12.00
Mwenyekiti
chama
cha walimu wa Tanzania (CWT) wilaya ya Mufindi Obi Kimbale akizungumza
na waandishi wa habari wakati wa mkutano mkuu wa chama cha walimu
Tanzania (CWT) wilaya ya Mufindi mkoani Iringa.
Baadhi ya walimu waliohudhuria mkutano mkuu wa chama hicho wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa.
Na
Fredy Mgunda,Mufindi
Chama
cha walimu Tanzania (CWT) wilaya ya Mufindi mkoani Iringa kimeitaka serikali ya
jamhuri ya muungano wa Tanzania kutatua changamoto za walimu ili kukuza na
kuboresha sekta ya elimu ambayo ndio kiungo muhimu katika maendeleo ya nchi
yoyote duniani.
Akizungumza
wakati wa mkutano mkuu wa chama hicho mwenyekiti wilaya ya Mufindi Obi Kimbale
aliitaka serkali kulipa madeni wanayoidaiwa...