Wednesday, January 31, 2018

UWT MANISPAA YA IRINGA WAAZIMISHA MIAKA 41 KWA KUFANYA USAFI NA KUTOA ZAWADI KATIKA KITUO CHA AFYA CHA NGOME

 mwenyekiti wa wanawake wa chama cha mapinduzi (UWT) manispaa ya Iringa Ashura Jongo akiwa na viongozi wengi wameazimisha miaka arobain na moja (41) kwa kufanya usafi katika kituo cha afya cha ngome pamoja na kugawa zawadi mbalimbali kwa wagonjwa 
 Huyu ni mmoja ya wanawake wa umoja wa chama cha mapinduzi CCM waliokuwa wakitoa zawadi kwenye kituo cha afya cha Ngome kata ya Kihesa manispaa ya Iringa
 Umoja wa wanawake wa chama cha mapinduzi (UWT) manispaa ya Iringa wameazimisha miaka arobain na moja (41) kwa kufanya usafi katika kituo cha afya cha ngome pamoja na kugawa zawadi mbalimbali kwa wagonjwa ambalo wamelazwa katika kituo hicho kwa lengo la kuwafikia na kutekeleza ilani ya chama cha mapinduzi
Umoja wa wanawake wa chama cha mapinduzi (UWT) manispaa ya Iringa wameazimisha miaka arobain na moja (41) kwa kufanya usafi katika kituo cha afya cha ngome pamoja na kugawa zawadi mbalimbali

Na Fredy Mgunda,Iringa.

UMOJA wa wanawake wa chama cha mapinduzi (UWT) manispaa ya Iringa wameazimisha miaka arobain na moja (41) kwa kufanya usafi katika kituo cha afya cha ngome pamoja na kugawa zawadi mbalimbali kwa wagonjwa ambalo wamelazwa katika kituo hicho kwa lengo la kuwafikia na kutekeleza ilani ya chama cha mapinduzi.

Akizungumza wakati wa kufanya usafi na kugawa zawadi,mwenyekiti wa umoja huo Ashura Jongo alisema kuwa anaishukuru serikali ya awamu ya tano kwa kufanya kazi kwa kuwafikia wananchi wa chini hasa wale wanyonge kwa kutimiza kile ambacho kilikuwa kimeahidiwa wakati wa kuomba kura za kuongoza nchi.

“Kiukweli naomba nichukue nafasi hii kumpongeza sana  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli kwa kuwa anafanya kazi kubwa sana kuhakikisha kuwa Tanzania inapiga hatua ya kimaendeleo hivyo ni lazima tuonge mkono juhudi hizi” alisema Jongo

Jongo alisema kuwa serikali imefanikisha kuleta mabadiliko ya haraka katika sekta ya afya tofauti na hali ilivyokuwa hapo awali hivyo wananchi wanatakiwa kuendelea kufanya kazi kwa kujituma ili kuunga mkono juhudi hizi.

“Najua kuwa mnaona kwa macho yenu kiasi gani serikali ya wamu ya tano jinsi gani huduma za afya zilivyo boreshwa na lazima tujivunie hiki kinachofanywa na Rais wetu,mimi binafsi naunga mkono juhudi hizi na ninaomba wananchi nao waunge mkono juhudi hizi” alsema Jongo

 Jongo alisema kuwa kuongezaka kwa hospital za rufaa kwenye mikoa,vituo vya afya kwenye kata au tarafa, zahanati kwenye vijiji na mitaa ni hatua kubwa ya kimaendeleo hivyo ndio serikali ya awamu hii inavyotekeleza vilivyo ilani ya chama cha mapinduzi ya mwaka 2015 hadi 2020.

“Nyie ni mashaidi kuwa zamani tulikuwa tunaishia kuwa na hospitali za mikoa tu lakini kwa sasa mambo yamebadilika kila kitu kinazidi kuwa kwenye ubora unaostahili kuwahudumia wananchi waliotuweka madarakani” alisema Jongo

Lakini sio afya tu hata ukiangalia saizi tunapata elimu bure ambayo inamwezesha kila mwanafunzi kusoma bure na kuhakikisha tunapunguza wimbi la wanafunzi kukosa elimu ambapo inasaidia kuwa nakizazi cha wasomi hapo baadae.

Naye mjumbe wa kamati ya utekelezaji wa umoja huo Devota Chaula alisema kuwa wanawake wengi wanakumbuna na changamoto mbalimbali hasa kukosa mikopo midogo midogo hivyo serikali ya awamu ya tano hivyo inatakiwa kuangalia kwa jicho la tatu kutusaidia kupata mikopo hiyo.

“Wanawake wanafanya kazi kwa umoja sana hivyo kukosa mikopo kuasababisha kuduma kwa kipato cha kukuza uchumi wa mtu moja moja na taifa kwa ujumla hivyo ukifanikiwa kumweza mwanamke basi umewawezesha wananchi wote hapa nchi” alisema Chaula

Chaula alisema kuwa watanzania wanatakiwa kubadili kwa kuacha kuishi kimazoea hivyo wanatakiwa kuendana na kasi ya serikali ya awmu ya tano kwa kufanya kazi kwa kujituma ili kukuza vipato vyao.

Kwa upande mratibu wa afya ya uzazi na mtoto Sezalia Endru aliwashukuru viongozi hao wa umoja wa wanawake wa ccm manispaa ya Iringa kwa kuwatembelea na kufanya usafi na zawadi walizozitoa kwa watumishi na wagonjwa waliokuwepo muda huo.


“Tunaomba mtufikishe salamu kwa Rais wa serikali ya awamu ya tano kwa kazi kubwa anayoifanya kwa kuboresha sekta ya afya kwa kuwa hali ya sasa kila kitu kinaenda kwa wakati” alisema Endru

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More