Friday, October 24, 2025
OSHA YADHAMIRIA KUONGEZA UELEWA WA WADAU KUPITIA VYAMA VYA WAFANYAKAZI
Tuesday, October 7, 2025
SERIKALI YAENDELEA KUWAUNGA MKONO WAKULIMA WA PAMBA KASULU
Mkuu wa wilaya ya Kasulu Kanali Isaac Mwakisu Serikali inaendelea kuleta unafuu kwa wakulima wa zao la pamba wilayani Kasulu kwa kuwapatia pembejeo muhimu kama mbegu, viuatilifu na vinyunyizi, hatua iliyochochea kilimo chenye tija na matokeo chanya.
Serikali imeendelea kuleta unafuu kwa wakulima wa zao la pamba wilayani Kasulu kwa kuwapatia pembejeo muhimu kama mbegu, viuatilifu na vinyunyizi, hatua iliyochochea kilimo chenye tija na matokeo chanya.
Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Mhe. Kanali Isaac Mwakisu, amesema hayo leo Jumanne, Oktoba 7, 2025, katika Kata ya Asante Nyerere, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Pamba Duniani yaliyokwenda sambamba na uzinduzi wa msimu mpya wa zao hilo kwa mwaka 2025/2026.
Amesema maadhimisho hayo ni fursa muhimu kwa Serikali, wanunuzi na vyama vya msingi kujadili maendeleo ya zao hilo na kuweka mikakati ya kuliboresha zaidi.
Aidha, amewataka wananchi kutumia kipindi hiki cha kampeni kusikiliza sera za wagombea wa vyama mbalimbali ili siku ya uchaguzi, Oktoba 29, watumie haki yao ya kikatiba kuchagua viongozi wanaowataka.
Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Theresia Mtewele, amesema maadhimisho ya Siku ya Pamba Duniani yaliyoanzishwa mwaka 2019 yanalenga kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa zao hilo kama chanzo kikuu cha kipato kwa wakulima wadogo na wafugaji vijijini.
Mkulima wa Pamba, Joel Kingi, ameishukuru Serikali kwa juhudi zake za kuhamasisha kilimo hicho, akieleza kuwa idadi ya wakulima imeongezeka kutoka 50 hadi kufikia 1,000 kutokana na upatikanaji wa pembejeo na viuatilifu.
Awali, Mkaguzi wa Pamba wa Wilaya hiyo, Michael Kiliga, amesema wilaya inashirikiana na vyama vya ushirika (AMCOS) nane kusambaza pembejeo kwa wakulima bure, hatua inayochangia kuimarisha uzalishaji wa zao hilo.
CCM WAFANYA BONANZA KUHAMASISHA WANANCHI KUSHIRIKI UCHAGUZI KWA AMANI
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimeandaa Bonanza Maalum katika Jimbo la Segerea, mkoani Dar es Salaam, kwa lengo la kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, kwa njia ya amani na utulivu.
Mgeni rasmi katika bonanza hilo alikuwa Mwenyekiti wa UWT Taifa, Mary Pius Chatanda, ambaye aliwataka wananchi kutumia haki yao ya kidemokrasia kwa kupiga kura kwa amani, akisisitiza kuwa kiongozi anayechaguliwa leo ndiye atakayekuwa na mamlaka ya kuleta maendeleo kwa miaka mitano ijayo.
“Kupiga kura ni haki ya msingi kwa kila Mtanzania. Tuchague viongozi wanaotuletea maendeleo ya kweli,” alisema Chatanda.
Akimnadi mgombea urais wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Chatanda alisema kuwa serikali ya awamu ya sita imeitekeleza ilani ya CCM ya mwaka 2020-2025 kwa asilimia 100, na hivyo anastahili kupewa tena ridhaa ya kuendelea kuongoza nchi.
Aidha, alitoa wito kwa wananchi kumchagua mgombea wa CCM katika nafasi ya urais, ubunge na udiwani ili kuimarisha juhudi za maendeleo nchini.
Kwa upande wake, mgombea ubunge wa Jimbo la Segerea, Bonnah Kamoli, alisisitiza kuwa mojawapo ya sera zake ni kuhamasisha mazoezi ya mara kwa mara kwa wananchi, ili kuboresha afya ya mwili na akili.
“Afya bora ni msingi wa maendeleo. Tukifanya mazoezi tutakuwa na nguvu za kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa taifa,” alisema Kamoli.
Kamoli aliwaomba wakazi wa Segerea kumpigia kura nyingi pamoja na kumpa kura ya kishindo Dkt. Samia Suluhu Hassan, ili kuendeleza kasi ya maendeleo katika jimbo hilo.
Naye Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (MNEC) na Mratibu wa Kampeni za CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Kasesela, aliwataka wananchi kupuuza wanasiasa na wanaharakati wanaotumia mitandao ya kijamii kuchochea vurugu na hofu wakati huu wa uchaguzi.
“Wachochezi wengi wapo nje ya nchi. Vurugu zikitokea, ni Watanzania waliopo hapa ambao watateseka. Amani ni tunu ya taifa letu,tuilinde,” aliongeza Kasesela.
Katika bonanza hilo, wananchi walishiriki katika michezo mbalimbali, burudani, na kupata elimu juu ya umuhimu wa kushiriki uchaguzi kwa njia ya amani.
Sunday, October 5, 2025
MNEC KASESELA AWASIHI WATANZANIA KUSOMA VITABU VYA DINI
Baadhi ya waumini wa dini ya wananchi waliohudhuria kongamano la waislamu kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29 mwaka huu lilofanyika mlimani city jijini Dar es salaam
Baadhi ya waumini wa dini ya wananchi waliohudhuria kongamano la waislamu kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29 mwaka huu lilofanyika mlimani city jijini Dar es salaamNa Fredy Mgunda
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (MNEC) na Mratibu wa Kampeni wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kanda ya Dar es Salaam, Richard Kasesela, amewataka Watanzania kumuabudu Mwenyezi Mungu kila wakati ili waweze kupata amani ya moyo na nafsi.
Akizungumza katika kongamano la Waislamu kuelekea uchaguzi mkuu, Kasesela alisema ni muhimu kwa wananchi kusoma vitabu vya dini mara kwa mara, kwani vinafundisha maadili mema na kuleta baraka katika kazi zao za kila siku.
"Vitabu vya dini vinatufundisha subira, heshima na upendo – misingi ambayo ni muhimu katika maisha na maendeleo ya taifa," alisema Kasesela.
Aidha, aliwaomba viongozi wa dini kuendelea kutoa elimu ya kiroho sambamba na mafunzo ya mbinu za kujikwamua kiuchumi, ili wananchi waweze kujitegemea na kuboresha maisha yao.
Katika hatua nyingine, Kasesela aliwahimiza wananchi wote kumpigia kura kwa wingi Mgombea Urais wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akieleza kuwa amefanya kazi kubwa ya kuleta maendeleo katika kipindi chake cha uongozi.
"Ni wajibu wetu kuonyesha shukrani kwa kumpigia kura Dkt. Samia tarehe 29 Oktoba. Tuonyeshe mshikamano wetu kwa kupitia sanduku la kura," alihitimisha Kasesela.






Friday, October 24, 2025
mwangaza wa hbari











