Friday, March 6, 2015

JESHI LA POLISI KAGERA LAANZA KUWANUSURU ALBINO NA KIFO...LAANZA KUWASAKA WAGANGA NYUMBA HADI NYUMBA

JESHI la Polis mkoani Kagera limeanza opereisheni ya kuwasaka waganga na wapiga ramli,ikiwa ni harakati za kutokomeza vitendo vya mauaji vinavyodaiwa kusababishwa na baadhi ya waganga wa kienyeji kwa kutoa ushauri kwa waharifu.
Opereisheni hiyo endelevu imeanza  Machi 4 kwa kuwahusisha katika wilaya ya Biharamulo kwa kuwashirikisha askari Polis pamoja na kikosi cha Mali Asili,nakufanikiwa kuwakamata jumla ya wapiga ramli 18 waliokuwa katika viji vya kata nne za Kabindi,Nyamigogo,Runazi na Nyabizozi zote zikiwa ndani ya tarafa Nyarubunga wilayani Biharamulo.
 
Kamanda wa jeshi la Polis mkoani hapa Hennry Mwaibambe,akiongea katika tukio hilo katika kituo cha Polis Kabindi,Opereisheni hiyo imeanza ili kuhakikisha vitendo vya mauaji na kishirikina vinatokomezwa,kwani vitendo vya mauaji vimekuwa vikishamiri katika maeneo ya wilaya ya Biharamulo.
 
Kamanda Mwaibambe alisititiza kuwa opereisheni hiyo si nguvu ya soda,bali itakuwa endelevu kwani wapo baadhi ya wahusika na vitendo vya uharifu wa mauaji wamekuwa wakihusika katika mauaji ya binadamu kwa kutafuta viungo vya binadamu hasa kwa kuwaua binadamu wenye ulemavu wa ngozi(Albino)hivyo jeshi la Polis mkoani Kagera kwa kushirikiana na maafisa wanyama poli poli la  Burigi,watahakikisha wanapambana na hali hiyo.
 
"Jeshi letu limejipanga kuhakikisha linalinda watu hawa(wenye ulemavu wa ngozi)tunaomba jamii iwe tayari kuwafichua wale wote wenye dhamira na kujihusisha katika vitendo hivyo vya kijama,vitendo hivi vinalitia doa taifa letu,lazima tuhakikishe tunatokomeza hali hii!natoa onyo kwa wale wanajihusisha na shughuli ya upigaji ramli na uganga wa kienyeji.tabia hii haivumiliki tena!"alisisitiza Kamanda Mwaibambe.
 
Aliongeza mara baada ya kukamilika taratibu za mahojiano,watuhumiwa wote 18 waliokamatwa watafikishwa mahakamani ili kujibu mashitaka yaliyo mbele yao.
 
Kwa upande wa Afisa Wanyama Poli Poli la Burigi Jimmy Mushana,alisema opereisheni hiyo imefanikiwa kuwakamata waganga wa kienyeji hao waliojihusha kupiga ramli na kumbaini walikuwa wana Nyara za serikali kinyume cha sheria za nchi.
 
Alisema nyara mbalimbali zilizotokana na wanyama 39 na ndege mmoja,ambazo thamani yake ni shilingi milion 60,464,250/=zilipatikana kutokana opereisheni hiyo.
 
Wakati huo huo,jeshi la Polisi linaendelea kumhifadhi mtoto Mwenye ulemavu wa ngozi(Albino)aliyedaiwa kutorokwa na mzazi(baba) wake aliyejulikana kwa jina la Pius Simon(22)ambaye alitokomea kusikojulikana kwa kisingizio kuwa alienda kuchoma mkaa.
 
Mtoto huyo Meshack Pius (3)aliachwa kwa babu yake aliyejukana kwa jina la Simon Kagobe(70)mkazi wa Nyabizozi,tangu mnamo Fbruari 18 na kuwepo hali ya hatari kwa kijana huyo,ambaye babu yake ilibidi amsalimishe katika kituo cha Polis Kabindi kwa kuhofia mtoto huyo kufanyiwa vitendo vya kinyama.
 
Kwa mujibu wa Kamanda Mwaibambe,mtoto huyo Meshack bado anahudumiwa na jeshi la Polis huku akiomba wasamalia wenye nia njema kujitokeza kumsaidia mtoto huyo hasiye na hatia wakati utaratibu wa serikali unatafuta jinsi ya kumsaidia kwani bado anahitaji huduma za malezi licha ya kuwa na akili timamu na afya njema.
 
Tukio la jeshi hilo kupokea watoto wenye ulemavu wa ngozi ni pili ndani ya miezi miwili iliyopita mwaka huu,kwani mnamo Januari mwaka huu,mtoto mwingine aliterekezwa kituoni hapo na kutafutiwa mazeneo ya kuishi kwa kushirikiana na uongozi wa mkoa.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More