Wednesday, March 4, 2015

JACKSON KISWAGA APIGA JEKI UJENZI WA MAABARA SEKONDARI YA NYABULA KALENGA


SHULE ya sekondari Nyabula imeingia katika hatua nyingine ya kukamilisha ujenzi wa maabara zake baada ya kupata msaada unaohusisha mabati 50 na mifuko ya saruji 30.

Msaada huo kwa shule hiyo inayomilikiwa na Kanisa Katoliki Parokia ya Nyabula ulitolewa na mdau wa maendeleo ambaye pia ni Kamanda wa Chipukizi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wa wilaya hiyo, Jackson Kiswaga.

Akikabidhi msaada huo hivikaribuni, Kiswaga aliwataka wananchi kujitokeza kuchangia shughuli mbalimbali za maendeleo katika maeneo yao ili kuondokana na dhana ya kila jambo kufanywa na serikali.

“Ukiwaita watu kwenye harambee ya kufanikisha kwa mfano, harusi, wengi watajitokeza na kutoa michango yao lakini ukiwaita kuchangia maendeleo yao hawajitokezi,” alisema.

Alisema katika dunia ya ushindani, elimu ndio ufunguo muhimu zaidi wa maisha kwakuzingatia kwamba ukishakuwa nayo hakuna mtu wa kukupokonya.

“Elimu ni kila katika katika ulimwengu huu unaolinganishwa hivisasa na kijiji kimoja. Elimu ni maisha, elimu ni maendeleo kwahiyo nitoe wito kwa wazazi, walezi na kila mwenye uwezo wa kufanya kazi aone umuhimu wa kuchanngia maendeleo yake,” alisema.

Alisema katika soko la ajira duniani kote waajiriwa wanapimwa au kupatikana kutokana kwa kuzingatia vigezo vya elimu vinavyotakiwa.

“Kwahiyo tukiulizwa vipaumbele vyetu, tunaweza kusema elimu elimu elimu kwasababu hiyo pekee ndio inayoweza kutumika kubadili mazingira yetu na kutuletea maendeleo,” alisema.

Kiswaga alisema kwa kuzingatia hilo ataendelea kusaidia maendeleo ya sekta ya elimu wilayani humo na kwingine kote atakakoombwa kwa kuzingatia nafasi atakayokuwa nayo.

Akishukuru kwa msaada huo, Padri wa Parokia ya Nyabula Philipo Kindole alisema utasaidia harakati zao za kukamilisha ujenzi wa maabara katika shule hiyo na akaomba wadau wengine kujitokeza kuichangia sekta hiyo.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More