Tuesday, January 17, 2017

Lowassa Kaachiwa Huru

Waziri mkuu Mstaafu na Mgombea wa Urais 2015 kupitia CHADEMA, Edward Lowassa leo alikamatwa na jeshi la Polisi  wakati akiwa anaenda kwenye kampeni za uchaguzi Kata ya Nkome na baadaye aliachiwa  huru ambapo taarifa za polisi zinadai kuwa walimzuia kwa sababu za kiusalama.

Kupitia kituo cha Television cha Azam wameripoti habari ya kukamtwa kwa Lowassa ambapo baadhi wa wananchi wameeleza ilivyokuwa.

"Tulikuwa kwenye msafara ya kumpokea Lowassa lakini tulipofika hapa stendi wananchi walitaka kuongea na Lowassa, kabla hata hajashuka kwenye gari askari walituvamia wakasema tuondoke moja kwa moja twende kituoni"- shuhuda

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More