Tuesday, May 29, 2018

MBUNGE RITTA KABATI ATOA SADAKA YA TENDE KWA WAUMINI WA DINI YA KIISLAM MANISPAA YA IRINGA


 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringakupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati akiongea na viongozi wa misikiti yote ya manispaa ya Iringa wakati wa utoaji sadaka ya tende kwa waumini wa dini ya kiislamu wa manispaa ya Iringa kwa ajili ya kuadhimisha mfungo wa ramadhan kwa waislamu wa wote wa manispaa ya Iringa. 


 Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza amemshukuru mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati kwa kutoa sadaka ya tunda la tende kwa waiislamu katika  kipindi hiki cha mfungo wa ramadhan.
 Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza akikabidhi tende alizokabidhiwa na mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringakupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati kwa kutoa sadaka  kwa waiislamu katika  kipindi hiki cha mfungo wa ramadhan.
Mkuu wa walimu na msimamizi wa misikiti ya Dhinureyn Tanzania Abdul Salam Ahmad Ayub akimshukuru mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati kwa sadaka aliyoitoa kwa waislam katika kipindi hiki cha mfungo wa Ramadhan.
Baadhi ya viongozi wa chama cha mapinduzi (CCM) na viongozi wa misiki ya manispaa ya Iringa walipohudhulia zoezi la utoaji wa sadaka ya tende ilitolewa na mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringakupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati

NA FREDY MGUNDA,IRINGA.

MBUNGE wa viti maalum mkoa wa Iringakupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati ametoa sadaka ya tende kwa waumini wa dini ya kiislamu wa manispaa ya Iringa kwa ajili ya kuadhimisha mfungo wa ramadhan kwa waislamu wa wote wa manispaa ya Iringa

Akizungumza wakati wa kukabidhi sadaka hiyo katika msikiti wa Dhinureyn Gangilonga Kabati alisema kuwa kila mwaka amekuwa akifutulisha katika maeneo mbalimbali hivyo mwaka huu ameamua kununua tende na kugawa kwenye misikiti yote ya manispaa ya Iringa.

“Unajua mwaka huu tende ni tunda ambalo linahitajika katika kipindi hiki cha mfungo na kuna watu ambao hawana uwezo wa kununua tende hizi na ukiangalia mwaka huu tende zimepanda bei sana hivyo kwa kiasa ambacho nakipata nimeamua kutoa sadaka hii kwa waumini wa kiislam” alisema Kabati

Kabati aliwataka wananchi wengine kuendelea kumuabudu mwenyezi mungu pale ambapo tunapata nafasi ili kupunguza maovu ambayo tumekuwa tukiyatenda kwa kukusudia au bila kukusudia na kufanya hivyo basi mwenyezi mungu atatuongezea pale ambapo tumepunguza kwa ajili ya kumtumiaka mungu.

“Katika kipindi hiki nawaomba wazazi,walezi na viongozi wetu naomba tutoe elimu kwa vijana wetu kwa kuwapa elimu ya dini pamoja maadili ya nchi yetu kwa lengo la kuwajenga vijana wawe wanamcha mungu hasa kipindi hiki cha mfungo wa ramadhan” alisema Kabati

Kabati alisema kuwa ametoa sadaka ya tende tani mbili ambayo ipo katika halmashauri ya manispaa ya Iringa kwa ajili ya misikiti yote na vituo vya watoto yatima ambavyo vinawatoto wa kiislam ambao wanafunga katika kipindi hiki cha mfungo.

“Mimi nimeleta tani mbili ili kuongezea nguvu wafungaji wa kipindi hiki lakini kutoa sadaka kwa mwenyezi mungu katika kipindi ambacho waislamu wapo kwenye mfungo wa ramadhan nakuwasidia wale ambao hawana uwezo wa kununua tunda hili la tende” alisema Kabati

Kwa upande wake mgeni rasmi Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza amemshukuru mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringakupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati kwa kutoa sadaka ya tunda la tende kwa waiislamu katika  kipindi hiki cha mfungo wa ramadhan.

“Tunashukuru sana kwa sadaka hii ambayo umetusaidia kwa waislam wa manispaa ya Iringa kwa msaada wako ambao utasiadia kwa wale ambao wanamahitaji maalumu na mungu atakuongezea aple ulipopunguza na mungu akubariki” alisema Masenza

Masenza aliwaomba maimamu kuwagawia tende hizo waislam ambao hawana uwezo wa kununua tende tukani ili nao wapate hiki chakula cha kwanza pindi unapofungua na wale wenye uwezo wa kununua tende dukani basi waendelee kununua

Naye mkuu wa walimu na msimamizi wa misikiti ya Dhinureyn Tanzania Abdul Salam Ahmad Ayub alisema kuwa msaada aliotoa mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringakupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati utawasaidia waislam waliofunga.

“Sadaka hii aliyoitua huyu mbunge Kabati umekuja wakati muafaka na umamanufaa makubwa sana kwa waislam kwa kuwa tumehimizwa kufuturu kwanza tende hivyo kwa muislam kula tende ni fadhila kubwa sana”alisema Ayub

Ayub alisema kuwa katika kipindi hiki cha mfungo waislam tunatakiwa kupeana vyakula ili kila mtu ambaye hana kitu aweze kupata chakula na ndio alivyofanya huyu mbunge Ritta Kabati kwa waislam wa manispaa ya Iringa.

“Zamani watu walikuwa wanatandika jamvi nje wakati wa kufutulu ili waweze kufutulu na waislam ambao hawana uwezo na ndio uzalendo wenyewe huo,hivyo tunamuombea mbunge huyu aendelee na moyo huo huo” alisema Ayub

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More