Wednesday, May 30, 2018

PDF WAWATAKA WAZAZI KUKABILIANA NA CHANGAMOTO ZA MTOTO WA KIKE KATIKA HEDHI


Diwani wa kata ya Mtambula, Isack Kilamlya akitoa neno kwa wazazi na wanafunzi juu ya kutambua na kutoa elimu juu ya hedhi na jinsi ya kujihifadhi kwa watoto wakati wa maadhimisho ya siku ya hedhi duniani
Afisa mradi wa shirika lisilo la kiserikali la peoples development forum (PDF) ambalo linafadhiwa na UNICEF 
upande wa usafi wa mazingira lishe bora watoto Adventina Lazaro akitoa neno kwa wazazi na wanafunzi juu ya kutambua na kutoa elimu juu ya hedhi na jinsi ya kujihifadhi kwa watoto wakati wa maadhimisho ya siku ya hedhi duniani


 Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Mwesa wakiwa na mabango yakiwa na maandishi yaliyoandikwa kwa maneno tofauti tofauti wakatika maadhimisho ya siku ya hedhi duniani
 Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi ya Mwesa  wakitengeneza pedi za asili kwa kuonyesha kuwa sio lazima kununua dukani bali waweza kutengeneza hata nyumbani kwako na zikakustili vizuri tu

NA FREDY MGUNDA, MUFINDI IRINGA.

SHIRIKA lisilo la kiserikali la peoples development forum (PDF) ambalo linafadhiwa na UNICEF mkoani Iringa wilaya ya Mufindi limelenga kuwawezesha wasichana kutimiza ndoto za maisha yao kwa kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazowafanya wabaki nyuma katika kuhudhuria masomo kipindi wakiwa katika hedhi. 

Hayo yamezungumzwa na afisa mradi wa shirika lisilo la kiserikali la peoples development forum (PDF) upande wa usafi wa mazingira lishe bora watoto Adventina Lazaro wakati wa maadhimisho ya siku ya hedhi Duniani ambapo wilaya ya Mufindi yalifanyika katika shule ya msingi Mwesa kata ya Mtambula,tarafa ya Kasanga lakini kimkoa yalifanyika kwa mara ya kwanza katika Bustani za Manispaa na kuhudhuriwa na wanafunzi wa kike kutoka shule mbalimbali za sekondari za mjini hapa

Lazaro alisema kuwa changamoto kubwa ambayo wanakabiliana nayo watoto wa kike wengi walioko mashuleni ni kipindi cha hedhi ambapo baadhi yao wamekuwa hawana elimu, kutojiamini na utoro mashuleni wanapokuwa kwenye vipindi vya hedhi hali inayosababisha utoro. 

lazaro alisema kuwa ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha kuwa mtoto wa kike anahudhuria masomo yake kwa mwaka mzima pasipo kuwa na vikwazo vinavyosababishwa ama na mazingira duni au ukosefu wa bajeti katika kupata taulo hizo maalum za hedhi. 

Aliwataka wadau na wananchi kwa ujumla kuvunja ukimya juu ya suala la hedhi salama kwa mtoto wa kike na kuwezesha mtoto wa kike kupata taulo maalum kila mwezi na mkoa wa Iringa una mkakati maalum wa kumaliza changamoto hizo. 

“Changamoto mbalimbali zinazowakabili wasichana wanapokuwa kwenye vipindi vya hedhi yanapaswa kujadiliwa na kutafutiwa ufumbuzi wa kudumu kwa kuwa yanachangia kurudisha nyuma jitihada za kuwainua watoto wa kike nchini na kuwataka mabinti kuondoka na aibu ya katika suala la hedhi hivyo mkakati upo kumaliza kwa kuwapatia bure mataulo maalum watoto wa kike” alisema lazaro 

Alisema kuwa serikali ya awamu ya tano inayo dhamira ya dhati kuhakikisha elimu bure inapatikana kwa jinsia zote hivyo basi suala la hedhi salama kwa wa kike ni jambo la msingi katika ngazi ya familia, jamii, na hata mashuleni kuwapatia elimu itakayowezesha kuwa na ufahamu wa masuala ya hedhi.

Awali diwani wa kata ya Mtambula, Isack Kilamlya alisema kuwa lengo la maadhimisho hayo ni kuvunja ukimya juu ya masuala ya hedhi ikiwemo kuondokana na dhana potofu kwamba hedhi ni ugonjwa pamoja na namna bora ya kuhakikisha mtoto wa kike anajiweka katika hali ya usafi ili abaki shuleni badala ya kukosa masoko kila apatapo hedhi. 

Kilamlya Alisema ukosefu wa mazingira bora kama vyoo, maji safi na salama pamoja na vyumba mahsusi vya kubadilishia nguo, hasa kwa watoto wa kike wanapokua katika hedhi mashuleni kuna changia utoro. 

“Hakuna vikwazo zaidi wezesha wanawake na wasichana kupata hedhi salama hivyo wananchi wanapaswa kutoa ushikiano kwa shirika hilo lina mikakati ya kuwezesha watoto wa kike kupata elimu kwa mtoto kike kama wanafunzi wengine na kuhudhuria masomo yake akiwa huru” alisema Kilamlya

Akisoma risala kwa mgeni rasmi Adili Mlema mwanafunzi wa darasa la sita katika shule ya msingi ya Mwesa alisema kuwa analishukuru shirika lisilo la kiserikali la peoples development forum (PDF) ambalo linafadhiwa na UNICEF kutoa elimu ya maswala ya hedhi ambayo sasa yamekuwa msaada kwa wanafunzi wa shule hiyo.

Mlema aliongeza kwa kuwataka wazazi na viongozi mbalimbali wa serikali na wasio wa serikali kutoa elimu ya hedhi kwa jamii husika ili kuondoa aibu ambayo wazazi wengi wanayo katika kuwaeleza watot wao wa kike.

“Bila shirika lisilo la kiserikali la peoples development forum (PDF) hadi leo hii tungekuwa hatuna elimu ya maswala ya hedhi ambapo wanafunzi wengi walikuwa wanaona aibu kuja shule siku wakiwa katika siku za hedhi” alisema Mlema

Naye mmoja wa wazazi aliyehudhulia siku ya hedhi wilaya ya Mufindi Emeliziena Danda aliwataka wazazi kutoa elimu juu ya hedhi kwa watoto wa kike wanakaribia kuvunja ungo ili wajue elimu hiyo.

“Nawapongeza sana shirika lisilo la kiserikali la peoples development forum (PDF) kuwa kututoa aibu wananchi kwa kutuambia ukweli ambao leo hii tumekuwa huru kuwaambia watoto wenu na watoto wetu nao wamekuwa huru kutuambia nini kinachiwatokea” alisema Danda.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More