NA MWANDISHI WETU, IRINGA
MGOMBEA wa nafasi ya Ubunge kwa tiketi ya CCM, Mwanahabari Frank Kibiki ameahidi kushirikiana na wadau wa soka kupandisha daraja timu ya soka ya Lipuli ya mjini Iringa iwapo atapewa ridhaa ya kupeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi mkuu ujao.
Akizungumza wakati wa kampeni za kujinadi zilizofanyika katika eneo la Kihesa kilolo, mjini Iringa Kibiki alisema michezo ni fursa ambayo inaweza kuinua uchumi wa mkoa wa Iringa endapo itapatiwa kipaumbele.
Alisema ikiwa atapewa ridhaa ya kuwa mbunge, atakaa chini na wadau wa soka wa manispaa ya Iringa na kuweka mikakati madhubuti ili kuhakikisha wananchi Lipuli inapanda daraja.
“Ndugu zangu, Lipuli ikipanda daraja uchumi wa Iringa mjini utakuwa kwa sababu...