Saturday, October 31, 2015

ASKARI WA KIKOSI CHA UPELELEZI AJIUA KWA KUJIPIGA RISASI SHINGONI

https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=150bdff8c446975b&attid=0.1&disp=inline&realattid=file0&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ_joySY0ohOhzwcnrrpp7U7iluESV3i8d4MV5-jIC5JtSYWT0605cQkDqR9T0FcZRtt4ycxzHRS27j4XtDq8XwxlO65rJpgWbSay6_iHnNEg8oy8WaZDsTe9Q-z3RZ7tYUCuWK2gJrqYVCZRzifcn15kGyOxWFe0jig8YkW9TJEvuqTHP7nfFyLC4GHRWWV499nP7pfS4mXZDWbcGbF1TjUixB3wXxOVY38Zag6iVurwHG8Mq__7ZwdpTXm-lAEnMzzcF9FEStXPYfLeaoj_RXht-_EroaBGCJZQhzDIfAPPQEf6OaLhzlmilhgZdWKZ68e4WFdmG3ZkXhM1AxIDkJmnEltc1cxnMY4YXvuCYEg1MPtj8ZyjJHkETDVmU7uQqVJQsB0NQ3VLGHLYuay2_t50R0QNlq5upoZ_DGvuOuz7wSpG5UAdttt5lQ_7dMtrcFN_quIiZFjwf3eJKGRTXsJrgwQimR5iID6Ko1OR4RRfaAg0hAPZkN8rrmbUDiIhSC9deguKOEqQ6TJNsp1gXdiKoCI0hIJAtRp79E62vv6DuO4qx014graBOpJVyP1Y_BUDV3VaOWm5zaWum6aEvV5omACCBWcunslLySQTqexpZUzTUYiZLZBcf4

 
Askari wa kikosi maalumu cha kupambana na ujambazi mkoa wa Iringa Pascal Shila (30) pichani amejiua kwa kujipiga risasi kichwani kutokana na msongo wa mawazo.

Askari mwenye namba G.343D/C Pashal James Shila wa Ofisi ya RCO-Kikosi cha Anti Robbery amejiua kwa kujipiga risasi na mwili wake kukutwa kwenye jengo bovu la ghorofa la mjerumani lilipo nyuma ya kituo cha polisi.

Akizungumza na mwangaza wa habari blog wakati wa kuaga mwili wa marehemu kwenye kituo kikuu cha polisi Manispaa ya Iringa, Kamanda wa polisi mkoa wa Iringa Ramadhani Mungi alisema tukio hilo lilitokea jana kati ya saa tisa na kumi jioni.

Kamanda Mungi alisema askari huyo kutoka ofisi ya upelelezi mkoa wa Iringa (RCO) alichukua silaha aina ya ya SMG saa sita mchana kutoka kwenye ghala ya kuhifadhia silaha kwa madai kuwa yeye na wenzake wanakwenda kufanya kazi ya dharura huko Ifunda.

Alisema baada ya hapo hakuonekana na saa saba mkewe alikwenda kwenye ofisi ya RCO kupeleka ujumbe alioandikiwa na mumewe kuwa amtunzie watoto kwa kuwa anawapenda sana.

Kamanda Mungi alisema kufuatia ujumbe huo askari wenzake walianza kumtafuta na baadaye kukuta mwili wake ukiwa kwenye jengo lililopo nyumba ya kituo kikuu cha polisi akiwa amejipiga risasi shingoni karibu na kidevuni na kabla hap alimtumia mkwewe meseji aliomba amtunzie watoto wake kwani ana wapenda sana.

Alisema jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi ili kuweza kubaini
chanzo cha tukio hilo na kuwa huenda limesababishwa na msongo wa mawazo aliokuwa nao marehemu.

Alisema tukio hilo limewaumiza askari sote kwa kuwa alikuwa anachukia uhalifu kwa dhati na kuwa mwili wake utasafirishwa kesho kwenda nyumbani kwao wilayani Kyela katika kijiji cha Ilolo kwa ajili ya mazishi.

Aidha alisema matukio kama hayo yanawakuta askari kwa kuwa nao ni sehemu ya jamii na kuwa jeshi la polisi hutoa mafunzo ya jinsi ya kupambana na msongo wa mawazo kwa askari wao.

Hata hivyo habari ambazo hazijathibitishwa na kamanda wa jeshi la
polisi mkoa wa Iringa zinaeleza kuwa chanzo cha msongo wa mawazo.

Uchunguzi awali unaonyesha kuwa kulikuwepo na ugomvi baina yake na mkewe usiku jana.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More