Monday, May 19, 2025

MADAKTARI BINGWA 47 WATIA NANGA MKOANI LINDI KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA

Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Bi. Zuwena Omary akizunguza wakati  kuwapokea rasmi madaktari bingwa 47 chini ya mpango wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, awamu ya tatu, kwa ajili ya kutoa huduma za kibingwa katika hospitali zote za wilaya ndani ya mkoa huo.
Baadhi ya Madaktari bingwa ambao wamewasili mkoani Lindi kwa ajili ya kutoa huduma za kibingwa kwa wananchi wote mkoani.

Na Fredy Mgunda, Lindi.

Serikali ya Mkoa wa Lindi imewapokea rasmi madaktari bingwa 47 chini ya mpango wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, awamu ya tatu, kwa ajili ya kutoa huduma za kibingwa katika hospitali zote za wilaya ndani ya mkoa huo.


Akizungumza wakati wa mapokezi hayo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Bi. Zuwena Omary, alisema kuwa ujio wa madaktari hao ni sehemu ya jitihada za serikali kusogeza huduma za afya karibu na wananchi, hasa wale walioko maeneo ya vijijini ambako awali walilazimika kusafiri mbali kupata huduma za kibingwa.


“Huduma hizi zitapatikana katika maeneo saba ndani ya mkoa kwa siku sita mfululizo kuanzia leo. Lengo ni kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma bora na kwa wakati,” alisema Bi. Omary.


Aliongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imekuwa mstari wa mbele kuboresha sekta ya afya kwa kujenga miundombinu ya kisasa, kununua vifaa tiba vya kisasa, pamoja na kuongeza wataalamu mbalimbali wa afya nchini.


Kwa upande wake, Mratibu wa timu hiyo ya madaktari, Michael Mbele, alieleza kuwa madaktari hao wamejipanga kikamilifu kutoa huduma zote muhimu za afya kwa wananchi wote, bila ubaguzi, katika hospitali za wilaya walizopangiwa.


“Tumewakilishwa na wataalamu wa kada zote za afya, kuanzia magonjwa ya ndani, watoto, wanawake, upasuaji na hata huduma za kisaikolojia. Huduma zote hizi sasa zitapatikana katika hospitali za wilaya,” alisema Mbele.


Wananchi wa Mkoa wa Lindi waliopata fursa ya kuhudumiwa walieleza furaha na shukrani kwa serikali, hususan kwa Mheshimiwa Rais, kwa kuendelea kuboresha huduma za afya nchini, hatua ambayo wameitaja kama ya kipekee na ya kupongezwa.

Thursday, May 15, 2025

BARAZA LA MADIWANI KASULU LIMEMCHANGIA MILIONI 1 RAIS DKT SAMIA KWA AJILI YA KUCHUKUA FOMU YA KUGOMBEA TENA URAIS.

Baraza la Madiwani na Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu limemshukuru na kumpongeza Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kutokana na kazi kubwa ambapo wamechangia kiasi cha  shilingi 1,000,000  kwa ajili  ya kuchukua fomu ya kugombea Urais kwa Mhe.Rais na shilingi 577,000 kwa ajili ya Mbunge wa Jimbo la Kasulu Vijijini,Mhe.Vuma Olle  kuchukua fomu ya kugombea ubunge
Baraza la Madiwani na Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu limemshukuru na kumpongeza Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kutokana na kazi kubwa ambapo wamechangia kiasi cha  shilingi 1,000,000  kwa ajili  ya kuchukua fomu ya kugombea Urais kwa Mhe.Rais na shilingi 577,000 kwa ajili ya Mbunge wa Jimbo la Kasulu Vijijini,Mhe.Vuma Olle  kuchukua fomu ya kugombea ubunge
Baraza la Madiwani na Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu limemshukuru na kumpongeza Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kutokana na kazi kubwa ambapo wamechangia kiasi cha  shilingi 1,000,000  kwa ajili  ya kuchukua fomu ya kugombea Urais kwa Mhe.Rais na shilingi 577,000 kwa ajili ya Mbunge wa Jimbo la Kasulu Vijijini,Mhe.Vuma Olle  kuchukua fomu ya kugombea ubunge



Baraza la Madiwani na Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu limemshukuru na kumpongeza Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kutokana na kazi kubwa ambapo wamechangia kiasi cha  shilingi 1,000,000  kwa ajili  ya kuchukua fomu ya kugombea Urais kwa Mhe.Rais na shilingi 577,000 kwa ajili ya Mbunge wa Jimbo la Kasulu Vijijini,Mhe.Vuma Olle  kuchukua fomu ya kugombea ubunge


 Na Fredy Mgunda,Kigoma.

Baraza la Madiwani na Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu limemshukuru na kumpongeza Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kutokana na kazi kubwa  na nzuri aliyoifanya ya kuleta fedha nyingi za utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo katika halmshaur hiyo.

Ambapo wamechangia kiasi cha  shilingi 1,000,000  kwa ajili  ya kuchukua fomu ya kugombea Urais kwa Mhe.Rais na shilingi 577,000 kwa ajili ya Mbunge wa Jimbo la Kasulu Vijijini,Mhe.Vuma Olle  kuchukua fomu ya kugombea ubunge.  

 Akizungumza leo katika kikao cha robo ya tatu cha Baraza Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo,Mhe. Eliya Kgoma,amesema kuwa ni ukweli usiopingika kuwa Rais Samia amefanya kazi kubwa ya maendeleo wilayani humo.

Kwa upande wake ,Mkurugenzi Mtendaji wa halmsahuri hiyo, Dkt.Semistatus H. Mashimba akizungumza kwa niaba ya watendaji wa Halmashauri,amesema kuwa wanaungana na Baraza hilo katika kumpongeza Rais Samia kutokana na fedha nyingi alizoleta kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo ambazo zimewanufaisha wananchi.

Katibu wa CCM Wilaya ya Kasulu,Jennifer Chinguile,amepokea mchango huo kwa niaba ya chama na kuahidi kuuwasilisha kwa Katibu Mkuu wa CCM,Balozi Emmanuel Nchimbi kabla ya mkutano mkuu unaotarajiwa kufanyika badae mwezi huu.

Kwa upande wake,Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Kasulu Vijijini, Simon Nzibuje ametoa shukrani kwa mchango huo na kuhaidi kuufikisha kwa mhusika.

Akitoa salamu za serkali, Mkuu wa Wilaya ya Kasulu,Mhe. Kanali Isaac Mwakisu amewataka wananchi kuwa na taadhari na kuhakikisha wanatunza chakula kutokana na hali isiyoridhisha ya usalama wa chakula kwa sasa.

Wednesday, May 14, 2025

WAHIFADHI TFS SAO HILL WAKAGUA UKARABATI WA MIONDOMBINU YA BARABARATARAFA YA NNE YA SHAMBA MGOLOLO

Wahifadhi tfs sao hill wakagua ukarabati wa miondombinu ya barabaratarafa ya nne ya shamba mgololo akiwa katika eneo la ukaguzi wa barabaraWahifadhi tfs sao hill wakagua ukarabati wa miondombinu ya barabaratarafa ya nne ya shamba mgololo akiwa katika eneo la ukaguzi wa barabara

Na Fredy Mgunda,Mufindi.

Ukaguzi huo umefanyika ikiwa ni hatua ya kuhakikisha kuwa mawasiliano ya barabara zilizopo ndani ya msitu yanaendelea  kuwepo ili kuhakikisha  shughuli za shamba na zile za watumiaji wa barabara hizo ambao ni wavunaji wa miti wanaosafirisha malighafi za miti wanapita katika barabara hizo bila vikwazo vyovyote.


TFS kupitia Shamba la Miti Sao Hill imeendelea kutatua changamoto mbalimbali ambazo zinajitokeza ili kuhakikisha wadau wanaovuna malighafi katika Shamba wanafanya shughuli hiyo kwa wakati na hivyo kupekelekea uvunaji na usafirisha wa malighafi unafanyika bila vikwazo, na kupelekea wadau hao kufanya shughuli zao kwa wakati za kujipatia kipato kwa kuvuna malighafi ya miti na pia serikali kukusanya mapato yake kwa wakati uliopangwa.


Shughuli mbalimbali zinaendele hapa TFS - Shamba la miti Sao Hii katika Tarafa zote nne (4) za shamba ikiwa ni pamoja na maandalizi ya bustani ya miche ya miti kwaajili ya msimu ujao wa upandaji na uvunaji wa malighafi ya miti katika kipindi hiki ambacho mvua katika baadhi ya maeneo zinaendelea kunyesha.


Thursday, May 8, 2025

KAMATI YA SIASA YA CCM MKOA WA LINDI YAIPONGEZA KILWA KWA UTEKELEZAJI WA ILANI

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mkoa, Mheshimiwa Kuruthum Issa Runje akikagua utekelezaji wa ilani ya CCM wilaya ya Kilwa mkoani LindiViongozi wa chama chama mapinduzi mkoa wa Lindi wakiendeea na ukaguzi wa ilani ya CCM kwa kugua miradi mbalimbali katika wilaya ya KilwaViongozi wa chama chama mapinduzi mkoa wa Lindi wakiendeea na ukaguzi wa ilani ya CCM kwa kugua miradi mbalimbali katika wilaya ya Kilwa


Na Fredy Mgunda, Kilwa Lindi 

Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Lindi ikiongozwa na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mkoa, Mheshimiwa Kuruthum Issa Runje, imefanya ziara maalum Wilayani Kilwa kwa ajili ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa chini ya Ilani ya CCM ya mwaka 2020–2025.

Katika ziara hiyo, kamati ilitembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo yenye jumla ya thamani ya Shilingi 44,551,077,124.12. Miradi hiyo inahusisha nyanja mbalimbali muhimu kwa ustawi wa wananchi wa Kilwa, ikiwemo maji, elimu na afya.

Miongoni mwa miradi iliyotembelewa ni pamoja na Mradi wa Maji kwa Miji 28 ambao unagharimu Shilingi 44,007,870,224.12. Mradi huu mkubwa unatarajiwa kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wakazi wa maeneo mbalimbali ndani ya Wilaya ya Kilwa.

Pia kamati ilikagua ujenzi wa nyumba ya mtumishi katika Shule ya Sekondari ya Mavuji (Shilingi 95,000,000), ujenzi wa madarasa mawili katika Shule ya Msingi Naipuli (Shilingi 64,000,000), na ujenzi wa jengo la Vijana Rika katika Kituo cha Afya Tingi (Shilingi 22,006,900). Aidha, walitembelea mradi wa ujenzi wa mabweni mawili, madarasa manne na vyoo katika Shule ya Sekondari Mtanga wenye jumla ya thamani ya Shilingi 362,200,000.

Akizungumza baada ya ziara hiyo, Mhe. Kuruthum Issa aliipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa, Baraza la Madiwani na watendaji wote kwa usimamizi thabiti na utekelezaji bora wa miradi hiyo. Alieleza kuwa utekelezaji huo unaonesha namna ambavyo Ilani ya CCM inatekelezwa kwa vitendo kwa ajili ya kuwaletea wananchi maendeleo ya kweli.

“Tunafurahishwa na kasi na uwajibikaji wa viongozi wetu wa Wilaya ya Kilwa katika kutekeleza Ilani ya Chama. Ushirikiano uliopo baina ya viongozi wa Serikali, CCM na wadau mbalimbali ni mfano wa kuigwa. Tuendelee kuchapa kazi kwa kushirikiana ili kuunga mkono jitihada za Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” alisema Mhe. Kuruthum.

Ziara hiyo ni sehemu ya utaratibu wa kawaida wa chama hicho kuhakikisha kuwa ahadi zake kwa wananchi kupitia Ilani ya Uchaguzi zinatekelezwa kwa ufanisi, uwazi na kwa kuzingatia vipaumbele vya maendeleo kwa wananchi.

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More