Tuesday, December 9, 2025
MAFUNZO YA OSHA YAWANUFAISHA ZAIDI YA WANAWAKE 200
Saturday, November 22, 2025
DC NYUNDO AWASIMAMISHA KAZI VIONGOZI WA KIJIJI KWA TUHUMA ZA UUZAJI ARDHI
Na Fredy Mgunda,Kilwa Lindi.
Mkuu wa Wilaya ya Kilwa, Mhe. Mohamed Nyundo, amewasimamisha kazi viongozi wa Serikali ya Kijiji cha Nanjirinji A, Kata ya Nanjirinji, ili kupisha uchunguzi wa tuhuma za ugawaji na uuzaji wa ardhi kinyume cha utaratibu pamoja na matumizi mabaya ya mali za umma.
Hatua hiyo imechukuliwa baada ya wananchi kuwasilisha malalamiko mbele ya Mkuu wa Wilaya, wakimtuhumu Mwenyekiti Hamadi Makakala na Mtendaji Mbaruku Malukula kwa kufanya maamuzi makubwa bila kuwashirikisha wanajamii, kinyume na misingi ya utawala bora.
Akizungumza baada ya kusikiliza malalamiko hayo, DC Nyundo alisema kuwa ameunda kamati maalumu ya uchunguzi itakayopitia tuhuma hizo kwa kina na kutoa mapendekezo yatakayoiwezesha Serikali kuchukua hatua stahiki.
“Hatutaacha mwanya kwa mtu yeyote kutumia madaraka vibaya au kudhulumu rasilimali za wananchi. Uchunguzi utafanyika kwa uwazi na hatua kali zitachukuliwa kulingana na matokeo,” alisema Nyundo.
Ameongeza kuwa wananchi wanapaswa kuwa waangalifu dhidi ya taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii, akiwataka kutegemea vyanzo vya uhakika ili kuepuka kupotoshwa.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa, Hemed Magaro, alitoa ufafanuzi kuhusu utofauti kati ya kuuza ardhi na kugawa ardhi kwa utaratibu maalumu, akisisitiza kuwa ardhi ya kijiji haiwezi kuuzwa bila kufuata sheria, taratibu na ridhaa ya mkutano mkuu wa kijiji.
Thursday, November 20, 2025
RC KHERI AWAAGIZA TFS KUONGEZA ELIMU YA UHIFADHI KWA JAMII.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, ameipongeza Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa kazi ya kulinda rasilimali za misitu na nyuki, huku akiutaka wakala huo kuongeza kasi ya kutoa elimu ya uhifadhi kwa wananchi ili kukabiliana na changamoto za kimazingira zinazoongezeka nchini.
Ametoa wito huo wakati wa ziara yake katika Shamba la Miti Sao Hill, wilayani Mufindi, akiwa ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Dkt. Linda Salekwa, na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo.
Akizungumza na wahifadhi, Mkuu wa Mkoa amesema nidhamu na weledi ndani ya TFS ni sharti kuzingatiwa ili kuhakikisha sera na taratibu za uhifadhi zinatekelezwa kikamilifu.
“Nidhamu ni msingi wa ufanisi. Kama wahifadhi wa misitu yetu, ni lazima mjikite kwenye uwajibikaji na kutanguliza maslahi ya Taifa,” amesema James.
Amesifu uhusiano mzuri baina ya TFS na wananchi wanaoishi pembezoni mwa shamba hilo, akisema ushirikiano huo unaimarisha ulinzi wa misitu na kuongeza uelewa wa jamii kuhusu umuhimu wa rasilimali hizo.
“Kulinda misitu ni jukumu la Taifa zima. Endeleeni kutoa elimu mara kwa mara ili jamii ielewe kuwa misitu ni uchumi, ni mazingira, na ni uhai,” amesema.
Mhe. James ametahadharisha kuwa ukame unaoikumba nchi katika miaka ya hivi karibuni unachangiwa kwa kiasi kikubwa na uharibifu wa misitu, hali inayosababisha kupungua kwa mvua na kuongezeka kwa joto.
“Ukame unaongezeka kwa sababu tumeshindwa kuhifadhi misitu. TFS iendelee kuhamasisha upandaji na utunzaji wa miti bila kuchoka,” amesisitiza.
Awali, Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Dkt. Linda Salekwa, amesema Shamba la Miti Sao Hill limekuwa msaada mkubwa kwa jamii kwa kushiriki miradi mbalimbali ya maendeleo.
“TFS imetoa madawati, kujenga madarasa, mabweni, bwalo la chakula na kuendelea kusaidia jamii kwenye miradi ya kijamii. Ni taasisi inayowajibika,” amesema.
Kwa upande wake, Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Miti Sao Hill, PCO Tebby Yoramu, amesema TFS imeendelea kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi kuhakikisha misitu inatumika kwa manufaa bila kuhatarisha uendelevu.
Ametaja shughuli zinazotekelezwa kuwa ni pamoja na ufugaji nyuki, uvunaji wa utomvu, uvunaji endelevu wa miti, na utoaji wa elimu kwa wananchi wa maeneo jirani.
Friday, October 24, 2025
OSHA YADHAMIRIA KUONGEZA UELEWA WA WADAU KUPITIA VYAMA VYA WAFANYAKAZI
Tuesday, October 7, 2025
SERIKALI YAENDELEA KUWAUNGA MKONO WAKULIMA WA PAMBA KASULU
Mkuu wa wilaya ya Kasulu Kanali Isaac Mwakisu Serikali inaendelea kuleta unafuu kwa wakulima wa zao la pamba wilayani Kasulu kwa kuwapatia pembejeo muhimu kama mbegu, viuatilifu na vinyunyizi, hatua iliyochochea kilimo chenye tija na matokeo chanya.
Serikali imeendelea kuleta unafuu kwa wakulima wa zao la pamba wilayani Kasulu kwa kuwapatia pembejeo muhimu kama mbegu, viuatilifu na vinyunyizi, hatua iliyochochea kilimo chenye tija na matokeo chanya.
Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Mhe. Kanali Isaac Mwakisu, amesema hayo leo Jumanne, Oktoba 7, 2025, katika Kata ya Asante Nyerere, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Pamba Duniani yaliyokwenda sambamba na uzinduzi wa msimu mpya wa zao hilo kwa mwaka 2025/2026.
Amesema maadhimisho hayo ni fursa muhimu kwa Serikali, wanunuzi na vyama vya msingi kujadili maendeleo ya zao hilo na kuweka mikakati ya kuliboresha zaidi.
Aidha, amewataka wananchi kutumia kipindi hiki cha kampeni kusikiliza sera za wagombea wa vyama mbalimbali ili siku ya uchaguzi, Oktoba 29, watumie haki yao ya kikatiba kuchagua viongozi wanaowataka.
Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Theresia Mtewele, amesema maadhimisho ya Siku ya Pamba Duniani yaliyoanzishwa mwaka 2019 yanalenga kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa zao hilo kama chanzo kikuu cha kipato kwa wakulima wadogo na wafugaji vijijini.
Mkulima wa Pamba, Joel Kingi, ameishukuru Serikali kwa juhudi zake za kuhamasisha kilimo hicho, akieleza kuwa idadi ya wakulima imeongezeka kutoka 50 hadi kufikia 1,000 kutokana na upatikanaji wa pembejeo na viuatilifu.
Awali, Mkaguzi wa Pamba wa Wilaya hiyo, Michael Kiliga, amesema wilaya inashirikiana na vyama vya ushirika (AMCOS) nane kusambaza pembejeo kwa wakulima bure, hatua inayochangia kuimarisha uzalishaji wa zao hilo.
CCM WAFANYA BONANZA KUHAMASISHA WANANCHI KUSHIRIKI UCHAGUZI KWA AMANI
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimeandaa Bonanza Maalum katika Jimbo la Segerea, mkoani Dar es Salaam, kwa lengo la kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, kwa njia ya amani na utulivu.
Mgeni rasmi katika bonanza hilo alikuwa Mwenyekiti wa UWT Taifa, Mary Pius Chatanda, ambaye aliwataka wananchi kutumia haki yao ya kidemokrasia kwa kupiga kura kwa amani, akisisitiza kuwa kiongozi anayechaguliwa leo ndiye atakayekuwa na mamlaka ya kuleta maendeleo kwa miaka mitano ijayo.
“Kupiga kura ni haki ya msingi kwa kila Mtanzania. Tuchague viongozi wanaotuletea maendeleo ya kweli,” alisema Chatanda.
Akimnadi mgombea urais wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Chatanda alisema kuwa serikali ya awamu ya sita imeitekeleza ilani ya CCM ya mwaka 2020-2025 kwa asilimia 100, na hivyo anastahili kupewa tena ridhaa ya kuendelea kuongoza nchi.
Aidha, alitoa wito kwa wananchi kumchagua mgombea wa CCM katika nafasi ya urais, ubunge na udiwani ili kuimarisha juhudi za maendeleo nchini.
Kwa upande wake, mgombea ubunge wa Jimbo la Segerea, Bonnah Kamoli, alisisitiza kuwa mojawapo ya sera zake ni kuhamasisha mazoezi ya mara kwa mara kwa wananchi, ili kuboresha afya ya mwili na akili.
“Afya bora ni msingi wa maendeleo. Tukifanya mazoezi tutakuwa na nguvu za kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa taifa,” alisema Kamoli.
Kamoli aliwaomba wakazi wa Segerea kumpigia kura nyingi pamoja na kumpa kura ya kishindo Dkt. Samia Suluhu Hassan, ili kuendeleza kasi ya maendeleo katika jimbo hilo.
Naye Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (MNEC) na Mratibu wa Kampeni za CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Kasesela, aliwataka wananchi kupuuza wanasiasa na wanaharakati wanaotumia mitandao ya kijamii kuchochea vurugu na hofu wakati huu wa uchaguzi.
“Wachochezi wengi wapo nje ya nchi. Vurugu zikitokea, ni Watanzania waliopo hapa ambao watateseka. Amani ni tunu ya taifa letu,tuilinde,” aliongeza Kasesela.
Katika bonanza hilo, wananchi walishiriki katika michezo mbalimbali, burudani, na kupata elimu juu ya umuhimu wa kushiriki uchaguzi kwa njia ya amani.
Sunday, October 5, 2025
MNEC KASESELA AWASIHI WATANZANIA KUSOMA VITABU VYA DINI
Baadhi ya waumini wa dini ya wananchi waliohudhuria kongamano la waislamu kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29 mwaka huu lilofanyika mlimani city jijini Dar es salaam
Baadhi ya waumini wa dini ya wananchi waliohudhuria kongamano la waislamu kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29 mwaka huu lilofanyika mlimani city jijini Dar es salaamNa Fredy Mgunda
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (MNEC) na Mratibu wa Kampeni wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kanda ya Dar es Salaam, Richard Kasesela, amewataka Watanzania kumuabudu Mwenyezi Mungu kila wakati ili waweze kupata amani ya moyo na nafsi.
Akizungumza katika kongamano la Waislamu kuelekea uchaguzi mkuu, Kasesela alisema ni muhimu kwa wananchi kusoma vitabu vya dini mara kwa mara, kwani vinafundisha maadili mema na kuleta baraka katika kazi zao za kila siku.
"Vitabu vya dini vinatufundisha subira, heshima na upendo – misingi ambayo ni muhimu katika maisha na maendeleo ya taifa," alisema Kasesela.
Aidha, aliwaomba viongozi wa dini kuendelea kutoa elimu ya kiroho sambamba na mafunzo ya mbinu za kujikwamua kiuchumi, ili wananchi waweze kujitegemea na kuboresha maisha yao.
Katika hatua nyingine, Kasesela aliwahimiza wananchi wote kumpigia kura kwa wingi Mgombea Urais wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akieleza kuwa amefanya kazi kubwa ya kuleta maendeleo katika kipindi chake cha uongozi.
"Ni wajibu wetu kuonyesha shukrani kwa kumpigia kura Dkt. Samia tarehe 29 Oktoba. Tuonyeshe mshikamano wetu kwa kupitia sanduku la kura," alihitimisha Kasesela.
Tuesday, September 30, 2025
VIONGOZI, WANANCHI WATAKIWA KUSHIRIKIANA KUDHIBITI MOTO MISITUNI
Sunday, September 28, 2025
ELIMU YA USALAMA NA AFYA KAZINI YAWAFIKIA WASIOONA.
Afisa Mafunzo wa OSHA, Bw. Simon Lwaho, akiwasilisha mada kuhusu vihatarishi mahali pa kazi na udhibiti wake kwa wanachama wa Jumuiya ya Wasioona Tanzania (TAB) katika semina ya mafunzo iliyoandaliwa na OSHA kwa kundi hilo.Friday, September 19, 2025
OSHA YAKABIDHI VIFAA CHUO CHA UFUNDI MIRONGO JIJINI MWANZA
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mhe. Amina Makilagi, akiwasilisha hotuba yake wakati wa Bonanza la OSHA la Huduma kwa Jamii (OSHA CSR BONANZA 2025) lililofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Nyakabungo Jijini Mwanza akiwa ni Mgeni Rasmi wa Bonanza hilo.
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mhe. Amina Makilagi na Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda wakimkabidhi Mkuu wa Chuo cha Ufundi cha Mirongo vifaa mbalimbali vya msaada vilivyotolewa na OSHA kukiwezesha chuo hicho. Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na kompyuta, makoti ya usalama na vifaa vya michezo.
Na Fredy Mgunda,Kwanza.
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mheshimiwa Amina Makilagi, amewataka waajiri na wafanyakazi kote nchini kuitekeleza kikamilifu Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi Na. 5 ya mwaka 2003 ili kupunguza au kuondoa kabisa ajali na magonjwa yanayotokana na mazingira duni ya kazi.
Mheshimiwa Makilagi alitoa wito huo jana wakati wa Bonanza la OSHA la Huduma kwa Jamii (OSHA CSR Bonanza 2025) lililofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Nyakabungo, Wilaya ya Nyamagana, Jijini Mwanza. Bonanza hilo lilihusisha shughuli mbalimbali za kijamii na michezo kwa lengo la kuimarisha mshikamano kati ya OSHA na jamii inayohudumiwa, pamoja na kutoa msaada kwa wanafunzi wa Chuo cha Ufundi Mirongo, wakiwemo wenye ulemavu.
Katika tukio hilo, OSHA ilikabidhi vifaa mbalimbali kwa Chuo cha Ufundi Mirongo, vikiwemo kompyuta, vifaa kinga vya usalama kazini, pamoja na vifaa vya michezo kama mipira na jezi za michezo.
Akizungumza kama Mgeni Rasmi, Mheshimiwa Makilagi aliipongeza OSHA kwa juhudi zake za kuhakikisha mazingira salama na yenye afya sehemu za kazi na kuonesha moyo wa huruma kwa makundi maalum katika jamii.
“Nitoe rai kwa waajiri na wafanyakazi nchini kuisoma na kuitekeleza Sheria Na. 5 ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ya mwaka 2003. Sheria hii ikitekelezwa ipasavyo, maeneo ya kazi yatakuwa salama, bila ajali wala magonjwa, hivyo kuongeza tija kazini,” alisema Mkuu wa Wilaya Makilagi.
Aidha, aliihakikishia OSHA ushirikiano wa Halmashauri na Ofisi yake katika kusimamia usajili na ukaguzi wa maeneo ya kazi, sambamba na kutoa ushauri wa kitaalamu juu ya maboresho ya mazingira ya kazi.
Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, alisema Bonanza hilo ni sehemu ya mpango wa taasisi hiyo wa kurudisha kwa jamii (Corporate Social Responsibility) na kwamba msaada uliotolewa kwa Chuo cha Mirongo umetokana na tathmini iliyofanywa na wataalam wa OSHA baada ya kutembelea chuo hicho.
“Tunaamini kuwa kwa kusaidia vyuo vya ufundi kama Mirongo, tunachangia kwa kiasi kikubwa maandalizi ya wataalamu wa baadaye katika fani muhimu za kiufundi na kazi,” alisema Bi. Mwenda.
Kaimu Mkuu wa Chuo cha Mirongo, Bi. Herieth Richard, pamoja na mwanafunzi wa fani ya ushonaji, Bi. Aneth Augustino, waliishukuru OSHA kwa msaada huo ambao wamesema umeongeza ari ya kujifunza na kushiriki katika shughuli za kijamii.
Bonanza hilo lilihusisha michezo ya mpira wa miguu, mpira wa pete, riadha, na michezo ya jadi kama kukimbia kwenye magunia, kukimbia na ndimu kwenye kijiko, rede na kukamata kuku. Washiriki walitoka OSHA na vyuo vya Ufundi vya Mirongo, Nyakato na Kisesa.
Chuo cha Ufundi Mirongo kinamilikiwa na Serikali chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), na hutoa mafunzo ya umeme, useremala, ushonaji na uchomeleaji kwa vijana wakiwemo wenye mahitaji maalum.
Thursday, September 18, 2025
MWENGE WA UHURU WAWEKA JIWE LA MSINGI WODI YA MAMA NA MTOTO MWAMI NTALE
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, Ismail Ali Ussi, ameweka jiwe la msingi katika wodi ya mama na mtoto katika Kituo cha Afya cha Mwami N’tale, kilichopo kata ya Heru, Halmashauri ya Mji Kasulu.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Ussi amesisitiza umuhimu wa wananchi kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu ujao kwa amani, utulivu, na kuchagua viongozi wanaowataka. Amesema kaulimbiu ya Mwenge wa Uhuru mwaka huu inahimiza amani kama msingi wa maendeleo ya taifa.
“Maendeleo tunayoyaona leo ni matokeo ya utulivu na amani inayotamalaki nchini. Hivyo ni wajibu wetu kuilinda na kuithamini hali hii,” alisema Ussi.
Mradi wa ujenzi wa kituo hicho umegharimu kiasi cha Tsh milioni 300, na tayari umekamilika kwa asilimia 100. Utaanza kutoa huduma za afya kwa kina mama na watoto katika eneo la Heru na maeneo jirani.
Kituo hiki kinatarajiwa kupunguza kwa kiwango kikubwa vifo vya mama na mtoto kwa kutoa huduma bora, za karibu, na za uhakika kwa wananchi.
Mwenge wa Uhuru umeendelea kuwa chombo muhimu katika kuhamasisha maendeleo, uwajibikaji, na uzalendo miongoni mwa Watanzania.
Wednesday, September 17, 2025
MWENGE WA UHURU WAZINDUA KITUO CHA POLISI NYAKITONTO KWA AJILI YA KUONGEZA USALAMA






Tuesday, December 09, 2025
mwangaza wa hbari






.webp)

.webp)
.webp)





















.jpg)
.jpg)








