Monday, September 26, 2016

TIC yahamasisha wadau kuwekeza Dodoma

Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimefungua milango ya uwekezaji wa nchi mbalimbali kuja kuwekeza Nchini hasa makao makuu ya Nchi, Dodoma.

 Hayo yamebainishwa na Mtendaji Mkuu wa (TIC), Clifford Tandari  juu ya fursa za uwekezaji zilizopo Mkoani Dodoma, wakati wa Mkutano Mkuu wa Uwekezaji wa Dunia kanda ya Afrika uliofanyika Mjini Kigali nchini Rwanda hivi karibuni. 

Mkutano huo uliandaliwa na COMESA kwa kushirikiana na Serikali ya Rwanda.
Rais Paul Kagame wa Rwanda na Rais Yoweri Museveni wa Uganda, wakipatiwa maelezo na Mtendaji Mkuu wa Kituo Cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Clifford Tandari, juu ya fursa za uwekezaji zilizopo Mkoani Dodoma, wakati wa Mkutano Mkuu wa Uwekezaji wa Dunia kanda ya Afrika uliofanyika Mjini Kigali nchini Rwanda hivi karibuni.
Rais Paul Kagame wa Rwanda na Rais Yoweri Museveni wa Uganda, wakimsikiliza kwa makini Mtendaji Mkuu wa Kituo Cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Clifford Tandari, alipokuwa akiwaelezea juu ya fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo Mkoani Dodoma, wakati wa Mkutano Mkuu wa Uwekezaji wa Dunia kanda ya Afrika uliofanyika Mjini Kigali nchini Rwanda hivi karibuni.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More