Wednesday, January 27, 2016

Hakimu Agoma Kujitoa Kesi ya Kulawiti

Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Said Mkasiwa amekataa kujitoa katika kesi ya kulawiti na kutuma picha kwenye mitandao ya kijamii inayowakabili washitakiwa Erick Kassira (39) na Juma Richard (31).

Mkasiwa alisema sababu zilizotolewa na washitakiwa hao kwamba wanatishwa na kulazimishwa kesi isikilizwe wakiwa wanaumwa, si za kisheria ambazo zitamfanya asiendelee kusikiliza shauri hilo.

Wakitoa pingamizi jana, washitakiwa hao walidai kuwa hakimu huyo anawalazimisha kusikiliza kesi wakiwa wanaumwa na kwamba anawakataa wadhamini ambao washitakiwa hao waliwapeleka mahakamani hapo.

Mshitakiwa Kassira alidai kuwa Januari 4, mwaka huu alimuandikia barua Hakimu huyo kumuomba asiendelee kusikiliza kesi hiyo, badala yake achague mwingine atakayeweza kusikiliza. 

Alidai kuwa hawana imani na hakimu huyo kwa kuwa anawapendelea zaidi upande wa mashitaka na kushindwa kuwasikiliza.

Hata hivyo, Hakimu huyo aliwaeleza washitakiwa hao kuwa sababu walizozitoa sio za kisheria na kwamba ataendelea kusikiliza shauri hilo. 

Wakati huo huo, shahidi wa tano katika kesi hiyo, Tegemea Chaula (52), mkazi wa Kiwalani na mhudumu wa nyumba ya kulala wageni ya Maembe iliyopo Yombo Kiwalani, alidai kuwa mlalamikaji alifika katika nyumba hiyo na kuulizia kama vyumba vipo.

Chaula alidai kuwa, Agosti 23, mwaka 2014 mlalamikaji aliingia saa 7:00 mchana ambapo alipatiwa chumba namba sita pamoja na funguo. 

Akiongozwa na Wakili wa Serikali, Sylvia Mitanto, shahidi huyo alieleza kuwa anamfahamu mlalamikaji kwa muda mrefu kama mshauri wa masuala ya Ukimwi na kwamba alikuwa anapeleka wateja katika nyumba hiyo ya kulala wageni.

Alidai saa 12:00 jioni alimuona mlalamikaji akiwa katika mlango wa kutokea akiwa amevaa shati na taulo huku akiwa hajavaa viatu. 

“Aliniita na kuniulizia Meneja wa gesti hii, Mohamed Hamza, nilimuita na kuongozana kwa pamoja kwenda chumbani kwa mlalamikaji ambapo alikuwa anaonekana hana furaha,’’ alidai Chaula.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More