Thursday, January 25, 2018

RC MASENZA AIPONGEZA KAMPUNI YA ASAS KWA KUCHANGIA MAENDELEO MKOANI IRINGA

Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza ameipongeza kampuni ya Asas ya mkoani Iringa akiwa kwenye moja ya shule ya sekondari wakati wa ziara yake ya kimkati ya kutatua changamoto za shule.

Na Fredy  Mgunda,Iringa

MKUU wa mkoa wa Iringa Amina Masenza ameipongeza kampuni ya Asas ya mkoani Iringa kwa kufanya kazi ya kusaidia kutatua changamoto za miundo mbinu na majengo katika maeneo ya taasisi hata maeneo ambayo serikali imeshindwa kutekeleza.
 
Hayo yamesemwa wakati wa ziara aliyofanya katika baadhi ya meneo ya mkoa huu,Masenza alisema kuwa kampuni ya Asas imekuwa ikitolea kufanya kazi za wananchi na kusaidia kutatua kero za wananchi pale inapopaswa kufanya hivyo.

“Iringa tuna kampuni nyingi ambazo zinafanya biashara hapa lakini mchango wa kampuni ya Asas imekuwa ikijitoa sana katika shughuli za kimaendeleo hivyo ni lazima niipongeze kwa kazi kubwa inayofanya kutatua kero za wananchi na kutoa misaada mbalimbali” alisema Masenza

Masenza alisema kuwa amefakiwa kufanya ziara kwenye baadhi ya maeneo na amekutana na kazi zilizofanywa na viongozi wa kampuni hii ya Asas mfano wa Iringa mjini Salim Asas amejitolea mifuko mia mbili hivi karibu licha kuwa anafanya kazi nyingi za kimaendeleo katika manispaa ya Iringa.

“Salim Asas amefanya mambo makubwa sana hapa Iringa mfono kwa uchache tu amesaidia mambo mengi jeshi la polisi,amesaidia sekta ya afya kwa kujenga baadhi ya mahodi katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Iringa,amekarabati majengo mengi hapa manispaa,mimi nasema kuwa nitaendelea kumpongeza kwa kazi kubwa anaifanya hapa” alisema Masenza

Aidha Masenza alisema kuwa alipokuwa kwenye ziara katika shule ya sekondari ya Ilambilole amekutana na mchango wa ujenzi wa jingo la madarasa ambalo limejengwa na kampuni hiyo kupitia mwenyekiti wa bodi wa shule hiyo ndugu Feisal Asas,lakini wamejenga hodi katika kituo cha Afya cha kising’a ambacho kipo kata ya kising’a.

“Nichukue nafasi hii kumpongeza Fesail Asas kwa kazi anayoifanya katika wilaya ya Iringa vijijini haina mfano anafanya kazi kubwa sana na hayo ni maeneo machache tu bali amefanya kazi katika maeneo mengi ambayo sisi kama serikali tulikuwa bado hatujafika” alisema Masenza

Masenza alisema kuwa amalizia na swala la ujenzi wa barabara ya kutoka kising’a kwenda Ilambilole kuna eneo amelijenga na kusaidia wananchi kupita hata leo kwenye msafara wa ziara ya mkuu wa mkoa gari zote zimepita kwenye barabara.

“Haya ndio ambayo nimejionea mwenyewe kwenye ziara yangu hii fupi ambayo yamefanywa nah ii kampuni ya Asas hivyo naomba wasituchoke waendelee kutusaidia kutatua changamoto pale wanapoweza basi nasi serikali tutaendelea kutekeleza pale tunapotakiwa kutekeza kutokana na miongozo yetu” alisema Masenza

Nichukue fursa kuiomba kampuni hii iendelee kutusaidia kutatua kero ambazo wanaona zinafaida kwa jamii na sio kwa mtu binafsi.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More