Wednesday, February 10, 2016

Diwani wa kata ya Nduli Basher mtove apata ufadhiri wa kujengewa shule ya sekondari katika kata yake.



 Diwani wa kata ya nduli Bashir Mtove akiwa kwenye harakati za kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa shule ambayo itajengwa kwa ufadhili wa kanisa la Orthodox


 Diwani wa kata ya nduli Bashir Mtove akiwa askofu  mkuu wa kanisa la Orthodox Tanzania   Dimitrios  Zachalegas
 picha baadhi ya vongozi waliokuwa wamehudhuria katika eneo hilo la kuweka jiwe la msingi la shule itakayojengwa kwa ufadhili wa kanisa la Orthodox

Na Esta Malibiche Majira
Iringa
 Diwani wa kata ya Nduli   Basher mtove amewashukuru  wafadhiri kutoka kanisa la Orthodox kwa kujitolea kujenga shule ya sekondari  pamoja na maabara,na kuwataka waendelee kuisaidia serikali bila kuchoka.

Alisema baada ya kuona adha  kubwa kutembea kwa  umbali  zaidi ya kilomitre 7 kwenda kupata elimu ya sekondari nduli ailiamua kuomba eneo  kwa ajili ya ujenzi kwa kushirikiana na wananchi baada ya kupewa akaanza kutafuta wafadhili ambao ni wadau wa elimu ndipo kanisa la Orthodox lilikubali kubeba majukumu kujitolea kujenga.

 “”Ninapenda kuushukuru uongozi wa kanisa la Orthodox  kupitia Askofu Tanzania kwa kukubali kufadhiri ujenzi wa madarasa na maabara ya shule ya sekondari na kutoa msaada wa chakula na vifaa vya shule katika kata yangu’’.alisema 

Alisema  kutokana na  kukithiri kwa  kwa vitendo vya ubakwaji kwa watoto wa kike na kupata mimba za utotoni  kwasababu ya umbali, shule hiyo itasaidia kutatua changamoto hiyo iliyokuwa inawasumbua kwa muda mrefu.

Diwani huyo aliishukuru serikali ya mkoa na wilaya kwa kushirikiana pamoja kutafuta eneo  kwa ajili ya zoezi hilo  na hatimae wakafanikiwa kupata  eneo lenye kilomita 17  ambalo lilitolewa na Shafii Haji mkazi wa mkoa wa  Iringa.

Naye askofu  mkuu wa kanisa la Orthodox[Irinoupolis  Tanzania   Dimitrios  Zachalegas amewataka wadau wa maendeleo nchini wametakiwa   kujitoa katika shuguli za maendeleo  kwa kuwekeza katika sekta mbalimbali ili kuleta chachu katika maendeleo nchini.

 Akizungumza na wananchi wa kijiji cha mgongo kata ya Nduli wilaya ya Iringa katika hafla fupi ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa shule ya sekondari inayojengwa chini ya   ufadhiri wa kanisa hilo .

Dimitrios alisema kutokana na kuona umuhimu  wa Elimu kwa watoto nchini kanisa hilo limejitolea kuunga juhudi za serikali kujenga shule ya sekondari katika eneo la Mtagala katikakati ya kijiji cha Mgongo   ili  wananchi wanaozunguka waweze kunufaika na wanafunzi waweze kupata Elimu  kwa uraisi zaidi. 

Alisema shule hiyo inatakiwa kujengwa muda wa miezi sita tu pamoja na maabara kuanzia sasa ili kuendana na kasi ya serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wake Dr. John.Pombe Magufuli kuhusu utekelezaji wa Elimu ya msingi na sekondari bila malipo.

Askofu alisema kuwa kwa mkoa wa Iringa kanisa hilo limeweza kujenga shule 4 za sekondari ikiwemo hiyo inayotarajiwa kujengwa katika kata ya nduli kijiji cha Mgongo 

‘’Tumejenga shule ya sekondari Ilolasimba,Kidamali,St.Marcus,Dimitris   pamoja hii tunayotarajia kuanza ujenzi hivi punde na tutaendelea kuisaidia serikali kutoa huduma tofauti katika jamii kulingana na mahitaji ya eneo husika’’ Alisema 

Pamoja na uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa shule ya sekondari viongozi hao waligawa msaada wa chakula tone tatu,sawa na  gunia 30 yenye tamani ya 1754500 kwa wananchi wa kijiji cha na kusema kuwa  serikali haiwezi kujitoa kwa kila kitu kuwakilimia wananchi bali mashirika na asasai zisizo za serikali zinapaswa kutoa michango yao katia jamii na kuachana na dhana ya kuiachia serikali pekee.

Aidha alitoa msaada wa daftari kwa wanafunzi,begi za kubebea daftari ,viatu aina ya yeboyebo kwa kila motto,biscuit .pipi pamoja na kutoa huduma ya afya kwa kuwatibu wagonjwa ambao walifika kupokea msaada wa chakula na wakapata matibabu.

Akitoa neno la shukrani kwa uongozi wa kanisa hilo Diwani wa kata ya Nduli   Basher mtove alisema ninawashukuru  wafadhiri kutoka kanisa la Orthodox kwa kujitolea kujenga shule ya sekondari  pamoja na maabara,na kuwataka waendelee kuisaidia serikali bila kuchoka.

Alisema baada ya kuona adha  kubwa kutembea kwa  umbali  zaidi ya kilomitre 7 kwenda kupata elimu ya sekondari nduli ailiamua kuomba eneo  kwa ajili ya ujenzi kwa kushirikiana na wananchi baada ya kupewa akaanza kutafuta wafadhili ambao ni wadau wa elimu ndipo kanisa la Orthodox lilikubali kubeba majukumu kujitolea kujenga.

 “”Ninapenda kuushukuru uongozi wa kanisa la Orthodox  kupitia Askofu Tanzania kwa kukubali kufadhiri ujenzi wa madarasa na maabara ya shule ya sekondari na kutoa msaada wa chakula na vifaa vya shule katika kata yangu’’.alisema 

Alisema  kutokana na  kukithiri kwa  kwa vitendo vya ubakwaji kwa watoto wa kike na kupata mimba za utotoni  kwasababu ya umbali, shule hiyo itasaidia kutatua changamoto hiyo iliyokuwa inawasumbua kwa muda mrefu.

Diwani huyo aliishukuru serikali ya mkoa na wilaya kwa kushirikiana pamoja kutafuta eneo  kwa ajili ya zoezi hilo  na hatimae wakafanikiwa kupata  eneo lenye kilomita 17  ambalo lilitolewa na Shafii Haji mkazi wa mkoa wa  Iringa. 

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More