Thursday, May 31, 2018

MBUNGE RITTA KABATI AWATEMBELEA WAFUNGWA WA GEREZA LA WILAYA YA IRINGA NA KUTOA MISAADA MBALIMBALI


 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati  akiwa na viongozi mbalimbali wa chama cha mapinduzi (CCM) mkoa wa Iringa pamoja viongozi wa gereza la Iringa alipoenda kutoa sadaka ya tende,pesa taslimu kiasi cha shilingi laki saba (700,00) na msaada wa mataulo maalumu kwa wafungwa wa Gereza manispaa ya Iringa kwa ajili wanawake kuyatumia wakati wakiwa katika kipindi cha hedhi

NA FREDY MGUNDA,IRINGA.

MBUNGE wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati ametoa sadaka ya tende,pesa taslimu kiasi cha shilingi laki saba (700,00) na msaada wa mataulo maalumu kwa wafungwa wa Gereza manispaa ya Iringa kwa ajili wanawake kuyatumia wakati wakiwa katika kipindi cha hedhi.


Akizungumza na waandishi wa habari mbunge Ritta Kabati alipowatembelea wafungwa wa Gereza la wilaya ya Iringa alisema kuwa lengo la kwenda kuwatembelea wafungwa ni kwenda kuzijua changamoto ambazo wamekuwa wanakabiliana nazo wakiwa kifungoni.

“Mimi nimekuwa muumini mkubwa sana kwa kujihusisha na maswala ya kijamii hivyo hii leo sio mara yangu ya kwanza kuja hapa Gerezani nimekuja mara nyingi na nimesikiliza kero nyingi na ndio maana zimekuwa zikitatuliwa mara kwa mara kwa kuwa huwa nawasemea vizuri nikiwa bungeni kwenye kuchangia hoja” alisema Kabati

Kabati alisema kuwa licha ya kuwa anakwenda kuwatembelea mara kwa mara lakini huwa anabeba zawadi kwa ajili ya wafungwa,hata hivyo alifanikiwa kutoa zawadi ya sadaka ya tunda la tende kwa ajili ya wafungwa waislamu ambao wamefungwa katika gereza  hilo.

“Huu ni mwezi mtukufu hivyo nimeamua kuja na tende hizi angalau na wafungwa waislamu na wapate tunda hilo ambalo waislamu wengi wamekuwa wakilitumia wakati mfungo wa ramadhani na huu ndio wakati sahihi ndio maana nimefanya hivyo” alisema Kabati

Aidha Kabati alisema kuwa ametoa msaada wa mataulo maalum kwa wafungwa wanawake kwa ajili ya kuwayatumia wakati wakiwa kwenye kipindi hedhi pamoja na kuchangia kiasi cha shilingi laki saba (700,00) pesa taslimu.

“Mimi ni mwanamke hivyo najua mahitaji yetu sisi akina mama hivyo msaada wangu huu wa haya mataulo maalum utaweza kuwasaidia kwa kipindi ambacho wapo Gerezani kwa kuwa wanaweza kuyatumia na kuyafua na kuendelea kutumia tena na pesa ambazo nimetoa nyingine zilikuwa ahadi za msimu ulipita nilipokuja kutelea hapa hivyo nimetoa hizo pesa pamoja na kuwaongeza nyingine” alisema Kabati

Kabati aliwapongeza viongozi wa gereza hilo kwa kuanzisha kiwanda kidogo ndani ya gereza hilo na kuwanya wafungwa kuongeza ujuzi na wengine kuendelea kukuza vipaji vyao wakiwa gerezani.

Naye mwenyekiti wa Jumuiya ya wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) mkoa wa Iringa
Nicolina Lulandala alimpongeza MBUNGE wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati kwa kujitoa kuisaidia jamii ambayo imekuwa ikikumbana na changamoto nyingi.

“Toka jana juzi na siku zilizopita watanzania na wanairinga tumeshuhudia shughuli anazozifanya huyu mbunge hivyo ni lazima sisi cha viongozi wa chama kumuunga mkono kwenye juhudi zake maana tusipofanya hivyo tutamkatisha moyo wa kujitolea kama ambavyo anafanya sasa” alisema Lulanda


Lulanda aliwapongeza pia viongozi wa gereza kwa kuanzisha kiwanda kidogo ndani ya gereza kitu ambacho kinaongeza ufanisi wa kazi kwa wafungwa na kuendelea kukuza vipaji vyao na kuibua pia vipaji vipya ndania ya gereza.

“Mimi na wezangu ambao tumefika hapa gerezani tumefurahi sana kitendo cha kuona kuwa kuwa kunakiwanda cha kutengeneza vikapu fagia na vitu vingine kweli nimefarijika ndio maana tukashawishi hata kuvinunua bidhaa ambazo wanazingeneza ambazo zinaubora mzuri kweli” alisema Lulanda

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More