Wednesday, November 25, 2015

WANAUME WA MAFINGA NDIO CHANZO CHA VIFO VYA AKIMAMA VINAVYOTOKANA NA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI

BAADHI ya wanaume nchini, wametajwa kuwa chanzo cha ongezeko la vifo vya wanawake, vitokanavyo na saratani ya shingo ya kizazi, kwa madai ya kuwazuia wenza wao kwenda kupima ugonjwa huo ambao umeonekana kupoteza uhai wa akinamama walio wengi.

Hayo yamezungumzwa na akinamama waliohudhuria huduma ya uchunguzi wa Saratani ya shingo ya Kizazi, mpango ulifadhiliwa na kampuni ya Green Resources – inayojihusisha na shughuli za upandaji wa miti katika Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa.

Flaviana Myovela na Mayasa Hassan ni baadhi ya akinamama waliohudhuria huduma hiyo, wamesema mwamko duni miongoni mwa wanawake wenzao, unatokana na baadhi ya wanaume kuwazuia wake zao kushiriki huduma ya uchunguzi wa saratani hiyo, wakidhani mpango huo umelenga kuwafunga vizazi wake zao.

Hongera Kiyungu  na Olester Mkweve wamesema ili kukabiliana na fikra hizo potofu,  serikali inalojukulu la kuwapatia  elimu wanaume, juu ya madhara yatokanayo na ugonjwa wa saratani ya shingo ya kizazi, ili waachane na fikra potofu ambazo kwa namna moja au nyingine zinachangia ongezeko la vifo vya wanawake.

Hata hivyo Rose Marick - mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Green Resource Tanzania, amesema sababu ya kusogeza huduma hiyo ni kuwapunguzia umbali wa kuifuata huduma hiyo, huku akitoa ushauri kwa akinababa wenye imani potofu juu ya huduma hiyo, kwa madai kuwa kulifumbia macho tatizo hilo ni kuchangia ongezeko la vifo kwa wanawake.

Zoezi hili la uchunguzi wa saratani ya shingo ya kizazi kwa wafanyakazi wa kampuni ya Green Resources  wilayani Mufindi na jamii inayoizunguka kampuni – limewalenga kuwafanyia uchunguzi  wanawake zaidi ya 2000 – ugonjwa ambao kwa mujibu wa takwimu za madaktari – wanawake 11 Tanzania kila siku  hufariki kwa ugonjwa huo.

Mpango huo wa kusogeza zoezi la upimaji wa Saratani ya shingo ya Kizazi  kwa wanawake utawanufaisha kundi hilo la wafanyakazi na wananchi wa eneo hilo la Twico, kwakuwa baadhi yao hushindwa kuifuata huduma hiyo katika Hospitali ya Mafinga ambayo ipo umbali wa km 15 kutoka katika eneo la Kiwanda.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More