Wednesday, November 30, 2016

MD KAYOMBO AFANIKISHA MRADI SHULE YA MATOSA

 Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo amepongezwa na walimu pamoja na wanafunzi wa shule ya sekondari Matosa iliyopo Kata ya Goba , Manispaa ya Ubungo kwa kufanikisha kwa kiasi kikubwa utekelezaji wa mradi wa SEDP II. Mradi huo unaohusisha ujenzi wa vyumba viwili vya darasa, nyumba za walimu, kisima cha maji, tanki la kuhifadhia maji pamoja na vyoo upo katika hatua nzuri ya kukamailika kutokana na juhudi pamoja na utendaji kazi uliotukuka wa Mkurugenzi Kayombo akishirikiana na watumishi wa Manispaa hiyo. Akizungumza na mtandao wetu mwalimu Mkuu wa shule hiyo alisema amefurahishwa na juhudi zinazofanywa na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo za kuleta...

ESRF YAFANIKISHA MKUTANO WA 5 WA MWAKA, WAJADILI UCHUMI

Imeleezwa kuwa ili kumwezesha kila mwananchi wa Tanzania kupata maendeleo na kuondokana na janga la umaskini, Serikali haina budi kutunga sera ambazo zitamgusa kila mwananchi na kuwa na faida jambo ambalo litawasadia kukuza uchumi wao binafasi na taifa kwa ujumla. Hayo yamesemwa katika mkutano wa tano wa mwaka wa kujadili sera za jamii na mahusiano yake kwenye mabadiliko ya kiuchumi nchini Tanzania na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Philemon Luhanjo katika mkutano wa siku moja wa kujadili sera za kijamii zinavyoweza kusaidia kubadilisha uchumi wa Tanzania, mkutano ambao uliandaliwa na ESRF. Luhanjo alisema ni vyema Serikali inapokuwa inatunga sera ihakikishe zinakuwa na faida...

UN NA EU YAWANOA MABALOZI 50 WA MALENGO YA DUNIA IRINGA

UMOJA wa Ulaya (EU) na Umoja wa Mataifa (UN) wameweka nguvu ya pamoja kuendesha kampeni ya uelewa wa malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) nchini Tanzania. Wakiwa Mkoani Iringa wamepata nafasi ya kuzungumza na wanachuo 1,000 kutoka vyuo vikuu vya Iringa na Ruaha kwenye semina iliyoelezea malengo ya dunia ambayo ni sehemu ya ajenda 2030 ya maendeleo endelevu duniani ambapo kati ya hao, vijana 50 wamepata semina ya mwongozo wa kuwa mabalozi wa malengo hayo (Global Goals Champions). Kampeni hiyo imelenga kuwafanya vijana waelewe malengo 17 ya dunia ambayo kwa sasa yana mwaka mmoja tangu yapitishwe na kuwatanabaisha wajibu wao katika kufanikisha utekelezaji wake ndani ya mazingira ya Tanzania.  Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa...

FAHAMU JINSI FEDHA ZA TETEMEKO LA ARDHI MKOANI KAGERA ZILIVYOTUMIKA

Na Mathias Canal Ndugu zangu kama ambavyo tunakumbuka Tarehe 10/09/2016 majira ya saa 9 na dakika 27 Alasiri maeneo ya Kanda ya ziwa hasa Mkoani Kagera kulitokea tetemeko la ardhi linalokadiriwa kuwa na ukubwa wa 5.9 katika vipimo vya Richter ambapo Kitovu cha tetemeko hilo ni kwenye makutano ya latitudo 10 06’ na longitudo 31055’ eneo ambalo ni kilomita 20 kaskazini mashariki mwa kijiji cha Nsunga na kilomita 42 kaskazini magharibi mwa mji wa Bukoba na Kitovu hicho kilikuwa kilomita 10 chini ya ardhi kwenye eneo hilo. Tetemeko hilo la ardhi liliacha familia kadhaa zikiwa na huzuni kubwa kwa kuwapoteza ndugu, jamaa na rafiki zao ambapo idadi ya watu waliofariki walikuwa ni 17 huku watu 560 wakipatiwa matibabu kutokana na...

SBL yatoa saruji ya 10m/- kwa waathirika wa tetemeko Kagera

Meneja Usalama wa SBL, Sebastian Kalugulu  akimkabidhi  Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu baadhi ya mifuko ya saruji 500 yenye thamani ya shilingi milioni 10 kwa wahanga wa janga la tetemeko la ardhi lililotoa mkoani Kagera.Makabidhiano hayo yalifanyika  Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera mjini Bukoba mapema leo. Meneja Usalama wa SBL, Sebastian Kalugulu  akitoa maelezo kwa mkuu wa mkoa wa Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu mara baada ya makabidhiano ya mifuko ya saruji 500 yenye thamani ya shilingi milioni 10 kwa wahanga wa janga la tetemeko la ardhi lililotoa mkoani Kagera.Makabidhiano hayo yalifanyika  Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera mjini Bukoba mapema leo. Mkuu...

MADAKTARI NCHINI WAMETAKIWA KUITISHA MIKUTANO YA KIJAMII ILI KUJADILI MAGONJWA

Katibu Mtendaji wa Chama cha Afya ya Jamii Tanzania (TPHA), Fabian Magoma  (kulia), akizungumza katika Kongamano la 33 la siku tano la Chama cha Afya ya Jamii Tanzania (TPHA) linaloendelea Hoteli ya Kebby Mwenge jijini Dar es Salaam leo asubuhi. Kushoto ni  Mwenyekiti wa TPHA anayemaliza muda wake, Daktari Bingwa  Elihuruma Nangawe. Dk. Manase Frank akitoa mada kwenye kongamano hilo.  Profesa Andrew Swai akitoa mada.  Wadau wa sekta ya afya wakifuatilia kwa karibu mada zilizokuwa zikitolewa katika kongamano hilo.  Kongamano likiendelea.  Dk. Andronicus Aloyce Rwelamila kutoka Hospitali ya Tumbi Kibaha (kushoto) na Muuguzi wa Hospitali hiyo, Mary Gowele wakiwa kwenye kongamano...

Page 1 of 69412345Next
Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More