Monday, June 4, 2018

MKURUGENZI WA NGOTI GREEN ACADEMY AWATAKA WAZAZI KUWALEA WATOTO KIMAADILI


 Mkuu wa shuleya Ngoti Green Academy  Jonson Mtewele kushoto akiwa na mkurugunzi wa Ngoti Green Academy Thomas Ngoti ambaye alikuwa anatoa neno kwa wazazi waliofika kwenye kikao cha pamoja baina ya wazazi walimu na wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo
 Mmoja wa wazazi walifika katika shule ya Ngoti Green Academy akitoa neno mbele ya wageni waalikwa na mkurugunzi wa Ngoti Green Academy Thomas Ngoti 
Picha za pamoja baina ya wazazi,walimu na viongozi wa shule ya Ngoti Green Academy  
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Ngoti Green Academy 

NA FREDY MGUNDA,IRINGA

Mkuu wa shule ya Ngoti Green Academy  amewataka wazazi na walezi mkoani Iringa kuwalea watoto katika maadili yanayostahili ili kuwa na kizazi chenye maadili na uwajibikaji kwa jamii na kuleta maendeleo ya nchi na familia zao.

Akizungumza na wazazi wa shule ya Ngoti Green Academy mkuu wa shule hiyo Jonson Mtewele alisema kuwa maadali ya mtanzania yanazidi kupotea kutoka na mmong’onyoko wa utandawazi

“Mimi nasema kuwa saizi tamaduni za kimagharibi zimeharibu sana utamaduni wenu maana wananchi wengi wanaiga bila kujua wanaiga maadili gani ndio maana saizi watoto wetu wengi wamekuwa hawana maadili” alisema Mtewele

Mtewele aliwataka wazazi kuacha kuwafundisha tamaduni za kimagharibi ambazo hazina maadili ya kimaendeleo kwa watoto wadogo ambao ndio wamekuwa waathirika wakubwa kwenye hizi tamaduni za kimagharibi.

“Mtoto kutoka mwaka mmoja hadi miaka nane ndio umri wa mtoto kupokea vitu vipya kichwani mwake ndio maana nasema ukikosea kumlea mtoto katika umri huo basi waweza kulea mtoto akiwa hana maadili yatayomuwezesha kufanikiwa katika maisha yake” alisema Mtewele

Aidha Mtewele alisema shule ya Ngoti Green Academy inawafundisha wanafunzi katika mfumo wa maadili ya dini kutoka na matendo ya bwana yesu aliyaonyesha duniani na kuwa mfano wa maadili bora.

“Tunataka mtoto akue katika maadili ya kikristo kwa maana kuwa tunamtaala wenye tabia njema siti ambazo bwana yesu alizionyesha akiwa duniani upole,unyenyekevu na wakati furani kukubali kuonewa na sio lazima abishe kila kitu na tunavyomuelekeza kwa namna hivyo tumegundua kuwa watoto watakuwa kati hali hiyo” alisema Mtewele  

Mtewele aliongeza kuwa shule hiyo inapokea watoto kuanzia mwaka mmoja hadi miaka nane kwa kuwa huo ndio wakati mzuri wa kuwalea watoto kimaadili na kuwajengea uelewa wa maisha ya baadae.

“Tumeruhusiwa kuwapokea watoto kuanzia umri wa mwaka mmoja hadi miaka nane baada ya hapo inakuwa vigumu kupokea watoto wa zaidi ya miaka hivyo kwa mjibu ya mtaala ambao tunao” alisema Mtewele

Naye mkurugunzi wa Ngoti Green Academy Thomas Ngoti alisema kuwa shule hiyo inatoa elimu iliyobora ambayo inatakiwa kitaifa na kimataifa kutokana na mtaala ambao wanautumia.

“Ngoti Green Academy inatoa elimu kwa upana wake ndio maana wazazi wengi wameanza kuwaleta watoto wao hapa kwa ajili ya watoto wao kupata elimu bora ambayo inapatika hapa nadio huo ubora wake” alisema Ngoti

Ngoti aliongeza kuwa wanampango wa kwenda kwenye ngazi ya sekondari na chuo kikuu kwa kuwa wamekuwa wakitoa elimu iliyobora hivyo hata serikali inawaamini kwa kuwa wanamtaala mzuri wa kutoa elimu bora kwa wanafunzi ambao watakuwa wanasoma kwenye sekondari na chuo kikuu.

“Ngoti Green Academy Thomas ni chombo kamili cha kuandaa watoto wadogo ambao bado hawajalishwa vitu vingi kichwani na ndio maana wanataka kuanziasha sekondari na chuo kikuu ili wanafunzi weweze kupata elimu bora kwa mtaala bora ambao wanautumia” alisema Ngoti

Ngoti alisema kuwa Ngoti Green Academy inapatikana maeneo ya Mtwivila sehemu inaitwa Mwambusi au unaweza kutembelea makao mkuu ya kampuni yalipo jingo la IMUCU gorofa namba moja chumba na kumi na nane lakini unaweza kupiga namba 0765800310 au 0718056561 hapo ndio itakuwa kazi rahisi kuwapata.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More