Thursday, May 31, 2018

WACHEZAJI NA WATUMISHI WA KLABU YA SINGIDA UNITED FC WAPEWA MIFUKO 50 ya CEMENT KILA MMOJA

Akizungumza na vyombo vya habari hiii leo,Mkurugenzi wa Singida United Ndg. Festo Sanga @sanga_nation amesema, Uongozi wa klabu kuanzia chini ya Rais na mwenyekiti wa timu hiyo wameamua kutoa mifuko ya Cement kwa kila mchezaji na mtumishi wa klabu hiyo kama shukrani na pongezi kwa namna walivyopambana kufanikisha sehemu ya malengo ya klabu kwa msimu wa 2017/2018.

Tukio hilo ambalo kama sila kwanza hapa nchini, basi ni tukio la heshima na upendo wa hali ya juu katika kuimarisha mahusiano ya klabu na wachezaji, Singida United imetoa mifuko hiyo kama alama katika maisha ya wachezaji na watumishi kwamba katika maisha ya soka kuna maisha mengine ya kuanza kujitegemea mapema.

Tayari wachezaji na Watumishi wameshachukua mifuko hiyo kwaajili ya ujenzi wa makazi yao huko makwao.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More