Thursday, February 2, 2017

JUMLA YA HATI ZA KIMILA 810 ZATOLEWA KWA WANANCHI WA KIJIJI CHA KINYWANG’ANGA MKOANI IRINGA

  waziri wa ardhi na makazi WILIAMU LUKUVI  ambaye ni mbunge wa jimbo la Ismani na Mkurugenzi Msaidizi wa USAID Tanzania, David Thompson alisema USAID wakikabdhi hati za kimila kwa wananchi wa kijiji cha kinywang'anga mkoani iringa
 

na fredy mgunda,Iringa

Wizara ya ardhi nyumba na maendeleo ya makazi imetoa jumla ya hati za kimila 810 kwa wananchi wa kijiji cha kinywang’anga kilichopo tarafa ya ismani mkoani Iringa ili kupunguza migogoro ya ardhi,hati hizo zinazotolewa kupitia Mradi wa Urasimishaji Ardhi (LTA) unaofanywa chini ya mpango wa Feed The Future kwa ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID). .



Akizungumza na wananchi wa kijiji cha kinywang’anga waziri wa ardhi na makazi WILIAMU LUKUVI  ambaye ni mbunge wa jimbo la Ismani alisema kuwa mpango huu wa kurasimisha ardhi kimila utakuwa na faida kubwa kwa wananchi na kukuza dhamani ya ardhi zao.

Akikabidhi hati hizo, Waziri Lukuvi aliupongeza mpango huo akisema utasaidia kupunguza eneo kubwa la ardhi ya Tanzania ambayo haijapimwa.



“Ni asilimia 15 tu ya ardhi yetu nchini imepimwa, kuna vipande vya ardhi zaidi ya milioni 12 vinatakiwa kupimwa lakini hadi sasa vilivyopimwa ni kama 400,000 hivi,” alisema.



Akiwapigia magoti USAID, Lukuvi aliwaomba wautanue mradi huo angalau ufike katika mikoa 10 huku akizikumbusha halmashauri nchini kote kila mwaka kuvitengenezea vijiji vitano hadi 10 mpango wa matumizi bora ya ardhi.



“Tunataka katika kipindi cha miaka 10 kutoka sasa ardhi yote ya Tanzania iwe na mipango ya matumizi bora na ipimwe ili kila mwenye kipande chake cha ardhi awe na hati yake,” alisema.



Wakati mipango hiyo ikiendelea, waziri huyo alisema sera ya ardhi ya mwaka 1995 imefanyiwa marekebisho makubwa yatakayoleta sera mpya ya mwaka 2017.



Alisema kwa kupitia sera hiyo, kutakuwa na usimamizi zaidi wa ulinzi wa ardhi ya watu masikini ili kupunguza uporaji wa rasilimali hiyo unaofanywa na matajiri.



“Marekebisho ya sera hiyo ya ardhi yatawezesha pia kufanyika kwa mrekebisho ya sheria mbalimbali za ardhi ili ziendane na sera na mazingira ya sasa,” alisema.



Aliwataka wananchi wanaondelea kupata hati miliki za kimila za ardhi kuzitumia kupata mikopo kutoka katika taasisi mbalimbali za fedha ili kuchochea maendeleo yao badala ya kusubiri pembejeo za ruzuku.









Mkurugenzi Msaidizi wa USAID Tanzania, David Thompson alisema USAID inafadhili mpango huo ili kuisaidia Tanzania kuwa na mfumo mzuri na wazi wa kulinda haki ya kumiliki ardhi kwa raia wote, wanaume na wanawake.



“Usajili wa ardhi ni muhimu kwasababu unaongeza ulinzi wa umiliki wa ardhi, unawezesha uwekezaji, unaongeza thamani ya ardhi na unapunguza migogoro ya ardhi,” alisema.



Thompson alisema Kinywang’anga ni moja kati ya vijiji 41 vya mikoa ya Iringa na Mbeya vitakavyonufaika na mradi huo wa miaka minne utakaopima na kutoa hati miliki za kimila zaidi ya 70,000 kwa wananchi wa vijiji hivyo.



Awali Meneja Msaidizi wa LTA, Malaki Msigwa alisema kati ya vijiji hivyo 41 vitakavyotayarishiwa mipango ya matumizi bora ya ardhi na kila mwenye ardhi kupimiwa na kupewa hati miliki za kimila, vijiji 36 vipo wilayani Iringa na vitano vipo wilayani Mbeya.




“Bada ya kukamilisha zoezi la upimaji mashamba na urasimishaji wa kijiji chote cha Kinywang’anga, hivi sasa mradi unaendelea na upimaji mashamba katika vijiji vya Kiponzero, Magunga na Usengelindete wilayani Iringa.”

MSIGWA aliongeza kuwa lengo la mradi ni kuhakikisha wanapunguza migogoro ya ardhi kwa wananchi wa vijijini.

Nao wananchi wa kijiji cha kinywang’anga waliwashukuru wafadhili pamoja na wizara ya ardhi na makzi kwa kuwasaidia kupata hati ambazo zitakuwa na faida nyingi kwao.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More