Monday, January 12, 2026

WANAFUNZI VYUO VIKUU WAMETAKIWA KUJIEPUSHA NA NDOA ZA REJAREJA, DKT MSOWOYA

Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa, Dkt Tumaini Msowoya akiongea na wanafunzi wa chuo kikuu cha Iringa wakati wa kuwakaribisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza wa masomo katika chuo hicho.
Baadhi ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Iringa wakimaliza Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa, Dkt Tumaini Msowoya wakati akitoa hotuba yake 
Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa, Dkt Tumaini Msowoya akikabidhi kiasi cha shilingi milioni mbili kwa uongozi wa chuo kikuu cha Iringa zilizotolewa na Dikson Mwipopo, Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa, kwa ajili ya kuwaunga mkono wanafunzi hao. 


Na Fredy Mgunda, Iringa.


Wanafunzi wa vyuo vikuu wametakiwa kujiepusha na ndoa za rejareja,makundi ya hovyo yenye viashiria vya kuharibu masomo na maisha kwa wanafunzi wenye ndoto ya kuja kulitumikia taifa la Tanzania na nje ya Tanzania.

Akizungumza wakati kuwakaribisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza chuo kikuu cha Iringa,Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa, Dkt Tumaini Msowoya alisema kuwa wanafunzi wanapaswa kuepukana na ndoa za rejareja, makundi ya hovyo na kuwa wazalendo kwa ajili ya maisha yao.


Dkt Msowoya amesema baadhi ya wanafunzi hujikuta wakitumbukia kwenye ndoa za rejareja na kusahau lengo la masomo kutokana na tamaa za kifedha na kuishi maisha mazuri chuo jambo ambalo limekuwa likipoteza dira ya masomo kwa wanafunzi wengi.


"Najua mna miaka zaidi ya 18 hivyo sio watoto Kwa mujibu wa kawaida lakini je, ndoa ndiyo imekuleta chuoni? Wazazi wako wanajua umeoa au kuolewa huku?" amesema na kuongeza, Dkt Msowoya

"Niliwahi kufanya utafiti kuhusu maisha ya wanafunzi wa vyuo vikuu nikagundua wengi wanaishi na wenza ilhali familia zao hazijui. Hii ni hatari,"

Dkt. Msowoya aliwahimiza wanafunzi kuipenda nchi yao, kusoma kwa bidii na kuepuka makundi yenye viashiria hasi katika masomo na maisha kwa ujumla.

Katika hafla hiyo, alitoa mchango wa shilingi milioni mbili (2,000,000) zilizotolewa na Dikson Mwipopo, Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa, kwa ajili ya kuwaunga mkono wanafunzi hao. 


Sunday, January 11, 2026

USHIRIKI WA WANANCHI WAIMARISHA UPANDAJI MITI SAO HILL

 
Wananchi wanaozunguka Shamba la Miti Sao Hill wameendelea kunufaika kielimu na kiuchumi kupitia ushiriki wao katika shughuli za uchukuaji miche ya miti zinazofanyika katika bustani za miche zilizopo Tarafa ya Kwanza Irundi na Tarafa ya Tatu Ihalimba.
Wananchi wanaozunguka Shamba la Miti Sao Hill wameendelea kunufaika kielimu na kiuchumi kupitia ushiriki wao katika shughuli za uchukuaji miche ya miti zinazofanyika katika bustani za miche zilizopo Tarafa ya Kwanza Irundi na Tarafa ya Tatu Ihalimba.
Wananchi wanaozunguka Shamba la Miti Sao Hill wameendelea kunufaika kielimu na kiuchumi kupitia ushiriki wao katika shughuli za uchukuaji miche ya miti zinazofanyika katika bustani za miche zilizopo Tarafa ya Kwanza Irundi na Tarafa ya Tatu Ihalimba.



Na Fredy Mgunda, Mufindi.

Wananchi wanaozunguka Shamba la Miti Sao Hill wameendelea kunufaika kielimu na kiuchumi kupitia ushiriki wao katika shughuli za uchukuaji miche ya miti zinazofanyika katika bustani za miche zilizopo Tarafa ya Kwanza Irundi na Tarafa ya Tatu Ihalimba.

Shughuli hizo ni sehemu ya mpango endelevu wa upandaji miti unaotekelezwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa lengo la kuendeleza misitu ya kupandwa, kuongeza uzalishaji wa rasilimali za misitu na kuimarisha uhifadhi wa mazingira.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Msaidizi wa Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Miti Sao Hill, PCO Said Singano, alisema uchukuaji wa miche unafanyika kwa kuzingatia taratibu na kanuni za kitaalamu ili kulinda ubora wa miche.

“Tunasisitiza miche ichukuliwe kwa uangalifu mkubwa ili isiharibu mizizi, kwa sababu ubora wa miche ndiyo msingi wa mafanikio ya upandaji miti mashambani,” alisema Singano.

Shughuli hizo pia zimeongeza uelewa wa wananchi kuhusu mchango wa Shamba la Miti Sao Hill katika uhifadhi wa mazingira, mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabianchi na upatikanaji endelevu wa mazao ya misitu kwa manufaa ya Taifa.

Mmoja wa wananchi walioshiriki zoezi hilo, Bw. Joshua Ng'umbi kutoka Kijiji cha Igowole Wilaya ya Mufindi, alisema ushiriki wake umemsaidia kuongeza kipato na kupata ujuzi mpya katika shughuli za misitu.

“Mbali na kupata ajira, nimejifunza kuchagua miche bora na namna sahihi ya kupanda miti ili iweze kuota vizuri na kukua kwa ubora unaoweza kuleta kipato kizuri wakati wa uvunaji,” alisema Bw. Joshua.

Kwa ujumla, zoezi la uchukuaji miche katika Tarafa za Irundi na Ihalimba limeendelea kuleta manufaa makubwa kwa Shamba la Miti Sao Hill na wananchi kwa kuimarisha juhudi za upandaji miti, kutoa ajira na kukuza uelewa wa masuala ya misitu na uhifadhi wa mazingira.

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More