Friday, October 28, 2016

AKAUNTI ZA LAKE FM MWANZA NA WAFANYAKAZI WAKE ZATOWEKA HEWANI

Ikiwa yamebaki masaa machache kuelekea kwenye show ya Usiku wa Mshike Mshike iliyoandaliwa na Lake Fm redio ya Jijini Mwanza, akaunti ya Instagram ya redio hiyo imevamiwa na watu wanaosadikika kuwa ni wahuni wa mtandaoni. "Siku hizi mitandao ya kijamii ina nguvu sana hususani kwenye kusambaza habari, hivyo nadhani wameamua kuingilia akaunti yetu baada ya kuona namna ambavyo tunaitangaza show ya Usiku wa Mshike Mshike inayofanyika leo". Uongozi wa Lake Fm umefafanua na kuongeza; "Tunapenda kuwaambia Wananzengo wetu kwamba show hiyo itafanyika kama kawaida na tayari Khadija Omar Kopa amewasili Jijini Mwanza kwa ajili ya kuwapa burudani hivyo wasishtuke kutoona posts zetu kwenye mtandao wa Instagram kwani tunapatikana Facebook na Twitter @lakefmmwanza". Mbali...

TAARIFA YA HOSPITALI KWA NAIBU WAZIRI – WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO MHE. DKT HAMISI KIGWANGALLA (MB) OKTOBA 27, 2016 KATIKA HAFLA YA UZINDUZI WA BODI YA HOSPITALI YA TAIFA YA MAGONJWA YA KUAMBUKIZA – KIBONG'OTO

Mhe. Naibu Waziri Dkt Hamisi  Kigwangalla (MB) – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe.  Ndugu Onesmo Buswelu, Mkuu wa Wilaya (SIHA) Dr Said Egwaga, Mwenyekiti wa Bodi ya Hospitali ya Magonjwa ya Kuambukiza Kibong'oto Dr Best Magoma, Mganga Mkuu wa Mkoa. Bwana Saimon Msuya, Katibu wa Mkoa (TUGHE) Wadau wa Maendeleo (WHO, USAID, CDC-EGPAF, KNCV) mliopo hapa Viongozi kutoka KCMC, Chuo Kikuu cha Nelson Mandela na CEDHA Mwenyekiti wa CCM (Wilaya) na viongozi wote wa chama Tawala na Serikali Viongozi wa vyama vya upinzani Wageni waalikwa Wanahabari Mabibi na Mabwana Mhe. Mgeni Rasmi,  Awali ya yote kwa niaba ya Wafanyakazi wa Taasisi ya Magonjwa ya Kuambukiza ya Kibong'oto napenda...

MAMLAKA YA MAJI SAFI NA USAFI WA MAZINGIRA MJINI MOSHI (MUWSA) YAONGEZA VYANZO VIWILI VYA MAJI

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya maji safi na usafi wa Mazingira mjini Moshi,Prof Faustine Bee (kushoto) akimuongoza Waziri wa Maji na Umwagiliaji ,Mhandisi Gerson Lwenge kuelekea katika chanz cha Mkashilingi kilichopo wilyani Hai kwa ajili ya uzinduzi, kulia kwa Waziri ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA).Joyce Msiru. Waziri wa Maji na Uwagiliaji ,Mhandisi Gerson Lwenge akizungumza wakati wa uzinduzi wa chanzo cha maji cha Mkashilingi kilichopo  wilayani Hai mkoani Kilimanjaro. Baadhi ya wananchi waliohudhuria uzinduzi huo wakimsilikiliza Waziri wa Maji na Umwagiliaji (hayupo pichani) wakati wa uzinduzi wa chanzo cha Mkashilingi. Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Said Meck...

Saturday, October 22, 2016

KONGAMANO LA SAUTI YA MWANAMKE KUWAWEKA PAMOJA WANAWAKE JIJINI MWANZA KUJIFUNZA NA KUPATA BURUDANI.

Kongamano la Sauti ya Mwanamke ambalo limeandaliwa na Kampuni ya CHOCOLATE PRINCES inayoandaa kipindi cha THE MBONI SHOW chini ya mtangazaji wake Mboni Masimba, kinachoruka TBC1, litawakutanisha wanawake wengi Jijini Mwanza kupata elimu ya kujikwamua kiuchumi pamoja na kupata burudani. Ni Jumapili tarehe 06.11.2016 katika Ukumbi wa Gold Crest Hotel kuanzia majira ya saa kumi alasiri kwa kiingilio cha shilingi elfu arobaini pamoja na chakul...

HUDUMA YA MCHUNGAJI DANIEL KULOLA WA KANISA LA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA YAFANA MKOANI DODOMA.

Huduma ya injili iliyofanywa na mchungaji kiongozi wa Kanisa la "EAGT Lumala Mpya Internationa Church " lililopo Sabsaba Ilemela Jijini Mwanza, Dkt.Daniel Moses Kulola (pichani), mkoani Dodoma imekuwa ya kufaana na watu wengi wameokoka na kubarikiwa. Ni katika mkutano wa injili ulioandaliwa na kanisa la Siloam EAGT Ipagala mkoani Dodoma kwa juma zima ambapo unatariwa kufikia tamati kesho Oktoba 23, 2016. Picha na Jorum Samwel Mchungaji Dkt.Daniel Kulola, akiendelea na huduma ya maombezi mkoani Dodoma Wengi waliponywa na wanaendelea kuponywa kwa jina la Yesu, vifungo vilivyowatesa kwa muda mrefu. Mchungaji Dkt.Daniel Kulola, akifanya maombezi mkoani Dodom...

PIKIPIKI YAZUA HOFU BAADA YA KUTELEKEZWA MWAKA MZIMA JIJINI DAR ES SALAAM, UKIIKARIBIA, IKIIGUSA INAJIWASHA POLISI WAGWAYA KUIPELEKA KITUONI

 Mwananchi akipita kwa kuikwepa pikipiki yenye namba za usajili T 684 CJZ aina ya Fokon iliyotelekezwa kwa zaidi ya mwaka mmoja katika Kituo cha waendesha bodaboda cha Maganga Veterinary Dar es Salaam.  Mwonekano wa pikipiki hiyo kwa nyuma. Pikipiki hiyo ikiwa katika kijiwe hicho cha  Veterinary Maganga Temeke jijini Dar es Salaam. Na Dotto Mwaibale PIKIPIKI yenye namba za usajili T 684 CJZ aina ya Fokon iliyotelekezwa kwa zaidi ya mwaka mmoja katika kituo cha waendesha bodaboda cha Maganga Veterinary Temeke jijini Dar es Salaam inazua hofu kwa wananchi na hata kwa askari polisi ambao wameshindwa kuipeleka kituoni. Imeelezwa kwamba pikipiki hiyo iliegeshwa katika eneo hilo na mtu mmoja ambaye alifika nayo akiwa...

WANAFUNZI WALIOHITIMU DARASA LA SABA 1993 SHULE YA MSINGI NYAKATO JIJINI MWANZA WAIKUMBUKA SHULE YAO.

Baadhi ya Wanafunzi waliohitimu darasa la saba mwaka 1993 (1987-1993) Shule ya Msingi Nyakato Jijini Mwanza (kushoto), wakimkabidhi Afisa Mtendaji wa Kata ya Muhandu ilipo shule hiyo, vifaa mbalimbali vya kurudufu taarifa ambavyo ni printa pamoja na kompyuta walivyovitoa kwa ajili ya shule yao hii leo.  Mbali na vifaa hivyo, pia wanafunzi hao ambao miongoni mwao ni wafanyabiashara na watumishi wa taasisi mbalimbali za serikali na binafsi, wametoa vifaa vya michezo kwa ajili ya wanafunzi wa shule hiyo ikiwemo mipira na jezi, pamoja na zawadi mbalimbali kwa ikiwemo kompyuka kwa baadhi ya waliokuwa waalimu wao kipindi hicho. Na BMG Baadhi ya Wanafunzi waliohitimu mwaka 1993 (1987-1993) Shule ya Msingi Nyakato Jijini Mwanza (kushoto),...

BENKI YA NMB MLIMANI CITY YATOA SEMINA FUPI KWA WATEJA WAKE KUHUSU HUDUMA WAZITOAZO

Wafanyakazi wa Benki ya NMB Tawi la Mlimani City wakijitambulisha kabla ya kuanza kwa semina hiy...

Page 1 of 69412345Next
Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More