Wednesday, September 7, 2016

SEREKALI YA KONGO YAMPA CHETI CHA BALOZI WA AMANI MWANAMUZIKI MESS JAKOBO CHENGULA KUTOKA TANZANIA


mwanamuziki wa nyimbo za injili Mess Jakobo Chengula akionyesha cheti ya hehima cha balozi wa amani alichozwadawa na serekali ya ya Kongo
Serekali ya Jamuhuri ya Demokrasia  ya Kongo  imemtunuku cheti cha heshima ya kipekee cha {Balozi wa Amani  } mwanamuzi wa nyimbo za injili kutoka Tanzania Mess Jakobo Chengula kwa kazi nzuri anayoifanya ya kuhubiri amani na upendo kupitia nyimbo zake .

Mess Jakobo Chengula ambaye kwa sasa anatamba na wimbo wa moyo wangu hauna woga aliomshirikisha mwanadada Upendo Nkone ni mwanamuziki pekee kutoka Tanzania aliyotunikiwa cheti hicho cha heshima cha balozi wa Amani  ulipokwenda kufanya huduma ya uimbaji katika nchi ya Kongo

Akizungumza na mtanzania Chengula alisema kuwa ni heshima ya kipekee aliyoipata yeye na taifa lake la Tanzania  kwa watu wa mataifa mengine kuona mchango wa wuziki wa injili  katika kuhubiria Amani ya dunia na afrika kwa kiujumla .

Chengula alisema kuwa cheti alichopewa ni cheti cha heshima ya ulinzi wa Amani kutokana ujumbe mzuri ulioko katika nyimbo zake  na matendo mema afanyao katika huduma yake hivyo ni farahi ya kipeke kwa nchi ya Tanzania kuonekana ni nchi inayoendeshwa kwa misingi ya Demokrasia na haki jambo lililopelekea hata mataifa mengine kuona haja ya kuwapa cheti wanamuziki wanaohubiri Amani kutoka tanzania 

“Unajuaa pale tulienda katika huduma ya kuhubiri neno la Mungu na uimbaji  na tulikutana watu kutoka mataifa mbalimbali na mimi peke yangu ndiye niliyotokea Tanzania na pale kulikuwa na viongozi mbalimbali  na waimbaji wengi tena wakubwa kutoka mataifa makubwa  lakini hawakupewa cheti cha balozi wa Amani  lakini mimi nilipewa asee hii ni heshima ya pekee ambayo Tanzania imepata kupitia mimi kule nchini Kongo “”.

“Kongo wamenionyesha kitu cha ajabu sana unaju nchi za wenzetu wanamuziki wanaheshimika sana unajua mimi nimefanya muziki muda mrefu hapa nchini alibamu yangu ya kwanza ni ile ya Mungu wangu habadiliki lakini sijawahi kupata mapokezi makubwa na ya kipeke kama yele niliyopata kule kongo hapa kwetu kuna heshima Fulani lakini kwa kuwa tumezoeya na tunaonana kila mara basi kunakuzoeyana lakini Mungu ni mwema tutabadilika tu na kuthamini cha kwetu  lakini kongo ohoo wametisha maze”

Hata hivyo Mess  alisema kuwa  anatarajia kuzindua albamu yake mpya ya moyo wangu hauna woga inayosambazwa na Msama promotion uzinduzi utakaofanyika jijini Dar eslaam  September 20 mwaka huu huku akiwataka wapenzi na mashabiki wa muziki wa injili kujitokeza kwawingi kwa ajili ya kumsapoti katika huduma yake

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More