Friday, July 3, 2015

CHUO KIKUU CHA IRINGA ZAMANI TUMAINI KESHO KINATARAJIA KUADHIMISHA SIKU YA UTALII NA UTAMADUNI MAADHIMISHO YATAFANYIKA KATIKA CHUO HICHO.

 
 MHADHILI WA CHUO KIKUU CHA IRINGA JIMSON SANGA 
 
 baadhi ya majengo ya chuo kikuu cha iringa zamani tumaini
 
  baadhi ya majengo ya chuo kikuu cha iringa zamani tumaini

na fredy mgunda,iringa



Chuo kikuu cha IRINGA ZAMANI TUMAINI kesho kinatarajiwa kuadhimisha siku ya utalii wa kitamaduni  katika chuo hicho.


Akizungumza na blog hii mkuu wa kitengo cha utalii cha chuo  hicho MHADHILI WA CHUO KIKUU CHA IRINGA JIMSON SANGA amesema kuwa wameamua kuadhimisha siku hiyo ili kuwakumbusha wananchi juu ya kuuezi utamaduni wao na kuacha kuiga tamaduni za kigeni.


Aidha SANGA amesema kuwa chuo hicho kimekuwa kikifundisha elimu ya utalii ndani ya chuo tu sasa imefika wakati wa kutoka na kuifikia moja kwa moja  jamii ambayo haina elimu hiyo.


“Tunaona wakina mama ntilie wanauza vyakula ya kitamaduni lakini hawana wateja kwa sababu wanashindwa kutoa huduma ya kuridhisha kwa wateja hata hivyo mama ntilie wengine hutoa huduma kwa kutofata mazingira ya kiafya”.alisema SANGA


Ameongeza kuwa watanzania  wengi hatuna tabia ya kuupenda utamaduni wetu au kuipenda asili yetu tunaona wananchi wengi wanapenda kuiga utamaduni wa kigeni hivyo tunatakiwa kuuenzi utamaduni wetu.


SANGA amemalizia kwa kuwataka wanachi wajitokeze siku ya jumamosi ili kujionea vitu mbalimbali ya kitamaduni.


Kwa upande wao WANAFUNZI WA CHUO HICHO hasa wanaosomea masomo ya maliasili na utalii wamewataka wananchi wa mkoa wa iringa kujitokeza kwa wingi katika maonyesho hao.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More