Monday, July 31, 2017

MWENYEKITI CHARLES MAKOGA : SHERIA MPYA KUTUMIKA KUKUZA MAPATO YA MJI WA MAFINGA

Mwenyekiti wa halmashauri ya Mafinga Mjini Charles Makoga akizungumza wakati wa baraza la madiwani wa halmashauri hiyo Baadhi ya madiwani wa halmashauri ya Mji wa Mafinga wakiwa katika baraza pamoja na wataalamu mbalimbali wa halmashauri hiyo. Na fredy Mgunda, Mafinga Halmashauri ya Mji wa Mafinga mkoni Iringa inatarajia kukuza mapato katika mwaka Mpya wa 2017/2018 kutokana na kuanza kuzitumia sheria mpya za ukusanyaji mapato pamoja na kuvijua vyanzo vingine vya mapato ambavyo ndio vitasababisha kukuza uchumi wa halmashauri hiyo. Akizungumza wakati wa baraza la madiwani Mwenyekiti wa halmashauri ya Mafinga Mjini Charles Makoga alisema kuwa sheria mpya walizoletewa toka mwezi wa tano zinawapa nafasi ya kuanza kuzitumia wakati wa kukusanya...

MAADHIMISHO YA NANENANE 2017 KITAIFA KUFANYIKA LINDI KUANZIA KESHO

Na Mathias Canal, Lindi     Maonesho ya Kilimo (NaneNane) yanataraji kuanza kesho Agosti 1, 2017 kote nchini kwa ngazi mbalimbali za kanda huku Maonesho hayo Kitaifa yakifanyika Mkoani Lindi huku Maandalizi na maonesho ya  Ki-Kanda yanaratibiwa na uongozi wa  mikoa husika. Maandalizi ya Maonesho ya 24 ya kilimo na sherehe za Nanenane yatafanyika kwa siku 8 ambapo Kitaifa yatafika ukomo jioni ya Agosti 8, 2017 katika Viwanja vya Ngongo na Maeneo mengine yatakapoadhimishwa kikanda  katika  viwanja vya maonesho ni John Mwakangale –Mbeya; Mwalimu J.K. Nyerere –Morogoro; Themi – Arusha; Nzuguni -  Dodoma; Nyahongolo – Mwanza; na Fatuma Mwassa - Tabora.  Maonesho ya mifugo sanjari na...

UNAITUMIAJE TEKNOLOJIA KURAHISISHA SHUGHULI ZAKO ZA KILA SIKU?

Na Jumia Travel Tanzania Kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia binadamu waliyonayo kwa sasa si jambo la kushangaza kumuwezesha mtu akafanya shughuli zako zote akiwa yupo sehemu moja ndanin ya muda mfupi. Kwa mfano, kwa kutumia simu yako ya mkononi unaweza kutatua changamoto kadhaa hapo nyumbani kwako kama vile kufanya miamala ya fedha kutoka benki na kisha kutoa kwa mawakala huduma za fedha, kulipia umeme, kulipia maji, kulipia king’amuzi, kuagiza chakula, kuagiza usafiri, kufanya manunuzi ya bidhaa na huduma mbalimbali. Lakini swali ni kwamba, je ni watanzania wangapi wanaiona fursa hiyo iliyoletwa na teknolojia kama suluhu za changamoto tofauti zinazowazunguk...

MAMA NAMAINGO ‘AWAFUNDA’ AKINAMAMA WA GREEN VOICES KILIMOBIASHARA NA UJASIRIAMALI

Mkurugenzi wa Namaingo, Biubwa Ibrahim Mratibu wa Mradi wa Green Voices kutoka Hispania, Alicia Cedaba, akiwapa majukumu washiriki wa warsha hiyo. MKURUGENZI Mtendaji wa kampuni ya Namaingo Business Agency, Biubwa Ibrahim, amewataka akinamama wanatekeleza mradi wa Green Voices Tanzania kuwa wabunifu na kutokata tamaa katika shughuli wanazozifany...

MTANDAO MPYA WA VYOMBO VYA HABARI VYA KIJAMII WASAJILIWA NCHINI

Mtandao mpya unaoundwa na Radio na vyombo vya habari vya kijamii Tanzania chini ya shirika la vyombo vya habari vya maudhui ya kijamii uliosajiliwa kwa jina la TANZANIA DEVELOPMENT INFORMATION ORGANIZATION-TADIO umeanzishwa rasmi baada ya kuvunjika kwa mtandao wa zamani wa COMNETA. Tukio hilo limetokea Julai 28, 2017 katika mkutano mkuu wa kwanza ambao pamoja na mambo mengine ulichagua safu mpya ya viongozi wa mtandao huo. Shirika la mtandao wa vyombo vya habari jamii Tanzania uliokuwa na jina la COMMUNITY MEDIA NETWORK OF TANZANIA – COMNETA, limevunjika rasmi mwezi machi mwaka huu. Katika mkutano huo kuwa kuundwa kwa shirika hilo jipya kunalenga kuhakikisha kunakuwa na mtandao makini wa Radio na vyombo vingine vilivyojikita katika kuibua...

Benki ya Watu iwa Zanzibar PBZ Yaibuka Kidedea Katika Mwajiri Bora Katika Ushirikishwaji na Chama cha Wafanyakazi ZAFICOW.

Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi ZAFICAW Bi. Rihii Haji Ali, akimkabidhi Cheti Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Juma Ameir Khafidh cha Mwajiri Bora Katika Ushirikiano na ZAFICOW kwa mwaka 2017. wakati wa hafla ya Bonaza la Wafanyakazi wa PBZ lililofanyika katika ufukwe wa Hoteli ya Visiter Inn Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja. Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi ZAFICAW Bi. Rihii Haji Ali, akimkabidhi Cheti Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Juma Ameir Khafidh cha Mwajiri Bora Katika Ushirikiano na ZAFICOW, wakati wa hafla ya Bonaza la Wafanyakazi wa PBZ lililofanyika katika ufukwe wa Hoteli ya Visiter Inn Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja.   Viongozi wa PBZ na wa ZAFICOW wakiimbi wimbo...

Sunday, July 30, 2017

MCHAPALO WA MIAKA 50 YA BENKI YA NBC WAFANA JIJINI MWANZA

Na George Binagi-GB Pazzo Jana Julai 28,2017 usiku wa kuamkia leo jumamosi, mchapalo (sherehe) wa kusherehekea miaka 50 tangu kuanzishwa kwa benki inayolitumikia Taifa la Wachapakazi, NBC umefana Jijini Mwanza ambapo benki hiyo imekutana na wadau wake wakiwemo wafanyabiashara. Kaimu Mkurugenzi wa benki ya NBC, Theobald Sabi alisema maadhimisho hayo yamefanyika Jijini Mwanza ikizingatiwa kwamba Jiji hilo ni la pili kwa ukubwa nchini na kwamba inao wateja wa muda mrefu wanaohudumiwa kwenye matawi yake matatu hivyo ni jambo jema kujumuika nao pamoja. "Hakika NBC ina historia ndefu katika kujenga uchumi wa nchini yetu, ni jambo lisilopingika kwamba NBC ni mama wa benki za kibiashara hapa Tanzania". Alidokeza Sabi huku akiwashukuru wafanyakazi...

Page 1 of 69412345Next
Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More