Friday, March 20, 2015

MKURUGENZI WA TIGO JACKSON KISWAGA ATUMIA ZAIDI YA SH MILIONI 10 KUFANIKISHA LIGI SOKA WILAYA YA IRINGA MAARUFU KAMA KISWAGA CUP



Kamu Meneja Mkuu wa Tigo Tanzania, Cecile Tiano akikabidi jezi kwa moja ya timu zinazoshiriki ligi ya wilaya ya Iringa (Kiswaga Cup) anayeshuhudia kushoto ni mdhamini wa ligi hiyo Jackson Kiswaga ambaye pia ni Mkurugenzi wa Tigo Nyanda za Juu Kusini

Akikabidhi vifaa hivyo

Kiswaga akieleza sababu za kufadhili ligi hiyo kwa lengo la kukuza sekta ya mchezo wa soka wilayani Iringa

Wakiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi wa timu hizo

 na fredy mgunda,iringa
“HAKIKUSOEA hata kidogo; kilicheza karata yake vizuri,” maneno hayo yanaweza kusemwa na mpenda soka yoyote wa wilaya ya Iringa baada ya Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Iringa (IDFA) April 26, 2014 kumteua na kumsimika Mkurugenzi wa Kampuni ya Tigo Nyanda za Juu Kusini, Jackson Kiswaga kuwa mlezi wake.



Katika awamu ya pili ya udhamini wake wa ligi soka nngazi ya wilaya hiyo maarufu kama Kiswaga Cup; Kiswaga amemwaga vifaa vyenye thamani ya zaidi ya Sh Milioni 10 vitakavyotumiwa na timu shiriki za ligi hiyo itakayoanza kutimua vumbi April 15, mwaka huu.



Hafla ya makabidhiano ya vifaa hivyo ilifanyika katika hoteli ya Gentle Hills juzi huku ikihudhuriwa na Kaimu Meneja Mkuu wa Tigo Tanzania, Cecile Tiano aliyekabidhi vifaa hivyo kwa timu hizo.



Vifaa vilivyotolewa kwa timu zinazoshiriki ligi hiyo ni pamoja na seti za jezi na mipira.


Taarifa kamili ya kilichofanywa na Kiswaga ambaye pia ni Kamanda wa Chipukizi wa Chama cha Mapiduzi Wilaya ya Iringa katika kufanikisha ligi hiyo kitakujia leo.
 
Timu hizo zinaingia katika msimu mwingine wa ligi hiyo huku ikikumbukwa kwamba timu ya Ugwachanya FC ndiye bingwa wa ligi hiyo msimu uliopita

MSHINDI KISWAGA CUP IRINGA VIJIJINI KUONDOKA NA KOMBE NA MILIONI MOJA, ZAWADI LUKUKI KUTOLEWA KWA WASHINDI WENGINE


0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More