ukiwa kwenye eneo la kumwagia maji machafu kwenye Mgodi wa Busolwa.
Bwawa la  kumwagia maji machafu ndani ya mgodi wa Busolwa.
Waziri wa madini Angellah Kairuki akitoka ndani ya mgodi wa Busolwa akiwa ameongozana na Mwenyekit wa chama cha mapinduzi Mkoani Geita,Joseph Kasheku Msukuma.


 PICHA NA MADUKA ONLINE.


Kampuni ya uchimbaji madini ya dhabau ya Busolwa  imemuomba waziri wa Madini, Angellah Kairuki kuwaongezea eneo la ukubwa wa kilomita 3.0 kutoka eneo jirani la uchimbaji ili kuweza kuongeza ufanisi zaidi kwenye shughuli za uchimbaji.

Hayo yameelezwa na meneja uzalishaji wa Mgodi huo, Felix Aldof  wakati wa ziara ya Waziri wa madini na naibu wake, ambapo alisema  kuwa udogo wa eneo la kufanyia kazi ni sababu kubwa kwa baadhi ya wachimbaji wadogo kuingia kwenye mgodi huo hali inayohatarisha shughuli za uchimbaji madini.

“Kampuni ya busolwa mining inayomiliki leseni namba ML 531/2014 inaomba iongezewe eneo la ukubwa wa  kilomita za mraba 3.0 kutoka eneo jirani na eneo letu la uchimbaji ili tuweze kuongeza ufanisi zaidi ifikishe ukubwa wa kilomita za mraba 3.53”Aliomba Felix.

Kutokana na maombi hayo Naibu waziri wa madini,Stanslaus  Haroon Nyongo,ameupongeza mgodi huo kutokana na uzalendo na kumilikiwa na watanzania huku akiwataka kuendelea na moyo wa kujitolea na kwamba utakuwa ni mgodi wa mfano kwa wengine kutokana na shughuli ambazo unafanya ikiwemo kusaidia jamii inayouzunguka.

Aidha kwa upande wake Waziri wa madini Angellah Kairuki ,ameahidi kushughulikia maombi yao na kwamba wawaachie nafasi wakaae ili wataalam waweze kupitia maombi hayo na muda sio mrefu watawarudishia majibu.

Pamoja na hayo ameushukuru Mgodi huo kwa kuajiri asilimia tisini na tisa ambao ni Watanzania na mchango ambao wameutoa zaidi ya Tsh Bilion  9.5 ambazo zimelipwa kwa serikali kama kodi na tozo mbalimbali.



0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More