
Na Mathias Canal, Iringa
vijijini Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kupitia Umoja wa
katiba ya Wananchi {UKAWA} kimezindua kampeni zake katika Jimbo la Kalenga
lililopo mkoani Iringa kwa muktadha wa kuanza vyema mikikimikiki ya kumnadi
mgombea wake ambaye mara kadhaa amesikika akisema jimbo hilo limekosa
muwakilishi wa wananchi bungeni.
Chadema/ukawa inataraji kuanza kampeni zake za kumnadi mgombea wa Urais,
wagombea ubunge, na udiwani mara baada ya uzinduzi wa kampeni zinazotaraji
kufanyika mwishoni mwa wiki hii.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hizo
zilizofanyika katika eneo la Ifunda, mgombea ubunge kwa tiketi ya
Chadema/Ukawa, Mdede Mussa Leonard amesema kuwa...