Tuesday, September 30, 2025

VIONGOZI, WANANCHI WATAKIWA KUSHIRIKIANA KUDHIBITI MOTO MISITUNI

Katibu Tawala wa Wilaya ya Mufindi, Reuben Chongolo, ametoa wito kwa viongozi na wananchi kushirikiana kwa dhati katika kudhibiti matukio ya moto misituni, akisisitiza kuwa misitu ndiyo uti wa mgongo wa uchumi na ustawi wa jamii.
Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Miti Sao Hill, PCO Tebby Yoramu, amesema kubwa TFS imekuwa ikitoa elimu kila mwaka kwa vijiji 60 vinavyozunguka shamba hilo juu ya matumizi sahihi ya moto na aliwataka wananchi kutoa taarifa za mapema pale wanapoona viashiria vya moto, ili kuepusha madhara makubwa.
Baadhi ya washiriki kikao hicho cha kuzibiti na kupambana na moto katika shamba la miti Zao Hill na maeneo mengine 
Baadhi ya washiriki kikao hicho cha kuzibiti na kupambana na moto katika shamba la miti Zao Hill na maeneo mengine 


Na Fredy Mgunda,Mufindi Iringa.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Mufindi, Reuben Chongolo, ametoa wito kwa viongozi na wananchi kushirikiana kwa dhati katika kudhibiti matukio ya moto misituni, akisisitiza kuwa misitu ndiyo uti wa mgongo wa uchumi na ustawi wa jamii.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya, Dkt. Linda Salekwa, katika kikao kilichofanyika leo kwenye ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Chongolo alisema moto umekuwa ukileta madhara makubwa kwenye mashamba ya miti ya wananchi na yale yanayosimamiwa na Serikali, ikiwemo Shamba la Miti Sao Hill.

“Nchi yetu hasa maeneo yenye misitu tumekua tukipata changamoto kubwa za moto. Lakini kutokana na mikakati ya TFS, tumekuwa na kamati za vijiji zinazoratibu matumizi ya moto, jambo ambalo limeleta manufaa makubwa,” alisema Chongolo.

Aliongeza kuwa ushirikiano kati ya TFS na wananchi ndio silaha pekee ya kuhakikisha misitu inabaki salama na kuendelea kuchangia mapato ya taifa. Pia aliwataka viongozi wa vijiji na kata kuwapa wananchi elimu endelevu kuhusu matumizi salama ya moto hasa kipindi cha kiangazi.

Kwa upande wake, Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Miti Sao Hill, PCO Tebby Yoramu, alisema TFS imekuwa ikitoa elimu kila mwaka kwa vijiji 60 vinavyozunguka shamba hilo juu ya matumizi sahihi ya moto. Aliwataka wananchi kutoa taarifa za mapema pale wanapoona viashiria vya moto, ili kuepusha madhara makubwa.

Viongozi waliohudhuria kikao hicho waliipongeza TFS kwa jitihada hizo na kuahidi kuendelea kushirikiana katika kutoa elimu na kusimamia uhifadhi wa misitu.

Kikao hicho kilihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Mafinga, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, maafisa tarafa, watendaji wa kata na vijiji pamoja na wenyeviti wa vijiji.

Sunday, September 28, 2025

ELIMU YA USALAMA NA AFYA KAZINI YAWAFIKIA WASIOONA.

Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi.Khadija Mwenda, akihitimisha mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi kwa watu wasioona ambao ni wanachama wa Jumuiya ya Wasioona Tanzania (TAB) wa mikoa ya Dar es Salaam na Pwani. Mafunzo hayo yamefanyika katika Ofisi za OSHA Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu Wa OSHA Bi. Khadija Mwenda akikambidhi Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wasioona, Bw. Omary Itambu vifaa saidizi vikiwemo vitabu vya usalama na afya vyenye maandishi ya nukta nundu, karatasi maalum za nukta nundu pamoja na fimbo nyeupe kwa ajli ya wanachama wake
Mkufunzi wa Huduma ya Kwanza wa OSHA, Bi. Moteswa Meda akiwasilisha mada kuhusu Misingi ya Huduma ya Kwanza mahali pa kazi kwa wanachama wa Jumuiya ya Wasioona Tanzania (TAB) katika semina ya mafunzo iliyoandaliwa na OSHA kwa kundi hilo.
Washiriki wa mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi ambao ni wanachama wa Jumuiya ya Wasioona Tanzania, wakifuatilia mada mbalimbali katika semina iliyoandaliwa na OSHA kwa ajili ya kundi hilo la watu wenye ulemavu.  
Afisa Mafunzo wa OSHA, Bw. Simon Lwaho, akiwasilisha mada kuhusu vihatarishi mahali pa kazi na udhibiti wake kwa wanachama wa Jumuiya ya Wasioona Tanzania (TAB) katika semina ya mafunzo iliyoandaliwa na OSHA kwa kundi hilo.

Na Fredy Mgunda.


Watu wasioona kutoka mikoa ya Dar es Salaam na Pwani wamenufaika na mafunzo yaliyotolewa na Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kwa lengo la kuwawezesha kushiriki shughuli za uzalishaji kwa kuzingatia kanuni bora za usalama na afya kazini.

Mafunzo hayo ya siku moja ambayo yametolewa kwa wanachama 50 wa Jumuiya ya Wasioona Tanzania (TAB) yamehusisha mada mbalimbali zikiwemo utambuzi na udhibiti wa vihatarishi vya usalama na afya pamoja na misingi ya huduma ya kwanza mahali pa kazi. Washiriki wa mafunzo hayo wanajihusisha na shughuli mbalimbali zikiwemo ushonaji, kilimo, ufugaji, uzalishaji wa bidhaa zikiwemo sabuni na biashara ndogondogo.

Akifungua mafunzo hayo, Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, amesema Taasisi anayoiongoza inatambua thamani na mchango wa watu wenye ulemavu katika kujenga uchumi wa Taifa jambo ambalo limepelekea mafunzo hayo kuandaliwa pamoja na mafunzo mengine ambayo OSHA imekuwa ikayatoa kwa makundi mbalimbali ya watu wenye ulemavu.

“Niwapongeze washiriki wote wa mafunzo kwa kuitikia mwaliko wa kushiriki mafunzo haya muhimu kwenu kwani ni dhahiri kuwa ulemavu ni hali tu ambayo haipaswi kuwa kikwazo kwenu kushiriki katika shughuli za kiuchumi,” amesema Mtendaji Mkuu wa OSHA na kuongeza"Alisema Ni Mwenda

Bi Mwenda alisema kuwa watawapatia vifaa saidizi zikiwemo fimbo nyeupe, karatasi za nukta nundu pamoja na vitabu maalum vya nukta nundu vyenye maudhui ya mafunzo ya usalama na afya kwa ajili ya rejea zaidi.

Aidha, Bi. Mwenda ameahidi kuwa mafunzo ya usalama na afya kwa makundi mbalimbali ya watu wenye ulemavu yatafuatiwa na zoezi la kutembelea maeneo yao ya kazi kwa ajili ya kutathmini mazingira ya kazi ili kushauri namna sahihi ya kuboresha mazingira hayo. 

Awali, akiwasilisha salamu za Jumuiya ya Wasiiona Tanzania, Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Bw. Omary Itambu, ameipongeza OSHA kwakuwa mstari wa mbele katika kuwawezesha watu wasioona pamoja na makundi mengine ya watu wenye ulemavu.

“Tunaiomba OSHA kuendeleza utamaduni huu wa kutujali watu wenye ulemavu. Kwa niaba ya washiriki wenzangu niwahakikishie OSHA kuwa mafunzo mliyotupatia si tu yatakwenda kuimarisha afya na usalama wetu bali yatatusaidia sana kuongeza thamani ya huduma na bidhaa tunazozalisha,” amesema Itambu.

Itambu ametoa wito kwa washiriki wenzake wa mafunzo kuwa mabalozi wazuri wa OSHA ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha wenzao ambao hawakupata fursa ya kushiriki mafunzo.

Akitoa neno la shukrani kwa niaba ya washiriki wengine wa mafunzo, Mratibu wa Idara ya Vijana wa Jumuiya ya Wasioona, Bw. Bakari Hassan, amesema jambo lililofanywa na OSHA ni la kuigwa na Taasisi nyingine za kiserikali na zisizo za kiserikali, akisisitiza kwamba mafunzo hayo na vifaa saidizi walivyopewa vitarahisisha utendaji na kuongeza tija katika shughuli zao za kila siku. 

Friday, September 19, 2025

OSHA YAKABIDHI VIFAA CHUO CHA UFUNDI MIRONGO JIJINI MWANZA

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mhe. Amina Makilagi, akiwasilisha hotuba yake wakati wa Bonanza la OSHA la Huduma kwa Jamii (OSHA CSR BONANZA 2025) lililofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Nyakabungo Jijini Mwanza akiwa ni Mgeni Rasmi wa Bonanza hilo. Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mhe. Amina Makilagi na Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda wakimkabidhi Mkuu wa Chuo cha Ufundi cha Mirongo vifaa mbalimbali vya msaada vilivyotolewa na OSHA kukiwezesha chuo hicho. Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na kompyuta, makoti ya usalama na vifaa vya michezo. 

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mhe. Amina Makilagi na Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda wakimkabidhi Mkuu wa Chuo cha Ufundi cha Mirongo vifaa mbalimbali vya msaada vilivyotolewa na OSHA kukiwezesha chuo hicho. Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na kompyuta, makoti ya usalama na vifaa vya michezo.
Mwenyekiti wa timu ya OSHA Iliyoshiriki SHIMIWI mwaka 2025 Ndugu Charles Mhilu akimkabidhi kikombe  Mtendaji Mkuu wa OSHA Bi Khadija Mwenda, mara timu hiyo ya OSHA kuibuka timu Bora yenye nidhamu miongoni mwa timu 50 shindani kwenye mashindano yailyoshirikisha zaidi ya timu 50 toka taasisi,wakala za Serikali na Timu toka RAS mashindano yaliyofanyika hivi karibuni jijini Mwanza.

Na  Fredy Mgunda,Kwanza.


Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mheshimiwa Amina Makilagi, amewataka waajiri na wafanyakazi kote nchini kuitekeleza kikamilifu Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi Na. 5 ya mwaka 2003 ili kupunguza au kuondoa kabisa ajali na magonjwa yanayotokana na mazingira duni ya kazi.


Mheshimiwa Makilagi alitoa wito huo jana wakati wa Bonanza la OSHA la Huduma kwa Jamii (OSHA CSR Bonanza 2025) lililofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Nyakabungo, Wilaya ya Nyamagana, Jijini Mwanza. Bonanza hilo lilihusisha shughuli mbalimbali za kijamii na michezo kwa lengo la kuimarisha mshikamano kati ya OSHA na jamii inayohudumiwa, pamoja na kutoa msaada kwa wanafunzi wa Chuo cha Ufundi Mirongo, wakiwemo wenye ulemavu.


Katika tukio hilo, OSHA ilikabidhi vifaa mbalimbali kwa Chuo cha Ufundi Mirongo, vikiwemo kompyuta, vifaa kinga vya usalama kazini, pamoja na vifaa vya michezo kama mipira na jezi za michezo.


Akizungumza kama Mgeni Rasmi, Mheshimiwa Makilagi aliipongeza OSHA kwa juhudi zake za kuhakikisha mazingira salama na yenye afya sehemu za kazi na kuonesha moyo wa huruma kwa makundi maalum katika jamii.


“Nitoe rai kwa waajiri na wafanyakazi nchini kuisoma na kuitekeleza Sheria Na. 5 ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ya mwaka 2003. Sheria hii ikitekelezwa ipasavyo, maeneo ya kazi yatakuwa salama, bila ajali wala magonjwa, hivyo kuongeza tija kazini,” alisema Mkuu wa Wilaya Makilagi.


Aidha, aliihakikishia OSHA ushirikiano wa Halmashauri na Ofisi yake katika kusimamia usajili na ukaguzi wa maeneo ya kazi, sambamba na kutoa ushauri wa kitaalamu juu ya maboresho ya mazingira ya kazi.


Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, alisema Bonanza hilo ni sehemu ya mpango wa taasisi hiyo wa kurudisha kwa jamii (Corporate Social Responsibility) na kwamba msaada uliotolewa kwa Chuo cha Mirongo umetokana na tathmini iliyofanywa na wataalam wa OSHA baada ya kutembelea chuo hicho.


“Tunaamini kuwa kwa kusaidia vyuo vya ufundi kama Mirongo, tunachangia kwa kiasi kikubwa maandalizi ya wataalamu wa baadaye katika fani muhimu za kiufundi na kazi,” alisema Bi. Mwenda.


Kaimu Mkuu wa Chuo cha Mirongo, Bi. Herieth Richard, pamoja na mwanafunzi wa fani ya ushonaji, Bi. Aneth Augustino, waliishukuru OSHA kwa msaada huo ambao wamesema umeongeza ari ya kujifunza na kushiriki katika shughuli za kijamii.


Bonanza hilo lilihusisha michezo ya mpira wa miguu, mpira wa pete, riadha, na michezo ya jadi kama kukimbia kwenye magunia, kukimbia na ndimu kwenye kijiko, rede na kukamata kuku. Washiriki walitoka OSHA na vyuo vya Ufundi vya Mirongo, Nyakato na Kisesa.


Chuo cha Ufundi Mirongo kinamilikiwa na Serikali chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), na hutoa mafunzo ya umeme, useremala, ushonaji na uchomeleaji kwa vijana wakiwemo wenye mahitaji maalum.

Thursday, September 18, 2025

MWENGE WA UHURU WAWEKA JIWE LA MSINGI WODI YA MAMA NA MTOTO MWAMI NTALE

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, Ismail Ali Ussi, ameweka jiwe la msingi katika wodi ya mama na mtoto katika Kituo cha Afya cha Mwami N’tale, kilichopo kata ya Heru, Halmashauri ya Mji Kasulu.
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, Ismail Ali Ussi, ameweka jiwe la msingi katika wodi ya mama na mtoto katika Kituo cha Afya cha Mwami N’tale, kilichopo kata ya Heru, Halmashauri ya Mji Kasulu.

Na Fredy Mgunda,Kasulu, Kigoma.

 Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, Ismail Ali Ussi, ameweka jiwe la msingi katika wodi ya mama na mtoto katika Kituo cha Afya cha Mwami N’tale, kilichopo kata ya Heru, Halmashauri ya Mji Kasulu.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Ussi amesisitiza umuhimu wa wananchi kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu ujao kwa amani, utulivu, na kuchagua viongozi wanaowataka. Amesema kaulimbiu ya Mwenge wa Uhuru mwaka huu inahimiza amani kama msingi wa maendeleo ya taifa.

“Maendeleo tunayoyaona leo ni matokeo ya utulivu na amani inayotamalaki nchini. Hivyo ni wajibu wetu kuilinda na kuithamini hali hii,” alisema Ussi.

Mradi wa ujenzi wa kituo hicho umegharimu kiasi cha Tsh milioni 300, na tayari umekamilika kwa asilimia 100. Utaanza kutoa huduma za afya kwa kina mama na watoto katika eneo la Heru na maeneo jirani.

Kituo hiki kinatarajiwa kupunguza kwa kiwango kikubwa vifo vya mama na mtoto kwa kutoa huduma bora, za karibu, na za uhakika kwa wananchi.

Mwenge wa Uhuru umeendelea kuwa chombo muhimu katika kuhamasisha maendeleo, uwajibikaji, na uzalendo miongoni mwa Watanzania.

Wednesday, September 17, 2025

MWENGE WA UHURU WAZINDUA KITUO CHA POLISI NYAKITONTO KWA AJILI YA KUONGEZA USALAMA

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ismail Alli Issu, amesema uwepo wa miradi mingi yenye thamani kubwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu ni kielelezo tosha kwamba usalama kwa sasa si hiari tena bali ni sharti la lazima katika kuendeleza maendeleo.
Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Mhe. Kanali Isaac Mwakisu, amesema kwa kuwa halmashauri hiyo ni mpya, suala la maendeleo linaendana moja kwa moja na uwepo wa ulinzi na usalama wa uhakika.
Kituo cha Polisi Nyakitonto chenye hadhi ya Daraja B kimezinduliwa na mbio za Mwenge wa uhuru 
Kituo cha Polisi Nyakitonto chenye hadhi ya Daraja B kimezinduliwa na mbio za Mwenge wa uhuru 


Na Fredy Mgunda,Kasulu Kigoma.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ismail Alli Issu, amesema uwepo wa miradi mingi yenye thamani kubwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu ni kielelezo tosha kwamba usalama kwa sasa si hiari tena bali ni sharti la lazima katika kuendeleza maendeleo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kituo cha Polisi Nyakitonto chenye hadhi ya Daraja B, Issu amesisitiza kuwa mara nyingi panapojengwa vituo vya polisi vya kisasa, basi tambua eneo hilo limepiga hatua kubwa za maendeleo.

“Mkuu wa Wilaya amesema tumejenga kituo hiki kwa sababu uhitaji wake umekuwa mkubwa. Ninyi wenyewe ni mashahidi, miradi yenye thamani kubwa iliyopo hapa Kasulu ndiyo kielelezo cha kasi ya maendeleo,” amesema Issu.

Ameongeza kuwa kutokana na hatua kubwa zilizopigwa, ana uhakika si muda mrefu Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu itapanda hadhi na kuwa Manispaa.Amewataka wananchi kushirikiana katika kulinda amani na usalama ili matarajio hayo yaweze kutimia kwa haraka.

Awali, Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Mhe. Kanali Isaac Mwakisu, amesema kwa kuwa halmashauri hiyo ni mpya, suala la maendeleo linaendana moja kwa moja na uwepo wa ulinzi na usalama wa uhakika.

Kituo hicho cha Polisi Nyakitonto kimejengwa kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri kwa gharama ya shilingi milioni 114 kikiwa ni sehemu ya jitihada za kuhakikisha usalama, amani na utawala wa sheria vinadumu katika wilaya hiyo.

Tuesday, September 16, 2025

TRA NACHINGWEA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAJASIRIAMALI WADOGO

Meneja wa TRA wilaya ya Nachingwea, Novatus Chamu akielezea namna dawati hilo litakavyo kuwa chombo muhimu cha kusikiliza kero, kutoa elimu ya kodi na ushauri wa kukuza mitaji kwa wajasiriamali wadogo.
Meneja wa TRA wilaya ya Nachingwea, Novatus Chamu akiwa kwenye picha pamoja na mgeni rasmi Stella kategile na baadhi ya watumishi wa TRA Nachingwea 
Mgeni rasmi Stella kategile akikataa utepe kuzindua rasmi dawati la TRA kwa ajili ya kusikiliza,kutoa huduma na elimu kwa wajasiriamali wadogo wadogo wa wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi.
Meneja wa TRA wilaya ya Nachingwea, Novatus Chamu akiwa kwenye picha pamoja na mgeni rasmi Stella kategile na baadhi ya wajasiriamali wadogo wadogo wa wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi.


Na Fredy Mgunda, Nachingwea Lindi.

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wilayani Nachingwea imezindua rasmi dawati maalum la kushughulikia changamoto za wajasiriamali wadogo, ikiwa ni hatua ya kuwawezesha kiuchumi na kuwainua kutoka ngazi ya chini ya biashara hadi kuwa wafanyabiashara wakubwa.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Meneja wa TRA wilaya ya Nachingwea, Novatus Chamu, alisema kuwa dawati hilo litakuwa chombo muhimu cha kusikiliza kero, kutoa elimu ya kodi, na ushauri wa kukuza mitaji kwa wajasiriamali wadogo.

“Kupitia dawati hili, tutaweza kusikiliza kero zao moja kwa moja, kuwapa elimu ya kodi na pia kuwashauri namna ya kukuza mitaji yao ili waweze kuchangia pato la taifa kwa ufanisi zaidi,” alisema Chamu.

Aliongeza kuwa hatua hiyo ni sehemu ya juhudi za serikali kusogeza huduma karibu na wananchi, hasa wale waliopo kwenye sekta isiyo rasmi ambao mara nyingi hukumbwa na changamoto ya uelewa mdogo kuhusu masuala ya kodi na taratibu za biashara.

Kwa upande wake, mgeni rasmi katika uzinduzi huo, Stella Kategile, alieleza kuwa dawati hilo ni jukwaa muhimu la kukuza uchumi wa wafanyabiashara wadogo. Alisisitiza kuwa serikali inalenga kuwawezesha wajasiriamali kupitia utatuzi wa changamoto zao badala ya kuwabana kwa kodi bila kuelewa hali zao halisi.

“Lengo la serikali siyo kukusanya kodi tu, bali pia kusikiliza na kutatua changamoto za wajasiriamali ili waweze kukua na kuchangia kikamilifu katika pato la taifa,” alisema Kategile.

Baadhi ya wajasiriamali waliopata fursa ya kuzungumza walipongeza hatua hiyo ya TRA, wakisema kuwa imekuja kwa wakati muafaka kwani changamoto nyingi zimekuwa zikiwakwamisha katika kuendeleza biashara zao.

“Kwa muda mrefu tumekuwa hatuna pa kupaza sauti zetu. Kupitia dawati hili, tuna matumaini kuwa sauti zetu zitasikika na biashara zetu zitakua,” alisema mmoja wa wajasiriamali hao.

Dawati hilo linatarajiwa kuwa kiunganishi muhimu kati ya TRA na wajasiriamali, na mchango wake unatarajiwa kuleta mabadiliko chanya katika muktadha wa ukusanyaji wa mapato na ukuaji wa sekta ya biashara nchini.


Thursday, September 11, 2025

BALOZI SIRRO;AWATAKA WANANCHI KULINDA AMANI ILIYOPO KIPINDI HIKI CHA UCHAGUZI.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Mhe. Balozi Simon Sirro amesema kuwa jiografia ya Kigoma inayopakana na Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, inaifanya mkoa huo kuwa na nafasi nyeti katika kudumisha amani. Akisisitiza kuwa amani si hiari bali ni sharti la msingi kwa ustawi wa wananchi.
Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Mhe. Balozi Simon Sirro amesema kuwa jiografia ya Kigoma inayopakana na Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, inaifanya mkoa huo kuwa na nafasi nyeti katika kudumisha amani. Akisisitiza kuwa amani si hiari bali ni sharti la msingi kwa ustawi wa wananchi.
Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Mhe. Balozi Simon Sirro amesema kuwa jiografia ya Kigoma inayopakana na Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, inaifanya mkoa huo kuwa na nafasi nyeti katika kudumisha amani. Akisisitiza kuwa amani si hiari bali ni sharti la msingi kwa ustawi wa wananchi.

Na Fredy Mgunda,Kigoma.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Mhe. Balozi Simon Sirro amesema kuwa jiografia ya Kigoma inayopakana na Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, inaifanya mkoa huo kuwa na nafasi nyeti katika kudumisha amani. Akisisitiza kuwa amani si hiari bali ni sharti la msingi kwa ustawi wa wananchi.


Balozi Sirro ametoa kauli hiyo, wakati wa Kongamano la kuliombea taifa Amani katika Uchaguzi Mkuu 2025 lililofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu Kasulu (TCC), lililoandaliwa na Kamati ya Maridhiano kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kasulu.


“Bila amani, biashara ya mipakani haiwezi kustawi, wananchi hawawezi kuendeleza shughuli zao za kilimo, uvuvi na biashara ndogo ndogo. Amani ndiyo uti wa mgongo wa maendeleo ya Kigoma na Tanzania kwa ujumla,” amesema.

Ameongeza kuwa viongozi wa dini wanapaswa kuepuka kutumia nyumba za ibada kama majukwaa ya kisiasa, kwani kuchanganya masuala ya dini na siasa kunaweza kuhatarisha mshikamano wa kijamii.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Mhe. Kanali Isaac Mwakisu, amewashukuru viongozi wa dini kwa kushirikiana na serikali katika matukio mbalimbali na kuwataka waendelee kuwaombea viongozi ili watoe maamuzi yenye busara kwa wananchi.

Naye Katibu wa Kamati ya Maridhiano Wilaya ya Kasulu Sheikh Nasib Rajab kutoka dhehebu la SHIA, amesema kongamano hilo limeonesha mshikamano wa wananchi licha ya tofauti za kiitikadi, jambo linalosaidia kuimarisha umoja na mshikamanano.

Vilevile, Askofu wa Kanisa la FPCT Jimbo la Kasulu, Shadrack Bunono, alibainisha kuwa mtu anayekalia kiti cha mamlaka anapaswa kutumia busara na hekima katika maamuzi yake kwa manufaa ya wananchi, na kusisitiza kuwa sala na maombi kwa viongozi ni msingi wa mafanikio katika wilaya hiyo.

Saturday, September 6, 2025

KASULU YAANDAA BONANZA LA MICHEZO KUHAMASISHA UCHAGUZI NA MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU

Mkuu wa Wilaya ya Kasulu,mkoani Kigoma, Mhe. Kanali Isaac Mwakisu, amesema wananchi wanapaswa kujitokeza kwa wingi kushiriki mapokezi ya Mwenge wa Uhuru pamoja na Uchaguzi Mkuu ujao, kwani matukio hayo ni ya kitaifa na yanabeba taswira ya mshikamano wa Watanzania.

Baadhi ya viongozi na wananchi waliojitokeza kwenye bonanza hilo
Mkuu wa Wilaya ya Kasulu,mkoani Kigoma, Mhe. Kanali Isaac Mwakisu na katibu tawala Theresia Mtewele wakishiriki katika bonanza kwa ajili ya mapokezi ya Mwenge wa Uhuru pamoja pamoja na kuhamasishwa wananchi kushiriki Uchaguzi Mkuu ujao, 


Na Fredy Mgunda, Kigoma.

Mkuu wa Wilaya ya Kasulu,mkoani Kigoma, Mhe. Kanali Isaac Mwakisu, amesema wananchi wanapaswa kujitokeza kwa wingi kushiriki mapokezi ya Mwenge wa Uhuru pamoja na Uchaguzi Mkuu ujao, kwani matukio hayo ni ya kitaifa na yanabeba taswira ya mshikamano wa Watanzania.


Akizungumza leo Jumamosi, Septemba 6, 2025, katika bonanza la michezo mbalimbali lililofanyika Viwanja vya Shule ya Msingi Kiganamo, Kanali Mwakisu amesema Mwenge wa Uhuru utakimbizwa wilayani humo Septemba 17 na 18, ambapo siku ya kwanza utapokelewa Kasulu Vijijini eneo la Mvugwe na siku inayofuata itakuwa Kasulu Mjini.


“Maudhui makuu ya bonanza hili ni kuwakumbusha wananchi kuwa Mwenge utakimbizwa katika wilaya yetu, na tunapaswa kushiriki kwa wingi ili kuonesha mshikamano na kuthamini amani na utulivu wa nchi yetu,” amesema.


Amesema kuwa Mwenge wa Uhuru ni tunu kubwa ya taifa, na wananchi wanapojitokeza kuupokea kwa shangwe ni kielelezo cha kuthamini amani na utulivu kwa mustakabali wa maendeleo ya nchi.


Aidha, amewakumbusha kuwa kwa mujibu wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Uchaguzi Mkuu utafanyika Oktoba 29, 2025, hivyo wananchi wanatakiwa kujitokeza kwa wingi baada ya kusikiliza sera za wagombea na kuwachagua viongozi wanaowataka.


Mmoja wa wananchi, Nelstella Kihoza, akizungumza na mwandishi wetu amesema kuwa umati mkubwa uliofurika viwanjani hapo ni ishara tosha ya mwamko wa wananchi wa Kasulu, na kwamba watajitokeza kwa wingi kushiriki Uchaguzi Mkuu kwa kuchagua viongozi wanaowataka, sambamba na kushiriki kikamilifu katika Mbio za Mwenge wa Uhuru.


Naye Mwalimu Yusufu Hamisi amrmpongeza Mkuu wa Wilaya kwa ubunifu wa kuandaa bonanza hilo, akisema limempa ari ya kuendelea kuhamasisha wananchi wengine kushiriki kikamilifu matukio hayo mawili muhimu ya kitaifa.

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More