Friday, July 8, 2016

Majambazi Yateka Kijiji Kwa Masaa Matatu Mkoani Kagera

MAJAMBAZI wanne wamevamia kijiji cha Benaco kilichopo katika Wilaya ya Ngara mkoani Kagera kwa muda wa saa tatu ambapo wamefanikiwa kupora Sh milioni 2.4 na simu ambazo hazikujulikana idadi yake kwa mfanyabiashara mmoja wa huduma ya M-Pesa.

Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Kagera ambaye pia ni ofisa upelelezi wa polisi mkoa huo, Abel Mtagwa, alisema kuwa tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia jana ambapo majambazi hao walikuwa na silaha moja ya kivita aina ya SMG.

Alisema kuwa wakati majambazi wakijiandaa kuondoka eneo hilo walimpiga risasi mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya sekondari ya Gankabo Wilayani Kibondo mkoani Kigoma aliyetambuliwa kwa jina la Nelson Simon (15) na kumjeruhi mguu wake wa kulia. Mwanafunzi huo amelazwa katika hospitali teule ya Murgwanza iliyopo wilayani humo

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More