Monday, June 4, 2018

VIONGOZI 11 WA UPINZANI WARUSHIWA KOMBORA LA UFISADI ZITTO KABWE ATAJWA KUWA NI NAMBA MOJA

 Mwanasheria Patrobas Katambi.
Mwenyekiti mstaafu wa Baraza la Umoja wa Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAVICHA), ambaye kwa sasa ni kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mwanasheria Patrobas Katambi, akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu viongozi wa upinzani kujinufaisha kupitia elimu na vyeo vyao. Soma taarifa hiyo hapa chini.

TUHUMA NZITO ZISIZOKANUSHIKA ZINAZOWAKABILI VIONGOZI WA UPINZANI KUJINUFAISHA KUPITIA ELIMU NA VYEO VYAO.

Ndugu, Watanzania na Ndugu Waandishi wa habari, Asasi za Kiraia na Taasisi zote wadau wa Maendeleo Tanzania, nawasalimu kwa Jina la Amani. 

Nchi yetu tumepewa na Mungu, utajiri wa Rasilimali za kila aina, ila Watu wake ni Masikini na Nchi ni Masikini Kiuchumi. 
Sababu kubwa ni makosa ya Aina ya siasa, Mifumo na Uongozi katika Uamzi, Mipango, Utekelezaji, Rushwa na Mgongano kati ya Maslahi binafsi  na Uzalendo (Ufisadi).

Ugonjwa wa Kukosa Uzalendo na Uaminifu ndio chanzo ya cha Serikali ya CCM awamu ya Tano, Chini ya Uongozi wa Mhe. Rais JP Magufuli kuamua kufanya Uchunguzi na Mabadiliko katika Sheria, mifumo, miundo, na utendaji ili kuinusuru Nchi yetu na Taasisi washirika Kiuchumi.

Bila upendeleo wa utoaji taarifa(Double Standard), Vyombo vya Habari kwa niaba na faida ya Watanzania leo wajue wapo Mafisadi wakubwa kutoka Vyama vya Upinzani, Walipata wapi Uhalali na Uhodari wa kuchambua na kutuhumu wenzao kwa ufisadi huu? Sio vibaya nao Watanzania wakawajua na kutoa hukumu bila Upendeleo, ili kuisaidia Nchi kupata Viongozi Wazalendo wa kweli.

Ikumbukwe hakuna dhambi kubwa au ndogo, dhambi ni dhambi, Ulaji ni ulaji, Haramu ni haramu, Wizi ni wizi.

Haramu ya Kiongozi wa CCM au Serikali, haiwezi kuwa Halali kwa Kiongozi wa Upinzani (Haramu ni Haramu tu.)

Katika list hii ya Mafisadi-Mibuyu 11 wa Upinzani. 

Leo naanza na mmoja (kwa machache) ambae ni Mhe.
Zitto Kabwe (MB. ACT)Kigoma mjini.

Anajipambanua na kuhubiri yeye ni Mzalendo na Mjamaa...
Ikiwa yafuatayo yanamkabili anapata wapi uhalali wa kunyooshea watu vidole?

1. Mhe. Zitto alipokea hongo kutoka Barrick kuzibwa mdomo pamoja na vifaa vya kukarabati shule jimboni kwake  vyenye thamani ya Dola $20.000 kinyume na sheria (CSR), baada ya kuwa mwiba kwao katika kudai mabadiliko ya mikataba ya madini isiyo na faida kwa Taifa.Mchakato wote  ulimnufaisha kwa zaidi ya Tshs Bilioni 1. Baada ya hongo, ghafla alikuwa mkimya kwenye Bunge na katika Kamati ya Rais JK chini ya Jaji mstaafu Mark Bomani,  hakukomaa kuizungumzia kabisaa "The Boman Report" na hata katika utungaji sheria mpya ya madini-2009 hakua mpingaji kama ilivyotarajiwa, Ukweli huo ambao hajaukanusha mpaka leo,  umethibitishwa na uchunguzi uliofanywa na Adam Hooper kwenye report yake aliyoiwasilisha chuo kikuu cha Carlton mwezi July, 2011 kwa mujibu wa gazeti la Guardian la Uingereza la Sept4, 2011.Je! hii sio kutumia cheo kutishia ili apewe hongo kwa taasisi,makampuni au Serikalini.

2. Mhe. Zitto anatuhumiwa kumiliki Ghorofa kubwa Dodoma ambalo ujenzi wake hauendani na kipato chake halali. Na awali zilipopigwa kelele akamua kusitisha ujenzi. Ghorofa hilo hajalitaja kwenye mali zake lakini ukweli uliopo ni mali yake (Kwa mujibu wa nyaraka za...)na hata mke wake mara kadhaa ameonekana akisimamia kwa kificho finishing ya jengo hilo na wapo mashahidi katika idara zote zinazohusika viwanja na ujenzi wa kuthibitisha umiliki wake.

3.  Mhe.Zitto ametajwa kwenye Jarida la The Africa Confidential liloandika kuhusu ufisadi katika Mifuko ya hifadhi ya jamii tangu awamu ya tatu,  ufisadi ambao ulihusisha vigogo wengi kwa miaka mingi. Mhe. Zitto ni miongoni mwa wanasiasa waliotajwa kwa majina, kwa namna kamati aliyoiongoza kwa miaka minane (8) ilivyofumbia macho madudu katika mifuko ya hifadhi hususani NSSF kinyume na ilivyotarajiwa.

4. Mhe. Zitto kunaushahidi kuwa, kwa miaka yote aligeuza Kamati ya PAC kama duka binafsi kwa kutisha Wakurugenzi Wakuu wa Taasisi za UMMA,  baadhi ya waliokuwa wajumbe wako wanakili kupokea bahasha, ambapo wewe ulichukua kiasi kukubwa zaidi kama Mwenyekiti na kufumbia macho makosa ya wazi na ubadhirifu katika taasisi za umma kama NHC, NSSF, TANAPA,TANESCO TPA nk. mpaka baadae majipu haya yamekuja kutumbuliwa na Serikali ya awamu ya Tano. Waeleze Watanzania Uongozi wa Kamati hiyo uliupataje mara kwa mara, hata baadhi ya Wabunge wa CCM walishangazwa na ngekewa hiyo.

5. Mhe. Zitto Watanzania wanajiuiza majipu aliyoyatumbua Rais Magufuli baada ya kuingia madarakani katika Mashirika ya UMMA, kwanini Kamati yako iliyaacha na kuyafumbia macho kama hukuwa kwenye project ya kutumiwa na mafisadi?

6. Mhe. Zitto, kwanini mwanzo alionekana kuisifia sana Serikali awamu ya tano na hasa Rais Magufuli, na sasa unaipinga vikali? Je tuamini haya ni matokeo ya kukosa Uenyekiti wa PAC na badae kupoteza matumaini ya kuwa, ungeteuliwa  Uwaziri wa nishati na Madini bila kujali Chama chako kama ilivyokuwa kwa Prof. Kitila Mkumbo na Anna Mgwila? Kumbuka wapinzani wenzako walivotoka nje bungeni kupinga matokeo ya Zanzibar yeye alibaki kama mkakati wa kuishawishi CCM na Mwenyekiti wake wamuamini na upewe tena Uenyekiti wa PAC anawajua aliopanga nao huo mkakati. Baada ya hayo yote kugonga mwamba amegeuka Mbogo na nakuanza kuitafutia madoa kwa nguvu zote halali na haramu Serikali ya awamu ya tano.

7.  Mhe. Zitto, ulikaliliwa kupitia press conference akisema  na kuponda sana Muungano wa UKAWA na kusisitiza UKAWA ni "UKAWA ni Wasaka tonge"  pia siku za badae kupitia press, uliwahi kusisitiza (ushahidi upo) "Kama mtu anataka siasa za ulaghai basi aende UKAWA" akawa anaisifu Serikali ya awamu ya tano na baadae kwa kulinda maslahi yake kisiasa,  aligeuka nakuanza kuiponda Serikali ya awamu ya tano kuwa ni ya Kidikteta na inaminya demokrasia. Je! unatuambia nini Watanzania kuhusu siasa za ulaghai na usakatonge za kutumia cheo na elimu kupindisha mambo ili kulinda maslahi binafsi na si ya UMMA?

9. Mhe. Zitto, Alipofukuzwa Chadema alidai kaonewa kwa kifitna kuwa alitaka kumpindua Mhe. Mbowe katika kiti chake, na akawatuhumu CHADEMA kwa ubadhirifu mkubwa wa fedha na uongozi wa Kidikteta. Je ilikuwa kweli? na kama sio kweli kwanini alisema uongo? Je Watanzania tuendelee kukuamini kwa lipi? 

10. Mhe. Zitto, Ulipotoka CHADEMA, Mhe. T Lissu alisema yale waliyokutuhumu nayo pamoja na kupewa gari mbili na Mhe. Mkono, hukukanusha bali ulielekeza tuhuma kwa  Mhe.Mbowe kama ulivyokaliliwa hapo chini, ukimjibu Mhe.Lissu Je! kwa siasa za aina hii zisizo na chembe ya uzalendo, Watanzania tuendelee kukuamini kwa yapi ya ukweli na yapi ya uongo tusiyaamini?

*Mhe.  ZITTO KABWE* Ulisema haya ukimjibu Lissu ulipofukuzwa Chadema...

"Lissu anasema nimepewa magari 2 na Mzee Mkono. Anasema kaambiwa na Mkono. Naamini Mkono alimwambia pia mwaka 2005 alimpa Freeman Aikaeli Mbowe tshs 40m ili Mbowe asifanye kampeni Musoma vijijini. Nadhani alimwambia pia mwaka 2008 (baada ya orodha ya mafisadi kutangazwa 2007) Mkono alimpa Freeman tshs 20m za uchaguzi wa Tarime na Freeman akasema kwenye chama ametoa mkopo na akalipwa. Nadhani alimwambia pia kuwa Mwaka 2010 Mkono alimpa Mbowe tshs 200m za kampeni ya Slaa. Pia hakusahau kumwambia kuwa Rostam Aziz alimpa Mbowe tshs 100m za kampeni. Lissu anajua kuwa gazeti la Tanzania Daima limeanzishwa na fedha za chama kutoka Conservative party?

Nimefanya internship yangu kwa Mkono and Company Advocates kuhusu masuala ya mikataba. Mzee Mkono ni Mzee wangu na alisaini petition ya kumtoa Waziri Mkuu Pinda.

Lissu awaambie waliyemtuma wamwambie ukweli wote. Lissu ajue yeye ni kifaranga tu, Mimi namtaka mama wa kifaranga ajitokeze. Aeleze aliingia deal gani na Sumaye mwaka 2005 kufuatia deni lake NSSF. Aweke wazi mkataba kati yake na NHC kuhusu nyumba ya Umma ilipo Club Bilicanas.

They must know I am not a push over. Chacha died, I won't.

Mtu ambaye hawezi kuheshimu mke wake aliyemzalia watoto hawezi kunyooshea mtu kidole kuhusu maadili."

Mwisho wa kuku nukuu.


11. Mhe. Zitto, Je! Huoni kwamba usahaulifu wetu Watanzania, kutokusoma kwa udadisi pamoja na kutofatilia sana historia ya matukio ndio mtaji wa Wanasiasa maslahi na walaghai wanaohatarisha amani, umoja na mshikamano na maendeleo ya Taifa letu ?

12. Mhe. Zitto, Je Nini maoni yako kwa Siasa hizi  za kijasiliamali, kinafiki, chuki, fitna, uzandiki na uongo zenye ujamaa wa kibepari usio na chembe ya uzalendo kwa matendo katika maslahi na ustawi wa Taifa letu Tanzania? Je! tuendelee na siasa hizi ili tuangamie kama nchi nyingi tajiri kwa rasilimali za Kiafrika zinavyoangamizwa na Viongozi wake wenye tamaa za madaraka, mali na sifa?

13. Mhe. Zitto,  ni kwanini Mhe. Jussa aliwahi kukutuhumu na kukujibu akamaanisha wewe una ndimi mbili, Ukiwa kiongozi tunae kuamini ukweli wa kauli hiyo ni upi?

14. Mhe. Zitto, Je unaweza ukawaweka wazi watanzania Ukiwa mzalendo na mjamaa, muumini wa Azimio la Arusha na Tabora, mbali na pesa yako binafsi, ulipata wapi Milioni zaidi ya miasaba (700) za Kitanzania kuanzisha Chama ACT, na za Kampeni Uchaguzi Mkuu 2015. Ukisimamisha wagombea Ubunge na Udiwani katika majimbo 219 ukivizidi vyama kongwe vyote vya upinzani sambamba na ukwasi wa mali,hisa, na uwekezaji ulionao ndani na nje ya nchi wenye thamani ya Mabilioni kinyume na kipato chako halali,  mbali na mali ulizo orodhesha katika Tume ya Utumishi wa Umma?

15. Mhe. Zitto scandal ya Escrow na IPTL aliwahi kuchapisha kitabu/ kijarida na baadae hukukisambaza vikateketezwa. Alituhumiwa kupokea hongo kutoka kwa Sing Seth ya zaidi Tshs 50 Milioni na alikwepa kujibu tuhuma hizo.Watanzania wanakiu ya kujua ukweli juu ya tuhuma hizo?

MWISHO.

Mhe. Zitto ajue sina ugomvi wala maslahi binafsi na wewe, Kama watanzania wengine, sitilii shaka elimu yako ila natilia shaka aina ya Siasa yako, na uhalali wako wa kutuhumu wengine. Watanzania tuko tayari kukuamini endapo, utatuthibitishia tuhuma hizo za mda mrefu, sio za kweli kwa ushahidi usioacha shaka yoyote ili tuamini kuwa hautumii Elimu na cheo chako kisiasa kujinufaisha na sio kwa faida ya Taifa letu. Nipo tayari kwa lolote, hata ikibidi kwenda mahakamani.

Asanteni kwa kunisikiliza, list nitaendelea.

Na: 

Patrobas Katambi
Mwanasheria.
Mwana-CCM.
M/Kiti Mstaafu BAVICHA Taifa.
June 3, 2018.
Dar es Salaam.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More