Thursday, February 26, 2015

MTOTO MCHANGA AUAWA NA KUTUPWA KICHAKANI MKOANI MOROGORO

Matukio ya kutupa watoto wachanga yameendelea mkoani Morogoro ambapo mtoto mchanga wa siku moja ameuwa na kutupwa vichakani katika eneo la kichangani mjini Morogoro. Mtoto huyo mwenye jinsi ya kike anaonekana ametupwa kwa saa kadhaa zilizopita ambapo wakizungumzia tukio hilo baadhi ya mashuhuda wamelalamikia kuongezeka kwa matukio ya watoto wachanga kutupwa  ambapo wameomba wazazi kuwahurumia watoto   wasio na hatia huku baadhi ya wakinamama waliokuwepo katika tukio hilo wameonyesha kusikitishwa na kueleza wakati mwingine inatokana na baadhi ya wanaume kukwepa majukumu.   Naye mwenyekiti wa mtaa na diwani wa kata ya kichangani John Waziri walioshuhudia tukio hilo wamesema tukio hilo si la kuvumilika...

UKAWA WAITAKA SERIKALI KUSITISHA ZOEZI LA UPIGAJI KURA YA MAONI YA KATIBA PENDEKEZWA

Viongozi wa vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi UKAWA umeitaka serikali kusitisha zoezi la upigaji wa kura ya maoni ya katiba kutokana na zoezi hilo kutokidhi vigezo vya kisheria na badala yake ielekeze nguvu na rasilimali fedha katika zoezi la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura ili kuliepusha taifa kuingia katika machafuko. Viongozi wakuu wa vyama vinavyounda umoja huo wa katiba ya wananchi ukawa wakiongozwa na Profesa Ibrahimu Lipumba wa chama cha wananchi CUF na Freeman Mbowe wa chama cha demokrasia na maendeleo Chadema, chama cha NLD Dr Emmanuel Makaidi, chama cha NCCR mageuzi Mosena Nyambabe wameitoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam mbele ya waandishi wa habari.   Mwenyekiti wa...

JESHI LA POLISI LAPATA AIBU KUBWA, POLISI WAKE AKUTWA AKIFANYA MAPENZI HADHARANI AKIWA AMEVAA SARE ZA JESHI HILO

      Unakumbuka ile Stori ya askari Asuma Mpaji na Veronica Nazaremo kufukuzwa kazi Mkoani Kagera baada ya picha zao kusambaa mitandaoni wakionekana kupigana mabusu? safari hii nakuletea tena stori inayofanana na hiyo ambayo imetokea Nchini Uingereza. Polisi wa nchi hiyo ya Uingereza waliamua kumshtaki mwenzao baada ya kufanya kitendo cha kudhalilisha jeshi la nchi la nchi hiyo kwa kufanya tendo la ndoa tena mbele za watu akiwa na sare za kazi. Kitendo hicho kimemfanya kufukuzwa kazi bila kupewa taarifa za awali haraka baada ya kwenda kwenye shughuli zake za kila siku za usalama na kufanya kitendo hicho huku akijua ni kinyume na sheria tena akiwa amezungukwa na watu. Msaidizi mkuu wa kituo...

SERIKALI ISIMAMIE VYEMA HAKI ZA BINADAMU KWA KUSHIRIKIANA NA SEKTA BINAFSI

   waandishi wa habari kutoka mikoa ya nyanda za juu kusini wakipata mafunzo ya kupinga unyanyasaji wa kijinsia yanayoendeshwa na TAMWA CHAMA cha Waandishi wa habari Wanawake (TAMWA) kimeishauri serikali  kusimamia vyema haki za binadamu, sambamba na kutoa adhabu kali kwa ajili ya kutatua tatizo la unyanyasaji wa kijinsia nchini. Vilevile waandishi wa habari nchini wametoa ombi kwa baraza la habari Tanzania (MCT) pamoja na TAMWA kufikiria kuziwezesha klabu za waandishi wa habari za mikoani vyombo vya usafiri ili kusaidia kutumia vyombo vya usafiri wa viongozi (sources). Hayo yalisemwa jana katika semina ya Tamwa iliyofanyika mjini hapa na kuwashirikisha waandishi wa habari kutoka...

Wednesday, February 25, 2015

FFU watumia mabomu kutuliZa vurugu Ilula ,magari yachomwa moto ,mahabusu waachiwa silaha zaporwa

Askari wa FFU wamelazimika kutumia mabomu ya machozi kutuliza vurugu  kubwa zilizoibuka leo Kati ya Polisi na wananchi wa mjini wa Ilula katika wilaya ya Kilolo mkoani Iringa kufuatia kifo chenye utata cha mwanamke mmoja Tukio hilo limetokea majira ya saa 5 asubuhi Leo na kudumu hadi Majira ya saa 10 jioni huku kituo cha Polisi kikivunjwa ,bunduki kuporwa na nyingine kuchomwa moto pamoja na magari matatu na Pikipiki Moja ya polisi. Wakielezea tukio hilo wakazi wa mji wa Ilula wameueleza mtandao huu wa www.matukiodaima.co.tz kuwa  chanzo ni askari watatu watatu akiwemo mkuu wa kituo cha Ilula kwenda kufanya msako wa wananchi wanaokunywa pombe muda wa kazi. Hivyo kutokana na tukio hilo mwanamke huyo...

KIJANA WA KITANZANIA AUNDA REDIO STESHENI

 - SHUJAAZ! DJ Tee (19) ni kijana mwenye ndoto kubwa katika maisha yake. Baada ya kuona mahangaiko ya vijana kuelekea kwenye mafanikio, wengi wakiwa wamemaliza shule na vyuo bila kupata kazi, ameamua kuunda redio stesheni ghetoni kwake aliyoipa jina la Shujaaz, ili aweze kushea ideas na vijana wote nchini Tanzania kuhusu mbinu mbalimbali za kuingiza pesa, kuwapa stori za vijana wanaochakarika katika maisha yao pamoja na kuwaburudisha. "Nimeamua kuiita Shujaaz kwa sababu, naamini kuwa kijana ambaye anajituma na kuweka mfano bora kwenye jamii ni shujaa". Alisema DJ Tee. "Ndoto zangu zinakaribia kuwa kweli". Story ya kijana huyu inapatikana kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi kupitia kijarida cha Shujaaz, kitakachokuwa kinasambazwa...

WATANZANIA WAASWA KUTHAMINI BIDHAA ZINAZOZALISHWA NDANI YA NCHI

KAIMU MENEJA WA SIDO MKOA WA IRINGA, MR NIKO MAHINYA AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI OFINI KWAKE KAIMU MENEJA WA SIDO MKOANI IRINGA, NIKO MAHINYA AKIWA NA MHANDISI WA KARAKANA YA SIDO IRINGA, MICHAEL MATONYA WAKATI WAKITEMBELEA UTENDAJI KAZI WA KARAKANA HIYO FUNDI WA KARAKANA YA SIDO ELAYSON TARIMO AKIANGALIA MASHINE YA KUNOA VYUMA, AMBAYO ILIKUWA IKINOA MAJEMBE YA KUKATIA CHAI MSIMAMIZI WA KARAKANA YA KUTENGENEZEA MASHINE MBALIMBALI YA SIDO MKOANI IRINGA, LEONARD LUMATO AKIENDELEA NA KAZI KATIKA KARAKANA HIYO KIJANA AKIENDELEA NA KAZI NDANI YA KARAKANA NA FRANK KIBIKI, IRINGA SHIRIKA la kuhudumia viwanda vidogo (SIDO), mkoani Iringa limewataka watanzania kujenga utamaduni...

Tuesday, February 24, 2015

CHAMA CHA ALBINO KUMSHITAKI RAIS KIKWETE UMOJA WA MATAIFA.

Msemaji wa Chama cha Albino Tanzania (TAS), Josephat Torner CHAMA cha Albino Tanzania (TAS), kimetoa miezi mitatu kwa Rais Jakaya Kikwete kuingilia kati vitendo vya mauaji ya albino yanayoendelea nchini. Akishindwa kuchukua hatua, watamshitaki Umoja wa Mataifa (UN). Akizungumza Afisa Habari wa TAS, Josephat Torner amesema, wamechoshwa na vitendo vya mauaji ya albino vinavyoendelea huku Rais Kikwete akiwa kimya. Torner amesema Rais Kikwete ni rais wa Watanzania wote hivyo analazimika kukomesha mauaji ya albino na akishindwa kuchukua hatua katika kipindi hicho walichompa watapeleka malalamiko yao UN. Alisema watalazimika kufika huko kwani chama chao kimesajiliwa chini ya UN hivyo wakishindwa kusaidia wa Rais Kikwete watalazimika...

MTANDAO WA HAKI ZA BINADAMU WATOA TAMKO JUU YA KUTEKWA NA KUTESWA KWA KIONGOZI WA WAHITIMU JKT

Mwenyekiti wa JKT Tanzania, Bw. George Mgoba akiwa wodini. TAMKO KWA VYOMBO VYA HABARI.docx by mobl...

TAMWA YATOA MAFUNZO KWA WANAHABARI WA MIKOA YA NYANDA ZA JUU KUSINI JUU YA KUPAMBANA NA UNYANYASAJI WA KIJINSIA

WENCE AKITOA ELIMU KWA WANAHABARI WALIOKUTANA MKOANI IRINGA WANAHABARI NWAKIWA MAKINI KUMSIKILIZA MTOA ELIMU MWANAHABARI FRANK KIBIKI AKIWA MAKINI KUFUATILIA NINI KINACHOENDELEA KWENYE MAFUNZO HAYO  na fredy mgunda,iringa Waandishi wa habari wametakiwa kuandika zaidi habari zinazohusu unyanyasaji wa kijinsia hususan dhidi ya wanawake na watoto ili kuiamsha zaidi jamii inayowafanyiwa vitendo hivyo na mamlaka husika ziweze kuchukua hatua za kisheria dhidi ya vitendo hivyo. Msisitizo huo ulitolewa na chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (Tamwa) kwa waandishi wa habari wa mikoa ya nyanda za juu kusini (IRINGA,MBEYA,SONGEA NA NJOMBE) ambapo wanahabari wameombwa kuendelea kufichua habari hizo hususan kwa wanaofanyiwa...

Friday, February 20, 2015

JAY Z NA MTOTO NJE YA NDOA

Skendo haziko mbali  na kivuli cha staa, hii iko duniani kote na safari hii imemkuta jamaa ambaye wengi wanaofanya Hip Hop wanamuangalia kama model wao, kutokana na nguvu yake kubwa kwenye muziki huo, leo zimeanza kusikika za upande wa pili ambazo huenda hattukuwahi kuzisikia siku za nyuma. Shawn Corey Carter ama Jay Z tunajua kuwa ana ndoa na mpenzi wake ambaye ni Beyonce na wana mtoto mmoj...

Page 1 of 69412345Next
Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More