
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo amepongezwa
na walimu pamoja na wanafunzi wa shule ya sekondari Matosa iliyopo Kata
ya Goba , Manispaa ya Ubungo kwa kufanikisha kwa kiasi kikubwa
utekelezaji wa mradi wa SEDP II.
Mradi huo unaohusisha ujenzi wa vyumba viwili vya darasa, nyumba za
walimu, kisima cha maji, tanki la kuhifadhia maji pamoja na vyoo upo
katika hatua nzuri ya kukamailika kutokana na juhudi pamoja na utendaji
kazi uliotukuka wa Mkurugenzi Kayombo akishirikiana na watumishi wa
Manispaa hiyo.
Akizungumza na mtandao wetu mwalimu Mkuu wa shule
hiyo alisema amefurahishwa na juhudi zinazofanywa na Mkurugenzi wa
Manispaa hiyo za kuleta...