Tuesday, September 16, 2025

TRA NACHINGWEA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAJASIRIAMALI WADOGO

Meneja wa TRA wilaya ya Nachingwea, Novatus Chamu akielezea namna dawati hilo litakavyo kuwa chombo muhimu cha kusikiliza kero, kutoa elimu ya kodi na ushauri wa kukuza mitaji kwa wajasiriamali wadogo.
Meneja wa TRA wilaya ya Nachingwea, Novatus Chamu akiwa kwenye picha pamoja na mgeni rasmi Stella kategile na baadhi ya watumishi wa TRA Nachingwea 
Mgeni rasmi Stella kategile akikataa utepe kuzindua rasmi dawati la TRA kwa ajili ya kusikiliza,kutoa huduma na elimu kwa wajasiriamali wadogo wadogo wa wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi.
Meneja wa TRA wilaya ya Nachingwea, Novatus Chamu akiwa kwenye picha pamoja na mgeni rasmi Stella kategile na baadhi ya wajasiriamali wadogo wadogo wa wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi.


Na Fredy Mgunda, Nachingwea Lindi.

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wilayani Nachingwea imezindua rasmi dawati maalum la kushughulikia changamoto za wajasiriamali wadogo, ikiwa ni hatua ya kuwawezesha kiuchumi na kuwainua kutoka ngazi ya chini ya biashara hadi kuwa wafanyabiashara wakubwa.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Meneja wa TRA wilaya ya Nachingwea, Novatus Chamu, alisema kuwa dawati hilo litakuwa chombo muhimu cha kusikiliza kero, kutoa elimu ya kodi, na ushauri wa kukuza mitaji kwa wajasiriamali wadogo.

“Kupitia dawati hili, tutaweza kusikiliza kero zao moja kwa moja, kuwapa elimu ya kodi na pia kuwashauri namna ya kukuza mitaji yao ili waweze kuchangia pato la taifa kwa ufanisi zaidi,” alisema Chamu.

Aliongeza kuwa hatua hiyo ni sehemu ya juhudi za serikali kusogeza huduma karibu na wananchi, hasa wale waliopo kwenye sekta isiyo rasmi ambao mara nyingi hukumbwa na changamoto ya uelewa mdogo kuhusu masuala ya kodi na taratibu za biashara.

Kwa upande wake, mgeni rasmi katika uzinduzi huo, Stella Kategile, alieleza kuwa dawati hilo ni jukwaa muhimu la kukuza uchumi wa wafanyabiashara wadogo. Alisisitiza kuwa serikali inalenga kuwawezesha wajasiriamali kupitia utatuzi wa changamoto zao badala ya kuwabana kwa kodi bila kuelewa hali zao halisi.

“Lengo la serikali siyo kukusanya kodi tu, bali pia kusikiliza na kutatua changamoto za wajasiriamali ili waweze kukua na kuchangia kikamilifu katika pato la taifa,” alisema Kategile.

Baadhi ya wajasiriamali waliopata fursa ya kuzungumza walipongeza hatua hiyo ya TRA, wakisema kuwa imekuja kwa wakati muafaka kwani changamoto nyingi zimekuwa zikiwakwamisha katika kuendeleza biashara zao.

“Kwa muda mrefu tumekuwa hatuna pa kupaza sauti zetu. Kupitia dawati hili, tuna matumaini kuwa sauti zetu zitasikika na biashara zetu zitakua,” alisema mmoja wa wajasiriamali hao.

Dawati hilo linatarajiwa kuwa kiunganishi muhimu kati ya TRA na wajasiriamali, na mchango wake unatarajiwa kuleta mabadiliko chanya katika muktadha wa ukusanyaji wa mapato na ukuaji wa sekta ya biashara nchini.


Thursday, September 11, 2025

BALOZI SIRRO;AWATAKA WANANCHI KULINDA AMANI ILIYOPO KIPINDI HIKI CHA UCHAGUZI.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Mhe. Balozi Simon Sirro amesema kuwa jiografia ya Kigoma inayopakana na Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, inaifanya mkoa huo kuwa na nafasi nyeti katika kudumisha amani. Akisisitiza kuwa amani si hiari bali ni sharti la msingi kwa ustawi wa wananchi.
Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Mhe. Balozi Simon Sirro amesema kuwa jiografia ya Kigoma inayopakana na Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, inaifanya mkoa huo kuwa na nafasi nyeti katika kudumisha amani. Akisisitiza kuwa amani si hiari bali ni sharti la msingi kwa ustawi wa wananchi.
Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Mhe. Balozi Simon Sirro amesema kuwa jiografia ya Kigoma inayopakana na Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, inaifanya mkoa huo kuwa na nafasi nyeti katika kudumisha amani. Akisisitiza kuwa amani si hiari bali ni sharti la msingi kwa ustawi wa wananchi.

Na Fredy Mgunda,Kigoma.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Mhe. Balozi Simon Sirro amesema kuwa jiografia ya Kigoma inayopakana na Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, inaifanya mkoa huo kuwa na nafasi nyeti katika kudumisha amani. Akisisitiza kuwa amani si hiari bali ni sharti la msingi kwa ustawi wa wananchi.


Balozi Sirro ametoa kauli hiyo, wakati wa Kongamano la kuliombea taifa Amani katika Uchaguzi Mkuu 2025 lililofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu Kasulu (TCC), lililoandaliwa na Kamati ya Maridhiano kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kasulu.


“Bila amani, biashara ya mipakani haiwezi kustawi, wananchi hawawezi kuendeleza shughuli zao za kilimo, uvuvi na biashara ndogo ndogo. Amani ndiyo uti wa mgongo wa maendeleo ya Kigoma na Tanzania kwa ujumla,” amesema.

Ameongeza kuwa viongozi wa dini wanapaswa kuepuka kutumia nyumba za ibada kama majukwaa ya kisiasa, kwani kuchanganya masuala ya dini na siasa kunaweza kuhatarisha mshikamano wa kijamii.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Mhe. Kanali Isaac Mwakisu, amewashukuru viongozi wa dini kwa kushirikiana na serikali katika matukio mbalimbali na kuwataka waendelee kuwaombea viongozi ili watoe maamuzi yenye busara kwa wananchi.

Naye Katibu wa Kamati ya Maridhiano Wilaya ya Kasulu Sheikh Nasib Rajab kutoka dhehebu la SHIA, amesema kongamano hilo limeonesha mshikamano wa wananchi licha ya tofauti za kiitikadi, jambo linalosaidia kuimarisha umoja na mshikamanano.

Vilevile, Askofu wa Kanisa la FPCT Jimbo la Kasulu, Shadrack Bunono, alibainisha kuwa mtu anayekalia kiti cha mamlaka anapaswa kutumia busara na hekima katika maamuzi yake kwa manufaa ya wananchi, na kusisitiza kuwa sala na maombi kwa viongozi ni msingi wa mafanikio katika wilaya hiyo.

Saturday, September 6, 2025

KASULU YAANDAA BONANZA LA MICHEZO KUHAMASISHA UCHAGUZI NA MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU

Mkuu wa Wilaya ya Kasulu,mkoani Kigoma, Mhe. Kanali Isaac Mwakisu, amesema wananchi wanapaswa kujitokeza kwa wingi kushiriki mapokezi ya Mwenge wa Uhuru pamoja na Uchaguzi Mkuu ujao, kwani matukio hayo ni ya kitaifa na yanabeba taswira ya mshikamano wa Watanzania.

Baadhi ya viongozi na wananchi waliojitokeza kwenye bonanza hilo
Mkuu wa Wilaya ya Kasulu,mkoani Kigoma, Mhe. Kanali Isaac Mwakisu na katibu tawala Theresia Mtewele wakishiriki katika bonanza kwa ajili ya mapokezi ya Mwenge wa Uhuru pamoja pamoja na kuhamasishwa wananchi kushiriki Uchaguzi Mkuu ujao, 


Na Fredy Mgunda, Kigoma.

Mkuu wa Wilaya ya Kasulu,mkoani Kigoma, Mhe. Kanali Isaac Mwakisu, amesema wananchi wanapaswa kujitokeza kwa wingi kushiriki mapokezi ya Mwenge wa Uhuru pamoja na Uchaguzi Mkuu ujao, kwani matukio hayo ni ya kitaifa na yanabeba taswira ya mshikamano wa Watanzania.


Akizungumza leo Jumamosi, Septemba 6, 2025, katika bonanza la michezo mbalimbali lililofanyika Viwanja vya Shule ya Msingi Kiganamo, Kanali Mwakisu amesema Mwenge wa Uhuru utakimbizwa wilayani humo Septemba 17 na 18, ambapo siku ya kwanza utapokelewa Kasulu Vijijini eneo la Mvugwe na siku inayofuata itakuwa Kasulu Mjini.


“Maudhui makuu ya bonanza hili ni kuwakumbusha wananchi kuwa Mwenge utakimbizwa katika wilaya yetu, na tunapaswa kushiriki kwa wingi ili kuonesha mshikamano na kuthamini amani na utulivu wa nchi yetu,” amesema.


Amesema kuwa Mwenge wa Uhuru ni tunu kubwa ya taifa, na wananchi wanapojitokeza kuupokea kwa shangwe ni kielelezo cha kuthamini amani na utulivu kwa mustakabali wa maendeleo ya nchi.


Aidha, amewakumbusha kuwa kwa mujibu wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Uchaguzi Mkuu utafanyika Oktoba 29, 2025, hivyo wananchi wanatakiwa kujitokeza kwa wingi baada ya kusikiliza sera za wagombea na kuwachagua viongozi wanaowataka.


Mmoja wa wananchi, Nelstella Kihoza, akizungumza na mwandishi wetu amesema kuwa umati mkubwa uliofurika viwanjani hapo ni ishara tosha ya mwamko wa wananchi wa Kasulu, na kwamba watajitokeza kwa wingi kushiriki Uchaguzi Mkuu kwa kuchagua viongozi wanaowataka, sambamba na kushiriki kikamilifu katika Mbio za Mwenge wa Uhuru.


Naye Mwalimu Yusufu Hamisi amrmpongeza Mkuu wa Wilaya kwa ubunifu wa kuandaa bonanza hilo, akisema limempa ari ya kuendelea kuhamasisha wananchi wengine kushiriki kikamilifu matukio hayo mawili muhimu ya kitaifa.

Wednesday, July 16, 2025

WANANCHI NACHINGWEA WANUFAIKA NA MIKOPO NAFUU, WAIKIMBIA "KAUSHA DAMU"

Mkurugezi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Nachingwea Mhandisi chionda Kawawa akimkabidhi bajaji ya mkopo ya asilimia 10 ndugu Hamis Chilumba ikiwa ni sehemu ya shilingi milioni 649,781,998 zilizotolewa na Halmshauri hiyo akiwa sambamba na Mkuu wa Kitengo cha Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri hiyo, Bi Stella Kategile
Mkurugezi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Nachingwea Mhandisi chionda Kawawa akimkabidhi Guta ya mkopo ya asilimia 10 ndugu Zawadi Kanga ikiwa ni sehemu ya shilingi milioni 649,781,998 zilizotolewa na Halmshauri hiyo
Mkurugezi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Nachingwea Mhandisi chionda Kawawa akiwakabidhi pikipiki za miguu miwili maarufu bodaboda kwa kikundi cha vijana ikiwa ni mkopo wa asilimia 10 ndugu  ikiwa ni sehemu ya shilingi milioni 649,781,998 zilizotolewa na Halmshauri hiyo


Na Fredy Mgunda, Nachingwea, Lindi.


Mikopo yenye riba kubwa, maarufu kama mikopo ya kausha damu, imekuwa kizingiti kikubwa kwa maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi wengi nchini, hasa wafanyabiashara wadogo. Riba kubwa na masharti magumu ya urejeshaji yamewafanya wengi kupoteza mitaji na biashara zao.

Hata hivyo, nuru imeonekana kwa baadhi ya wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea, mkoani Lindi, baada ya serikali kuanzisha mpango wa utoaji wa mikopo isiyo na riba kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kupitia asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri.

Wananchi waliopokea mikopo hiyo, wakiwemo Zawadi Kanga, Ashura Chingu, Husura Mponga na Ramadhani Nambunga – wameeleza jinsi fedha hizo zilivyowasaidia kuondokana na adha ya mikopo yenye masharti kandamizi kutoka kwa taasisi binafsi na mabenki.

“Mikopo hii ya asilimia 10 ni tofauti kabisa. Hatunyonywi tena kama zamani. Tunafanya biashara kwa amani na kurejesha kwa mpangilio mzuri,” alisema mmoja wa wanufaika.

Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi hundi kwa vikundi mbalimbali, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea, Mhandisi Chionda Kawawa, alisema kuwa mpango huo ni sehemu ya mkakati wa serikali ya awamu ya sita wa kuwawezesha wananchi kiuchumi.

“Mikopo ya kausha damu imekuwa kikwazo kikubwa kwa maendeleo ya wananchi wetu. Halmashauri imedhamiria kuwa sehemu ya suluhisho kwa kutoa mikopo isiyo na riba ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi ya wananchi,” alisema Mhandisi Kawawa.

Kwa mujibu wa Kawawa, jumla ya shilingi 649,781,998 zimetolewa kwa vikundi 54 vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, ili kuwainua kiuchumi na kuchangia pato la taifa kupitia shughuli zao za uzalishaji.

Aidha, aliwataka wanufaika kutumia fedha hizo kwa uangalifu na kurudisha mikopo kwa wakati ili kuwezesha mzunguko wa fedha kwa vikundi vingine.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri hiyo, Bi Stella Kategile, aliwakumbusha wanavikundi umuhimu wa uaminifu na nidhamu ya fedha.

“Wakirejesha kwa wakati, watakuwa wamefungua milango kwa wengine kunufaika. Pia, wataweza kukopa zaidi ya walichopata awali,” alisisitiza Bi Kategile.

Mpango huu wa mikopo isiyo na riba unatajwa kuwa mfano wa kuigwa katika kupunguza utegemezi na kuongeza ushiriki wa wananchi katika shughuli za kiuchumi vijijini.


Tuesday, June 17, 2025

TFS YAJIDHATITI KUKABILIANA NA MAJANGA YA MOTO MSITUNI

Baadhi ya vijana wakipewa mafunzo ya utimamamu wa mwili kwa ajili ya kulinda na kuzuia mtoto usiharibu miti ya mashamba ya miti Sao Hill.Baadhi ya vijana wakipewa mafunzo ya utimamamu wa mwili kwa ajili ya kulinda na kuzuia mtoto usiharibu miti ya mashamba ya miti Sao Hill.Baadhi ya vijana wakipewa mafunzo ya utimamamu wa mwili kwa ajili ya kulinda na kuzuia mtoto usiharibu miti ya mashamba ya miti Sao Hill.





Na Fredy Mgunda,Mufindi

Ikiwa ni kuelekea msimu wa kipindi cha kiangazi, Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania TFS kupitia Shamba la Miti Sao Hill umeendesha zoezi la usahili kwa watumishi wa muda watakaounda kikosi maalumu kwa  ajili ya kupambana na kudhibiti majanga ya moto katika maeneo yanayolizunguka Shamba.


Zoezi hilo limefanyika leo Juni 16, 2025 katika viwanja vya Shamba la Miti Sao Hill likishirikisha wahifadhi wa Shamba, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji pamoja na Jeshi la Polisi, likilenga kupata vikosi vitakavyohudumu katika Makao Makuu ya Shamba pamoja na Tarafa ya II ya Shamba Ihefu.


Akizungumza katika zoezi hilo Mhifadhi Mwandamizi anayesimamia Utumishi na Utawala Felista Bayo amesema kuwa katika mwaka wa fedha 2025/2026 Shamba linatarajia kuajiri watumishi wa muda 192 kwa ajili ya kukabiliana na kupambana na majanga ya moto kwa kipindi chote cha kiangazi.


Ameongeza kuwa licha ya maombi kuwa mengi kulinganisha na nafasi zilizotajwa, Shamba la Miti Sao aaHill lina shughuli nyingine zinazoendelea katika vituo vyake vyote ikiwa ni pamoja shughuli za bustani na usafi wa mashamba, hivyo wanaokosa nafasi katika vikosi hivyo wanapata fursa ya kuendelea na shuguli nyingine za Shamba.


Kwa upande wake Mhifadhi anayesimamia Kitengo cha Ulinzi wa Msitu dhidi ya moto Murya Sawa amesema kuwa baada ya kukamilisha zoezi hili ni matarajio ya TFS kupitia Shamba la Miti SaoHill kuwa watumshi hawa muda  waliopata nafasi watafanya kazi hiyo kwa weledi kwa kutanguliza uzalendo huku akihimiza ushirikiano baina ya wananchi wote wanaoishi karibu na maeneo ya hifadhi katika kulinda rasilimali za misitu.


Naye Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Wilaya ya Mufindi Ashery Kitundu amesema kuwa lengo mama la jeshi la zimamoto ni kuhakikisha matukio ya moto hayatokei kwa kutoa elimu, na kuyadhibiti pindi yanapotokea hivyo ni watumishi hawa wa muda watakuwa mabalozi wazuri katika maeneo yao waliyotoka kwa kushirikiana na jeshi la zimamoto katika kutoa elimu ya kuepuka na kukabilina na majanga ya moto.


Usaihili huo unatarijiwa kuendelea hapo kesho katika Tarafa ya Kwanza ya  Shamba Irundi kisha Tarafa ya Tatu Ihalimba, na Tarafa ya Nne Mgololo.

Thursday, June 12, 2025

VIJANA FANYENI MAZOEZI MARA KWA MARA KUIMARISHA AFYA

Katika ulimwengu wa leo unaokumbwa na changamoto nyingi za kiafya, viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Lindi wametoa wito maalum kwa vijana na wananchi wote kufanya mazoezi mara kwa mara kama njia ya kuimarisha afya na kuzuia magonjwa yasiyoambukiza. Wito huo umetolewa wakati wa maonyesho ya madini yanayoendelea katika viwanja vya madini wilayani Ruangwa.Katika ulimwengu wa leo unaokumbwa na changamoto nyingi za kiafya, viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Lindi wametoa wito maalum kwa vijana na wananchi wote kufanya mazoezi mara kwa mara kama njia ya kuimarisha afya na kuzuia magonjwa yasiyoambukiza. Wito huo umetolewa wakati wa maonyesho ya madini yanayoendelea katika viwanja vya madini wilayani Ruangwa.Katika ulimwengu wa leo unaokumbwa na changamoto nyingi za kiafya, viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Lindi wametoa wito maalum kwa vijana na wananchi wote kufanya mazoezi mara kwa mara kama njia ya kuimarisha afya na kuzuia magonjwa yasiyoambukiza. Wito huo umetolewa wakati wa maonyesho ya madini yanayoendelea katika viwanja vya madini wilayani Ruangwa.



Na Fredy Mgunda,Lindi.

Katika ulimwengu wa leo unaokumbwa na changamoto nyingi za kiafya, viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Lindi wametoa wito maalum kwa vijana na wananchi wote kufanya mazoezi mara kwa mara kama njia ya kuimarisha afya na kuzuia magonjwa yasiyoambukiza. Wito huo umetolewa wakati wa maonyesho ya madini yanayoendelea katika viwanja vya madini wilayani Ruangwa.

Viongozi hao wamebainisha kuwa afya njema siyo tu msingi wa maisha bora, bali pia ni mtaji muhimu kwa maendeleo ya mtu binafsi na taifa kwa ujumla.

“Afya bora ndiyo msingi wa maisha na maendeleo ya mtu binafsi na taifa. Tunapaswa kujenga utamaduni wa kufanya mazoezi kila wakati ili kuimarisha kinga ya mwili dhidi ya magonjwa mbalimbali,” walisisitiza viongozi hao.

Mazoezi ya mwili yameelezwa kuwa na faida lukuki ikiwa ni pamoja na kupunguza hatari ya kupata magonjwa ya moyo, kisukari, shinikizo la damu na unene uliopitiliza. 

Kwa vijana, mazoezi husaidia katika kujenga miili imara, kuimarisha uwezo wa kujifunza na kujiamini, na pia kupunguza msongo wa mawazo.

Pamoja na kutoa wito wa mazoezi, viongozi hao waliwahamasisha wananchi kuendelea kujitokeza kwa wingi katika maonyesho ya madini yanayoendelea, kwani yameleta fursa nyingi za kiuchumi na kielimu kwa wakazi wa Lindi na maeneo jirani.

 Maonyesho hayo yanalenga kuinua sekta ya madini kwa kuonesha teknolojia mpya, mbinu za usindikaji, pamoja na fursa za uwekezaji katika rasilimali za madini.

Kwa kuzingatia mchango mkubwa wa vijana katika maendeleo ya taifa, viongozi hao wamehimiza kuwa ni muhimu kwa vijana kuwekeza katika afya zao kupitia mazoezi na pia kutumia fursa kama hizi za maonyesho kupata maarifa yatakayowasaidia kuinua maisha yao na ya jamii kwa ujumla.

Mazoezi ya mwili ni njia rahisi na ya gharama nafuu ya kujilinda dhidi ya maradhi na kuimarisha afya. Viongozi wa Mkoa wa Lindi wameweka wazi kuwa ni wajibu wa kila mmoja, hasa vijana, kuchukua hatua na kuwa mabalozi wa afya bora kupitia mazoezi ya mara kwa mara. 

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI ZANZIBAR AZINDUA MAONYESHO YA MADINI LINDI

Waziri wa Nishati na Madini wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mheshimiwa Shaibu Hassan Kaduara, amezindua rasmi awamu ya pili ya Maonyesho ya Madini (Lindi Mining Expo) mkoani Lindi, yakilenga kuvutia wawekezaji na kutangaza fursa mbalimbali za rasilimali madini zinazopatikana mkoani humo.
Waziri wa Nishati na Madini wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mheshimiwa Shaibu Hassan Kaduara, amezindua rasmi awamu ya pili ya Maonyesho ya Madini (Lindi Mining Expo) mkoani Lindi, yakilenga kuvutia wawekezaji na kutangaza fursa mbalimbali za rasilimali madini zinazopatikana mkoani humo.
Waziri wa Nishati na Madini wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mheshimiwa Shaibu Hassan Kaduara, amezindua rasmi awamu ya pili ya Maonyesho ya Madini (Lindi Mining Expo) mkoani Lindi, yakilenga kuvutia wawekezaji na kutangaza fursa mbalimbali za rasilimali madini zinazopatikana mkoani humo.
Waziri wa Nishati na Madini wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mheshimiwa Shaibu Hassan Kaduara, amezindua rasmi awamu ya pili ya Maonyesho ya Madini (Lindi Mining Expo) mkoani Lindi, yakilenga kuvutia wawekezaji na kutangaza fursa mbalimbali za rasilimali madini zinazopatikana mkoani humo.

Na Fredy Mgunda, Ruangwa, Lindi.


Waziri wa Nishati na Madini wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mheshimiwa Shaibu Hassan Kaduara, amezindua rasmi awamu ya pili ya Maonyesho ya Madini (Lindi Mining Expo) mkoani Lindi, yakilenga kuvutia wawekezaji na kutangaza fursa mbalimbali za rasilimali madini zinazopatikana mkoani humo.


Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Waziri Kaduara alisema thamani ya dhahabu imeendelea kupanda katika soko la dunia kutokana na athari za vita kati ya Urusi na Ukraine, ambako dhahabu inayozalishwa na Urusi imewekewa vikwazo kuingia katika masoko ya kimataifa.


"Sera ya Taifa ya Uwekezaji ya 1996, pamoja na Sera ya Maendeleo ya Viwanda ya 1996–2020 na ile ya Viwanda Vidogo ya mwaka 2003, zipo kwenye mchakato wa kupitia upya kwa lengo la kuendana na mahitaji ya sasa ya maendeleo ya kimkakati," alisema Kaduara.


Waziri huyo alibainisha kuwa miradi ya madini ni miongoni mwa miradi ya kimkakati nchini, ambayo inaendelea kufanyiwa tathmini kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya sera mpya itakayowezesha Watanzania kunufaika zaidi na sekta hiyo.


Lindi Yajitokeza Kama Kitovu cha Madini Nchini

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mheshimiwa Zainab Telack, alisema mkoa huo umebarikiwa kuwa na rasilimali kubwa za madini ambazo tayari zimeanza kuwanufaisha wananchi moja kwa moja.


“Maonyesho haya yanafungua milango kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi. Yanachochea uchumi wa eneo hili na kuongeza thamani ya madini tunayochimba,” alisema RC Telack.


Aliongeza kuwa maonyesho ya awamu ya kwanza mwaka 2023 yalivutia wageni kutoka mataifa 14 na zaidi ya watu 6,000 walihudhuria, jambo lililoongeza hadhi ya Lindi kama eneo la kimkakati kwa shughuli za madini nchini.


“Kwa sasa tunaona ongezeko la wawekezaji, uboreshaji wa miundombinu na fursa za ajira, hali inayodhihirisha kuwa Lindi ni sehemu muhimu katika ajenda ya maendeleo ya taifa,” aliongeza.


Ongezeko la Wachimbaji na Teknolojia ya Uchimbaji

Kwa mujibu wa Mratibu wa Maonyesho hayo, Bw. Mwinjuma Mkungu, ambaye ni Katibu Tawala Msaidizi Uchumi mkoani Lindi, idadi ya wachimbaji imeongezeka kutoka 2,265 hadi 2,948 baada ya maonyesho ya kwanza, huku mitambo ya kisasa ya uchimbaji ikiongezeka pia.


“Tumeona ongezeko kubwa la wawekezaji na mapato ya serikali yameongezeka kwa asilimia 10.1 baada ya maonyesho ya awali. Hii inaonyesha mchango wa moja kwa moja wa maonyesho haya kwa uchumi wa taifa,” alisema Mkungu.


Alfred Chilumba, mchimbaji mdogo, alishuhudia mabadiliko makubwa baada ya kupata elimu kupitia maonyesho ya awali.


“Tulikuwa hatujui kama tunaweza kutumia mitambo ya kisasa. Maonyesho haya yametufungua macho,” alisema.


Anna Milanzi, mama lishe anayehudumu kwenye maonyesho hayo, alisema ametumia fursa ya ongezeko la wageni kuongeza kipato chake.


“Kwa siku za kawaida napika kilo 5 za unga, lakini leo nimepika kilo 15. Biashara imenoga,” alisema kwa furaha.


Maonyesho Yadumu kwa Siku Kadhaa

Maonyesho hayo ya siku kadhaa yanahusisha maonesho ya bidhaa za madini, teknolojia mpya za uchimbaji, warsha za kitaalamu, na majadiliano baina ya serikali, wawekezaji na wachimbaji wadogo.


Yamebeba kauli mbiu: “Madini na Uwekezaji wa Fursa za Kiuchumi Lindi – Shiriki Uchaguzi Mkuu 2025”, yakisisitiza uhusiano kati ya maendeleo ya sekta ya madini na ushiriki wa wananchi katika mustakabali wa taifa.

Monday, May 19, 2025

MADAKTARI BINGWA 47 WATIA NANGA MKOANI LINDI KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA

Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Bi. Zuwena Omary akizunguza wakati  kuwapokea rasmi madaktari bingwa 47 chini ya mpango wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, awamu ya tatu, kwa ajili ya kutoa huduma za kibingwa katika hospitali zote za wilaya ndani ya mkoa huo.
Baadhi ya Madaktari bingwa ambao wamewasili mkoani Lindi kwa ajili ya kutoa huduma za kibingwa kwa wananchi wote mkoani.

Na Fredy Mgunda, Lindi.

Serikali ya Mkoa wa Lindi imewapokea rasmi madaktari bingwa 47 chini ya mpango wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, awamu ya tatu, kwa ajili ya kutoa huduma za kibingwa katika hospitali zote za wilaya ndani ya mkoa huo.


Akizungumza wakati wa mapokezi hayo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Bi. Zuwena Omary, alisema kuwa ujio wa madaktari hao ni sehemu ya jitihada za serikali kusogeza huduma za afya karibu na wananchi, hasa wale walioko maeneo ya vijijini ambako awali walilazimika kusafiri mbali kupata huduma za kibingwa.


“Huduma hizi zitapatikana katika maeneo saba ndani ya mkoa kwa siku sita mfululizo kuanzia leo. Lengo ni kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma bora na kwa wakati,” alisema Bi. Omary.


Aliongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imekuwa mstari wa mbele kuboresha sekta ya afya kwa kujenga miundombinu ya kisasa, kununua vifaa tiba vya kisasa, pamoja na kuongeza wataalamu mbalimbali wa afya nchini.


Kwa upande wake, Mratibu wa timu hiyo ya madaktari, Michael Mbele, alieleza kuwa madaktari hao wamejipanga kikamilifu kutoa huduma zote muhimu za afya kwa wananchi wote, bila ubaguzi, katika hospitali za wilaya walizopangiwa.


“Tumewakilishwa na wataalamu wa kada zote za afya, kuanzia magonjwa ya ndani, watoto, wanawake, upasuaji na hata huduma za kisaikolojia. Huduma zote hizi sasa zitapatikana katika hospitali za wilaya,” alisema Mbele.


Wananchi wa Mkoa wa Lindi waliopata fursa ya kuhudumiwa walieleza furaha na shukrani kwa serikali, hususan kwa Mheshimiwa Rais, kwa kuendelea kuboresha huduma za afya nchini, hatua ambayo wameitaja kama ya kipekee na ya kupongezwa.

Thursday, May 15, 2025

BARAZA LA MADIWANI KASULU LIMEMCHANGIA MILIONI 1 RAIS DKT SAMIA KWA AJILI YA KUCHUKUA FOMU YA KUGOMBEA TENA URAIS.

Baraza la Madiwani na Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu limemshukuru na kumpongeza Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kutokana na kazi kubwa ambapo wamechangia kiasi cha  shilingi 1,000,000  kwa ajili  ya kuchukua fomu ya kugombea Urais kwa Mhe.Rais na shilingi 577,000 kwa ajili ya Mbunge wa Jimbo la Kasulu Vijijini,Mhe.Vuma Olle  kuchukua fomu ya kugombea ubunge
Baraza la Madiwani na Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu limemshukuru na kumpongeza Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kutokana na kazi kubwa ambapo wamechangia kiasi cha  shilingi 1,000,000  kwa ajili  ya kuchukua fomu ya kugombea Urais kwa Mhe.Rais na shilingi 577,000 kwa ajili ya Mbunge wa Jimbo la Kasulu Vijijini,Mhe.Vuma Olle  kuchukua fomu ya kugombea ubunge
Baraza la Madiwani na Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu limemshukuru na kumpongeza Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kutokana na kazi kubwa ambapo wamechangia kiasi cha  shilingi 1,000,000  kwa ajili  ya kuchukua fomu ya kugombea Urais kwa Mhe.Rais na shilingi 577,000 kwa ajili ya Mbunge wa Jimbo la Kasulu Vijijini,Mhe.Vuma Olle  kuchukua fomu ya kugombea ubunge



Baraza la Madiwani na Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu limemshukuru na kumpongeza Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kutokana na kazi kubwa ambapo wamechangia kiasi cha  shilingi 1,000,000  kwa ajili  ya kuchukua fomu ya kugombea Urais kwa Mhe.Rais na shilingi 577,000 kwa ajili ya Mbunge wa Jimbo la Kasulu Vijijini,Mhe.Vuma Olle  kuchukua fomu ya kugombea ubunge


 Na Fredy Mgunda,Kigoma.

Baraza la Madiwani na Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu limemshukuru na kumpongeza Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kutokana na kazi kubwa  na nzuri aliyoifanya ya kuleta fedha nyingi za utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo katika halmshaur hiyo.

Ambapo wamechangia kiasi cha  shilingi 1,000,000  kwa ajili  ya kuchukua fomu ya kugombea Urais kwa Mhe.Rais na shilingi 577,000 kwa ajili ya Mbunge wa Jimbo la Kasulu Vijijini,Mhe.Vuma Olle  kuchukua fomu ya kugombea ubunge.  

 Akizungumza leo katika kikao cha robo ya tatu cha Baraza Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo,Mhe. Eliya Kgoma,amesema kuwa ni ukweli usiopingika kuwa Rais Samia amefanya kazi kubwa ya maendeleo wilayani humo.

Kwa upande wake ,Mkurugenzi Mtendaji wa halmsahuri hiyo, Dkt.Semistatus H. Mashimba akizungumza kwa niaba ya watendaji wa Halmashauri,amesema kuwa wanaungana na Baraza hilo katika kumpongeza Rais Samia kutokana na fedha nyingi alizoleta kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo ambazo zimewanufaisha wananchi.

Katibu wa CCM Wilaya ya Kasulu,Jennifer Chinguile,amepokea mchango huo kwa niaba ya chama na kuahidi kuuwasilisha kwa Katibu Mkuu wa CCM,Balozi Emmanuel Nchimbi kabla ya mkutano mkuu unaotarajiwa kufanyika badae mwezi huu.

Kwa upande wake,Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Kasulu Vijijini, Simon Nzibuje ametoa shukrani kwa mchango huo na kuhaidi kuufikisha kwa mhusika.

Akitoa salamu za serkali, Mkuu wa Wilaya ya Kasulu,Mhe. Kanali Isaac Mwakisu amewataka wananchi kuwa na taadhari na kuhakikisha wanatunza chakula kutokana na hali isiyoridhisha ya usalama wa chakula kwa sasa.

Wednesday, May 14, 2025

WAHIFADHI TFS SAO HILL WAKAGUA UKARABATI WA MIONDOMBINU YA BARABARATARAFA YA NNE YA SHAMBA MGOLOLO

Wahifadhi tfs sao hill wakagua ukarabati wa miondombinu ya barabaratarafa ya nne ya shamba mgololo akiwa katika eneo la ukaguzi wa barabaraWahifadhi tfs sao hill wakagua ukarabati wa miondombinu ya barabaratarafa ya nne ya shamba mgololo akiwa katika eneo la ukaguzi wa barabara

Na Fredy Mgunda,Mufindi.

Ukaguzi huo umefanyika ikiwa ni hatua ya kuhakikisha kuwa mawasiliano ya barabara zilizopo ndani ya msitu yanaendelea  kuwepo ili kuhakikisha  shughuli za shamba na zile za watumiaji wa barabara hizo ambao ni wavunaji wa miti wanaosafirisha malighafi za miti wanapita katika barabara hizo bila vikwazo vyovyote.


TFS kupitia Shamba la Miti Sao Hill imeendelea kutatua changamoto mbalimbali ambazo zinajitokeza ili kuhakikisha wadau wanaovuna malighafi katika Shamba wanafanya shughuli hiyo kwa wakati na hivyo kupekelekea uvunaji na usafirisha wa malighafi unafanyika bila vikwazo, na kupelekea wadau hao kufanya shughuli zao kwa wakati za kujipatia kipato kwa kuvuna malighafi ya miti na pia serikali kukusanya mapato yake kwa wakati uliopangwa.


Shughuli mbalimbali zinaendele hapa TFS - Shamba la miti Sao Hii katika Tarafa zote nne (4) za shamba ikiwa ni pamoja na maandalizi ya bustani ya miche ya miti kwaajili ya msimu ujao wa upandaji na uvunaji wa malighafi ya miti katika kipindi hiki ambacho mvua katika baadhi ya maeneo zinaendelea kunyesha.


Thursday, May 8, 2025

KAMATI YA SIASA YA CCM MKOA WA LINDI YAIPONGEZA KILWA KWA UTEKELEZAJI WA ILANI

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mkoa, Mheshimiwa Kuruthum Issa Runje akikagua utekelezaji wa ilani ya CCM wilaya ya Kilwa mkoani LindiViongozi wa chama chama mapinduzi mkoa wa Lindi wakiendeea na ukaguzi wa ilani ya CCM kwa kugua miradi mbalimbali katika wilaya ya KilwaViongozi wa chama chama mapinduzi mkoa wa Lindi wakiendeea na ukaguzi wa ilani ya CCM kwa kugua miradi mbalimbali katika wilaya ya Kilwa


Na Fredy Mgunda, Kilwa Lindi 

Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Lindi ikiongozwa na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mkoa, Mheshimiwa Kuruthum Issa Runje, imefanya ziara maalum Wilayani Kilwa kwa ajili ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa chini ya Ilani ya CCM ya mwaka 2020–2025.

Katika ziara hiyo, kamati ilitembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo yenye jumla ya thamani ya Shilingi 44,551,077,124.12. Miradi hiyo inahusisha nyanja mbalimbali muhimu kwa ustawi wa wananchi wa Kilwa, ikiwemo maji, elimu na afya.

Miongoni mwa miradi iliyotembelewa ni pamoja na Mradi wa Maji kwa Miji 28 ambao unagharimu Shilingi 44,007,870,224.12. Mradi huu mkubwa unatarajiwa kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wakazi wa maeneo mbalimbali ndani ya Wilaya ya Kilwa.

Pia kamati ilikagua ujenzi wa nyumba ya mtumishi katika Shule ya Sekondari ya Mavuji (Shilingi 95,000,000), ujenzi wa madarasa mawili katika Shule ya Msingi Naipuli (Shilingi 64,000,000), na ujenzi wa jengo la Vijana Rika katika Kituo cha Afya Tingi (Shilingi 22,006,900). Aidha, walitembelea mradi wa ujenzi wa mabweni mawili, madarasa manne na vyoo katika Shule ya Sekondari Mtanga wenye jumla ya thamani ya Shilingi 362,200,000.

Akizungumza baada ya ziara hiyo, Mhe. Kuruthum Issa aliipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa, Baraza la Madiwani na watendaji wote kwa usimamizi thabiti na utekelezaji bora wa miradi hiyo. Alieleza kuwa utekelezaji huo unaonesha namna ambavyo Ilani ya CCM inatekelezwa kwa vitendo kwa ajili ya kuwaletea wananchi maendeleo ya kweli.

“Tunafurahishwa na kasi na uwajibikaji wa viongozi wetu wa Wilaya ya Kilwa katika kutekeleza Ilani ya Chama. Ushirikiano uliopo baina ya viongozi wa Serikali, CCM na wadau mbalimbali ni mfano wa kuigwa. Tuendelee kuchapa kazi kwa kushirikiana ili kuunga mkono jitihada za Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” alisema Mhe. Kuruthum.

Ziara hiyo ni sehemu ya utaratibu wa kawaida wa chama hicho kuhakikisha kuwa ahadi zake kwa wananchi kupitia Ilani ya Uchaguzi zinatekelezwa kwa ufanisi, uwazi na kwa kuzingatia vipaumbele vya maendeleo kwa wananchi.

Saturday, April 5, 2025

MAONESHO YA MADINI MKOA WA LINDI KUFANYIKA JULAI 11 HADI 14, 2025.

Mkuu wa Mkoa wa Lindi,Zainab Telack ameongoza Kikao cha kwanza cha maandalizi ya Maonesho kilichofanyika Ruangwa huku akitaja Juni 11 hadi 14, 2025 kuwa tarehe ya msimu wa pili wa  monesho ya madini katika mkoa huo ambayo yataambatana na mnada wa madini
Baadhi ya a washiriki wa kikao cha maandalizi ya wiki ya madini Lindi.


Na Fredy Mgunda, Lindi.

 Mkuu wa Mkoa wa Lindi,Zainab Telack ameongoza Kikao cha kwanza cha maandalizi ya Maonesho kilichofanyika Ruangwa huku akitaja Juni 11 hadi 14, 2025 kuwa tarehe ya msimu wa pili wa  monesho ya madini katika mkoa huo ambayo yataambatana na mnada wa madini,Maonesho hayo yatafanyika katika viwanja vya madini Ruangwa Mkoani Lindi.

Telack akiongoza kikao hicho  kilichowakutanisha Viongozi wa Serikali Mkoa wa Lindi, wawakilishi wa makampuni ya uchimbaji na uchenjuaji wa madini, wachimbaji wadogo wadogo, Taasisi mbalimbali za Serikali na kifedha, Bodi ya korosho na vyama vya ushirika, vikiwemo Lindi Mwambao na RUNALI, amesema maonesho ya mwaka huu yatakuwa yatofauti sana hivyo kila mmoja kwanafasi yake anaalikwa kushiriki.

Maonesho ya Madini Mkoa wa Lindi yanatarajiwa kuwa jukwaa muhimu kwa wadau wa sekta hiyo kutangaza fursa za madini, kuimarisha usimamizi wa rasilimali madini, na kuhamasisha uwekezaji endelevu kwa maendeleo ya wananchi wa Mkoa wa Lindi na Taifa kwa ujumla.

Telack ameweka mkazo katika msimu mpya wa pili wa madini wa mwaka huu kufanyika kwa mnada mkubwa wa madini ambao utatoa fursa kwa  wachimbaji na wadau wa madini kuona, kuuza na kununua  vito mbalinbali vya thamani vinavyotoka Mkoani Lindi.

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More